Namuangalia Membe ndio anamalizia kuingizwa ward ya watu wenye uangalizi maalumu (ICU)akiwa kwenye machela.
Lissu yeye ndio anachechemea ulingoni, kwakeli Anko Magu anashambulia pande zote kwa ustadi mkubwa kila kitu kimepangwa kikapangika ukiangalia ratiba zake tu utaligundua hilio.
Kwanza ndie mgombea atakaefikia watu wengi ukiangalia kuanzia usafiri wake mpaka crew yake nzima anayoongozana nayo ,
utagundua nyuma yupo manager kampeni aliyeisomea hii shughuli.
Ukirudi kwenye suala la sera utagundua ndio sera zinazo uzika na kutekelezeka kwa uraisi na ndizo zinazomgusa mwananchi wa daraja la mwisho, ana onyesha unyenyekevu na wala haombi kura kwa huruma ,bali kwa yale aliyokwisha kuyafanya na anayotaka kuyafanya kipindi kingine cha miaka mitano.
Kila nikimuangalia Membe pumzi zimeshakata mapema kila nikimtafuta hapatikani kwenye simu akipatikana kachanganyikiwa na kichwa kinamuuma kwenye jua kwa kupigwa na jua bila wasikilizaji ,aliyemuingiza chaka zitto kamkimbia anaona anatoa pesa yake mfukoni, wakati yupo CCM hakuzoea kutoa mfukoni mwake hili limekua tatizo kubwa kwake, anataka kubwaga manyanga lakini anaona aibu jinsi gani alijigamba na hii aibu na fedhea hajui ajifiche wapi.
Huyo Lissu mmmh yeye anapuyanga tu watu wanajaa kwenda kumshangaa kwa vile kawaambia ana risasi ana tembea nayo mwilini watu wanafikiri wataiona lakini kwa sera hana kwa sababu zote hazitekelezeki na ni ndoto za alinacha maziwa kutoa mabomba .
Yeye anamshambulia Magufuli binafsi badala ya kumwaga sera inaonyesha jinsi upepo wa Magufuli ulivyowaelemea
Magufuli ni habari nyingine ni heavy weight candidate amewaelemea wote na ataibuka na ushindi wa kishindo tayari kukamilisha miaka mitano mingine
NB;HATULIPI MATUSI TUNALIPA MAENDELEO kama mnabisha tukutane jamhuri siku ya kuapishwa JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI ni kale kale kajoni!
Safari kwenye jopo la kampeni!