Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Kumbe bado Ni rais?! Nilijua ameshakabidhi madaraka kwa kujibu wa sheria ya uchaguzi na Katiba..

Huyo ni mgombea wa urais na sio rais wa nchi...
bado ni rais; katiba haimuwondolei urais mpaka siku rais mwingine akiapishwa. Rais mawaziri, wakuu wa mikoa na spika bado wana nafasi hizo hadizinapojazwa na mwingine; nchi haiwezi kuongozwa na ombwe.

 
Yaani pale jukwaani nikimuona tu Polepole nazima runinga na siku yangu inakuwa imeharibika. Huyo jamaa ana damu ya kunguni. Hafai kabisa kuambatana na mgombea.
 
Sasa hiyo 90% unaipima na kuipataje ikiwa mgombea wa CCM hana mvuto, mpaka malori yatumike, shule zifungwe na wanafunzi wahudhurie?
Ninakumbuka vizuri, gari la Mrema lilisukumwa na washabiki, siku ya uchaguzi walikuwa majumbani kwao wanalalana au kwenye biashara zao.

Lowasa alijaza nyomi siyo ya karne hii, mwishoni mkasema CCM imeiba kura.

Keshokutwa mmeandaa vitisho eti msiposhinda, damu itamwagika.
 
Kama ni msikivu muite kwenye mdahalo kama atakuja!
 
Mkuu ubora upo na ukitaka ushahidi wa ubora ni tarehe 28 Oktoba mwaka huu.

Chama tawala kina wanachama milioni nane hao ni wapiga kura bado hatujaongelea wale wapya wanaoshawishiwa na kampeni.

Kila ukiona nguo ya kijani kwenye kampeni tambua hiyo ni kura tayari.
 
Ulichoandika hakiwakwepeshi na gharika mtakayokutana nayo Oktoba.
 

Hawa ni wepesi tu sio wa kumuumiza mtu kichwa.
 
Kuna tafsiri nyingi hapa
1. Keshajihakikishia ushindi kwa njia zisizojulikana
2. Amekata tamaa
3. Uchovu na afya
4. Mbinu ya kumpumbaza adui
5.UKATA
 
Ningekuwa slowslow kwa utopolo huu leo buku 7 usingepata
 
Kama ni msikivu muite kwenye mdahalo kama atakuja!
Huo muda wa mdahalo unatumiwa kwa kampeni nyingine zenye tija zaidi.

Mdahalo wanafanya wagombea ambao hawajawahi kuingia ikulu.

Ule wa 1995 ulifanyika wakati wagombea wote hawajulikani kwa ukaribu kwa wananchi.

Leo Magufuli anajulikana anasimamia nini na ana maono gani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…