Spika Tulia: Tusichanganye Maadili ya Mtanzania na Imani za kidini. Lipi kosa la walimu waliosimamishwa kazi Kwa kucheza muziki? Warudisheni kazini

Waziri Mkenda katoa majibu ya kihuni. Cheo cha Mwalimu Mkuu ni cheo cha uteuzi alafu anatamka kwamba wakate rufaa (kudai haki ipi?). Viongozi wapunguze mihemko ya kufanya maamuzi kwa kufuata kelele za mitandaoni. Mkenda ni prof ni muhimu kuotendea haki elimu yake kwa kulosadia taifa kwenye mambo makubwa kuliko ku deal na issues ndogo ndogo ambazo kimsingi ni very rare kutokea kwenye mazingira ya shule na pengine siyo msingi wa mmomonyoko wa maadili.
 
Kosa la kucheza mziki linaitaji uchunguzi gani? Tuache kushabikia vitu vya hovyo. Kazi ya mbunge ni kuishauri na kuisimamia serikali, Tulia kakosea nini kama mbunge na spika au wewe ndiye unaetafuta sifa kwa waziri.
Bunge halifanyi kazi kwa kauli za mbunge mmoja mmoja na serikali inapaswa ifanye kazi yake kwa kuangalia maslahi ya kila upande sasa katika hilo uenda kuna wazazi wamelalamika hivyo katika hali hiyo ni wajibu wa serikali kufanya uchunguzi kabla hatua stahiki kuchukuliwa,serikali haifanyi kazi kama mganga wa kienyeji iseme itapiga ramli.
 
Wewe unaona walimu ndio punching bag na kada ya kuonewa tu. Akina Zuchu na Harmonize si huwa wanaitwa kwenye kampeni za CCM kukata viuno, na kampeni hizohizo watoto wa shule huwa wanakuwepo.

Sasa yanini walimu ndio wafukuzwe kazi peke yao. Serikali inatumia kigezo gani kusema wimbo wa Zuchu hauna maadili wakati serikali hiyohiyo kupitia BASATA iliuruhusu na huwa haifanyi rating ya age.
Siyo kila nyimbo inapigwa kila mahali, watoto wanapaswa kufundishwa maadili mema, Maudhui ya ile nyimbo yanafaa watu walioko kwenye ma-bar na magenge mengine ya wahuni
 
Wewe unaweza kwenda kufanya ngono kanisani? Na Paroko akikukamata watu wamuulize ni kwanini anakukamata wakati ulikuwa unaifanya ngono vizuri sana?

Kila sehemu ina taratibu zake, kama hao watoto wameharibikia huko makwao, kuna watoto wengine ambao wako salama, wasiharibiwe. Shuleni ni mahali pa kusoma, kuna maadili yake!
 
Siyo kila nyimbo inapigwa kila mahali, watoto wanapaswa kufundishwa maadili mema, Maudhui ya ile nyimbo yanafaa watu walioko kwenye ma-bar na magenge mengine ya wahuni

Basata ndio wasimamizi wa maudhui na waliibariki nyimbo iwe hewani.

Wangekuwa wanaruka nyimbo iitwayo '"'Yesu ni bwana"" ingekuwa ni sawa?

#YNWA
 
Role ya mwalimu ni kulea pia, so jamii inategemea vitu vikubwa zaidi ya kuwachezesha watoto nyimbo za kipumbavu
 
ubavu wanao sasa?
kwa sasa waupande ule hawaguswi!
halafu haka kamwanamke kaliko imba ni kazuri na hapo ndo hakana hela
 
Basata ndio wasimamizi wa maudhui na waliibariki nyimbo iwe hewani.

Wangekuwa wanaruka nyimbo iitwayo '"'Yesu ni bwana"" ingekuwa ni sawa?

#YNWA
Shida siyo nyimbo bali inapigwa wapi? Huwezi kusikia gospel inapigwa msikitini au kaswida inapigwa kanisani. Hali kadhalika, nyimbo zenye maudhui ya ngono hazitakiwi kupigwa kwa watoto
 
Shida siyo nyimbo bali inapigwa wapi? Huwezi kusikia gospel inapigwa msikitini au kaswida inapigwa kanisani. Hali kadhalika, nyimbo zenye maudhui ya ngono hazitakiwi kupigwa kwa watoto
Maudhui yapi ya ngono huku basata wameibariki?

#YNWA
 
Mimi ni mtumishi haya unayosema nayajua vizuri kama ungesikiliza mahijiano yote ya spika na Waziri inaonekana kwamba wamepewa adhabu na sio kusimamishwa tu!
Na kingina amefanya hayo kwa sheria ipi

Kwakuwa kwa mujibu wa Standing orders for public services (KANUNI ZA KUDUMU ZA UTUMUSHI WA UMMa 2009) Zikisomwa pamoja na Sheria ya Ajira na mahusiano kazini 2004..haziruhusu mtumishi kupewa adhabu bila kuambiwa kosa lake mkuu...

Sasa ntaanza na STANDING ORDER kanuni ya F.26 mpaka 30 zinaelekeza kuhus Displinary procedure za kufuata sio kujichukulia mamlaka mkononi kwa kuwa unayo mamlaka hayo..



Endelea na hiyo 30.ili upate picha vizuri


Kwa mujibu wa kosa lake alitakiwa aandike barua ya maelezo tu baada ya kupokea barua hiyo ndo ilipaswa ifuate batua ya onyo na si vinginevyo
 
Waache tu watoto wasikilize hii miziki ya kuhamasisha ushg na kubanduana
Maana inaelekea mfumo ndiyo unataka hivyo
Mitoto yenyewe ishajikatia kamba
Poleni wazazi wenye watoto kwenye kizazi hiki,
Na mpaka kufika 2030 mitoto itakuwa imeachakaaaaa
Haya sasa huko mashuleni ruksa watoto kukata mauno

Ova
 
Dr Tulia.. Kwenye Hili naku unga mkono!
Tuacheni masihara hako kanyimbo ka zunchu honey kila mtoto huku mitaani wanaimba.
Na waimbaji wote hao
Wanajuaa kubanduanaaa

Ova
 
Mfano hauendani na Mada husika mkuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…