Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Nimeamini kabisa kuwa ccm sasa imebakia midomoni tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa watu wanaokuja kwenye mikutano ya kampeni ulitaka watembee kwa miguu?, Mfano mie nakaa ubungo kuwe na mkutano kimara nitembee kwa miguu ili nigundue nini ?
Kama ukitaka kwenda kwenye mkutano unalipa nauli yako au usafiri wako unakwenda, siyo lazima ulipiwe na chama, hiyo ni rushwa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama JPM anataka aongeze margin yake ya ushindi namshauri yafatayo:

a) Aachane na Tundu Lissu. Kwa upande huu alianza vizuri maana Tundu Lissu alipokuwa anatafuta wadhamini alimtaja Rais Magufuli mara nyingi
sana lakini JPM alinyamaza. Hii ilimpa credit hadi pale alipokuwa Ikungi ndipo akashawishika kumsema Lissu kinamna kwamba aache kugombea
na atampa kazi ndogo ndogo. Alivyojibu Lissu haikuwa vizuri wa Rais. Mama Samia naye alifanya kosa hilo hilo. Ushauri: just ignore him. Endeleeni
kunadi sera zenu
b) JPM ajiepushe kutisha watu kwamba watakuwa na miaka 5 ya taabu endapo watachagua mpinzani kuwa mbunge. Upinzani upo hapa kisheria
na kila mpigakura ana haki ya kumpigia yeyote anayempenda. Sijuia JPM ana maana gani akisema watapata tabu. Nadhani anasema kuwanyima maendeleo.
Kwa nini awanyime maendeleo wakati wanalipa kodi? Kama ni hivyo hii pia inatengeneza picha hasi kwa Rais kwamba anabagua raia wake kutokana na itikadi yao.
Picha kama hii haitakiwi kuhusishwa na Rais ambaye kila siku amekuwa akinukuliwa akisema "maendeleo haya vyama". Namshauri ajiepushe na kauli kama hizi maan kiukweli siamini kama zitamwongezea kura. Kinyume chake inaweza kuwa kitu cha kumpunguzia kura.

Nawasilisha.
 
Si mara moja wala mara mbili nimesikia hasa katika matukio ya uzinduzi viongozi waliopewa dhamana na JPM mwenyewe wakimuaminisha kuwa kazi ameshaimaliza hana haja ya kuzunguka 2020.

Sasa hivi wanapoyaona haya wana yapi tena ya kumuambia? Wana ujasiri wa kusema lolote tena? Au ndio wanamuambia tulia mzee haka ni kaupepo tu kanapita?
 
Aisee CCM na JPM wao wana hali mbaya sana. Si bara si Zanzibar.

Kwa hali niliyoiona leo Zanzibar kwenye mkutano wa Lissu ni dhahiri CCM lazima wanyooshe mikono mwaka huu!

Sasa ni wazi!! Uchaguzi wa kihistoria Tanzania ni mwaka huu!
 
Aisee CCM na JPM wao wana hali mbaya sana. Si bara si Zanzibar.

Kwa hali niliyoiona leo Zanzibar kwenye mkutano wa Lissu ni dhahiri CCM lazima wanyooshe mikono mwaka huu!

Sasa ni wazi!! Uchaguzi wa kihistoria Tanzania ni mwaka huu!
CCM inahali mbaya ipiiiii, maaaana sioni wapinzani wowotee, wapinzania wa CCM asilimia kubwa wako wananadi KIKI badala ya kunadi sera zao.
 
Yani wamelegea utafikiria samaki aliechina,ccm kinabebwa na nec,policeccm,tiss bila hivyo kinasahaulika milele...hii ndio hali ya leo mwanza wamejaza watoto tu mabasi ya zuberi, zakaria, macoaster ndio yalikua yanasomba tu watoto
 
Tukiachilia mbali kile KIWANDA CHA MATUSI. NA KIKI ZA MIUJIZA, nani mpinzani wa Jemadariii ,MAGUFULI??
hata hizi kampeni anazofanya Magufuli nikutimiza wajibu tuuuu. Hata akiamua kujitulia ikulu ushindi wa asilimia mia, ukopale pale.
100% una maana hata wagombea wenzake watampigia kura?shule mlisomea nini kwa kweli?
 
Ccm inahali mbaya ipiiiii, maaaana sioni wapinzani wowotee, wapinzania wa ccm asilimia kubwa wako wananadi KIKI badala ya kunadiiii sela zao.
Wamelipwa kusema uongo ili matokeo yakitoka washindwa wakimbie kushitaki kwa mabwana zao.Kipigo chenu hakiepukiki mpaka mpoteane.
 
Cha msingi ni kuachia tu wengine watawale tuone tofauti
Neno chama cha mapinduzi limetokana na mapinduzi yaliyopelekea umwagaji damu kule Zanzibar na mkakati wake ulikuwa kuifuta kabisa Zanzibar kama nchi ili iwe kimkoa tu ndani ya Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…