Wakuu habari za Leo, ninaimani kuwa mu wazima wa afya njema, tukiwa tunandelea na kampeni za uchaguzi kumekuwa na vituko toka kwa wagombea tofauti tofauti, kila mmoja na vituko vyake.
Kituko kilicho nisononesha ni cha huyu Mgombea Wa CHADEMA ndugu Tundu A.Lissu kutaka kuwaaminisha wafuasi wake kuwa unaarufu wake umepanda na kusifikia level za kina J.Magufuli hadi kufikia hatua ya kutaka mdahalo na JPM, maana yake haoni mwingine kwa wagombea urais zaidi 10,huku ni kuwapotosha wafuasi wake.
Kwanini nimesema hivyo, Lissu Mara kadhaa amekuwa akisisitiza kuwa anataka mdahalo na mgombea wa urais kupitia chama tawala cha CCM, swali la kujiuliza hapa ni kuwa kwanini Lissu alazimishe mdahalo na Magufuli tu, je katika uchaguzi huu washindani ni wawili tu?,je hawaoni akina B. Membe, Prof. Lipumba nk?
Ukweli ni kwamba Lissu ana wadharau sana Watanzania amefikia level za kujiona yuko juu ya Watanzania wote ,na elimu na uelewa alionao ni wajuu hakuna mtanzania wa kumliko.
Kitendo cha Mh. Lissu kuwadanganya na kuwaaminisha wafuasi wake kuwa kwa sasa amekomaa kisiasa na anao uwezo wa kufanya midahalo na kina Magufuli ni kitendo cha kilaghai kinacholenga kuwaaminisha wafuasi wake kuwa tofauti na Magufuli hakuna mwingine wa kuweza kujadiliana naye, kwanini asitake midahalo na kina Membe?
Hii inadhihirisha kuwa mtu huyu akipewa madaraka ni hatari sana na ni miongoni mwa watu wanaoamini kuwa hawezi kushirikiana na watu wanyonge, na ni kweli hili tumeliona maana kampeni zake muda mwingi zinazungumzia habari za ulaya na mabeberu tu, Ulaya kwenyewe katika akiwa mgonjwa na kaka miaka miwili, je angekulia ulaya na kusomea ulaya si angefikia hatua ya kututemea mate?
Shime Watanzania agopeni sana mtu anayeishi kwa kuigiza maisha huyu ni hatari sana, akipewa madaraka mtu huyu rafiki zake watakuwa ni watu wenye vipato vya juu hali ambayo itapelekea kuongezeka kwa pengo kati ya masikini na tajiri na kupelekea chuki na mafarakano miongoni mwa Watanzania.
Say NO for Tundu A. Lissu
View attachment 1576065