Uchaguzi 2020 SPECIAL THREAD: Taarifa za Kampeni na Sera za Mgombea Urais kupitia CHAUMMA, Hashim Rungwe Sipunda

Inaelekea hujamuelewa Mgombea wetu Urais wa Chauma.

Kifupi anajaribu kuhimiza lishe bora kwa Watanzania huku mkazo ukitiliwa kwa wanafunzi wanaoshinda shuleni muda mrefu bila kupata chakula mchana. Kwa waliosoma zamani wanakumbuka mchana wanafunzi waliweza kupatiwa msosi shuleni, mwanafunzi mwenye njaa hawezi kuwa active darasani.

Lishe bora kwa Watanzania ni muhimu maana itasaidia kuondoa tatizo la udumavu wa miili na akili, unaweza ukawa unakula lakini unajaza tumbo tu na si lishe bora unayokula. Kupitia lishe bora hata shahawa zitokazo kwa mwanaume huwa bora, mshika mimba naye anakuwa strong, kiumbe kitokacho nacho kinakuwa bora.

Chagua Rungwe, chagua Chauma upate lishe bora kwa maendeleo ya familia yako na Taifa letu, tumuunge mkono kwa Mzee wetu ameona jambo muhimu saana.
 
Sisi wafuasi wake tunamuelewa kweli kweli! Na tunamtaka aendelee hivyo hivyo! Nyinyi yule wa kwenu si anatembea na wale wasanii wenzake 100!

Tuone sasa kati ya Ubwabwa Kuku na hayo manyimbo yenu ya matusi na kejeli za kishamba kwa Wapinzani wenu wa kisiasa, kipi kinashibisha.

Rungwe oyeeee!! Chauma oyeee! Ubwabwa oyeee! Bombardier Ziiiiiiii!! Flyovers Ziiiiiii!!!!
 
Kinachoniuma hua hatoi ratiba ya maeneo anayotembelea. Nashauri atoe ratib ya wiki nzima kwa sisi wafuasi wake tujue tunamkuta wapi boss wetu na mahotpot y ubwabwa

Mahotpot yamesheheni ubwabwa kuku, ataweza kugawa kwa makutano wote au ataishia kula na wachache hightable!!
 
Tunatambua umuhimu wa lishe bora, basi wekeni mikakati na sera wezeshi kwa watu kumudu lishe na sio kutembea na shehena na kula hadharani... tuseme mtawagawia wananchi hiyo misosi?

Hicho mnachofanya ni kuringishia watu, mzaha si mzaha!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ