Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu


Au inawezekana afya haimruhusu kuendelea na mikikimikiki ya kampeni. Tungoje CCM watujuze zaidi

Lakini kikubwa zaidi, wana CCM wengi hawana shauku ya kumpigania Magufuli kwenye kampeni za mwaka huu isipokuwa kwa unafiki na hofu tu ya kushughulikiwa.
 
Pamoja na kutegemea kuiba kura , ajue kabisa watu wameshamuwekea plan B na dunia nzima inafuatilia kila kinachoendelea Tanzania Mpaka uchaguzi ukamilike .
 

Mikutano mingi haimaanishi kuwa ni ubora. Watu wanapima ubora na sio wingi. Hayo kwenye soka tunasema chenga twawala.
 

TUNA JAMBO LETU ZANZIBAR KAA KWA KUTULIA
CCM NI CHAMA IMARA
YAJAYO NI NEEMA ZANZIBAR YA DR HUSSEIN MWINYI
 
Ndugu,hao wote uliowataja hawana mvuto kabisa,kwakuwa hawana jipya.
Wapiga kuja wanajipima wao wenyewe kwa miaka hii mitano hali ikoje?Hao ulio wataja zaidi Treni/ndege/madaraja/zahanati hawana jipya!
Mtaani hali mbaya,wanyonge mlo moja taabu.
Tangu tupate uhuru hakuna rais aliyesifiwa kwa kuleta hali nzuri mtaani.

Huwa tunasubiri rais aondoke ikulu ndio tumpe sifa za kinafiki, tatizo ni zaidi ya kumnyooshea kidole rais anayekuwepo madarakani.
 
Yaan hii nayo hoja? Rudi kajifue
 
The


Idiot !!!Morogoro hukuona picha?
 
Kusema kampeni za CCM ni ngumu ni vichekesho. Rais Magufuli hata asipopiga kampeni kuanzia leo ushindi ni 90%

Rafiki zetu wa CHADEMA mtaula wa chuya huu mwaka hampati hata mbunge.

Hivi kama kwa miaka yote mitano alivipiga pin vyama vingine akabaki yeye na ccm yake kupiga kampeni na kutoa rushwa kila alipopita, mpaka sasa hajiamini, na anendelea na hizo kampeni, kwa nini kama tayari ana ushindi si angetulia tu ili oa wengine kwa hii miezi michache ya kampeni wagawane hizo 10% iliyobaki?

Kati ya mwaka atakaopata ugumu wa kampeni ni mwaka huu maana mbinu za ccm zimefeli na imebakia moja tu ya kutangaza kwa nguvu/mabavu aliyeshindwa kuwa kashinda.
 
Mikutano mingi haimaanishi kuwa ni ubora. Watu wanapima ubora na sio wingi. Hayo kwenye soka tunasema chenga twawala.
Ukiwa na viongozi wanne wanaofanya kampeni katika maeneo manne tofauti sio sawa na mmoja anaye kampeni sehemu moja tu.

Suala la ubora wa utekelezaji wa sera ndio linaloibeba CCM.
 
Morogoro hukuona picha?
Ukweli ni kwamba, mkitukana huwa ni dalili kuwa kilichoandikwa kimewashika, so najua hapa hoja imekuingia. Morogoro niliona tena UTV achana na editing ya mitandaoni. Wale watu kwa mji mkubwa wa Morogoro walipaawa wawe kwa level ya Mgombea udiwani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…