Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Mwendo kasi ni kwa ajili ya inner city movements hivyo kimkakati ni vizuri wawepo katikati wao na ofisi zao.

By the way, gazeti la Mtanzania la juzi juzi naibu waziri wa tamisemi aliongea kuwa kuna mwekezaji mwingine ataleta mabasi yake (Emiratea toka dubai), je nae ataweka mabasi yake hapo ubungo??
 
Nafikiri magari ya kwenda Kaskazini kituo kipelekwe kule Tegeta dawasco na mikoa ya kanda ya ziwa na magharibi kipelekwe Kibaha. Then magari ya kusini yabakie Temeke


Ushauri mzuri pia, lakini kama nguvu ya kujenga hizo stand Temeke, Kibaha na Tegeta zikiunganishwa na kuweka barabara za uhakika kutokea hapo Mbezi itakuwa imetatua kero nyingi kwa wakati mmoja
 
Kutumia elimu yao positively si rahisi mkuu. Wako kimaslahi binafsi zaidi, jambo ambalo linatuumiza sisi walipa kodi.
 
Ni ajabu sana ata baada ya miaka 50 ya uhuru bado tunawaza stand za mabasi ..
Aliyeturoga sijui ni nani..

Haya ni matumizi mabaya ya ofisi..

Hasara ishatokea pale jangwani kodi ya Mwananchi imetumika vibaya..nani awajibike..??
 
Unaweza kujenga kitu sehemu sahihi lakin natural calamities huwez kuzikwepa kama ikitokea zikaja tofaut hata huko ma mbele wanahangaika na haya majanga
Jangwani panajulikana tokea Taifa la Tanzania linanzishwa, ni sehemu korofi kwa kujaa maji.
 
Kosa ndo limeshafanyika,pale Jagwani wageuze tu kuwa mradi wa viboko maana tukiweka samaki watabebwa na mafuriko.hahah
 
Mpaka sasa, Kitua cha mabasi ya mikoani pale Ubungo, kwa abiria wengine kama wataondoka Mbagala, Kigamboni, Kongowe nk ni mateso hasa kwa wale wa kipato cha chini.
Abiria wa tabaka hili hupata shida sana ikizingatiwa kwamba hushindwa kumudu gharama za kukodi vyumba vya kulala karibu na stendi ya Ubungo.

Leo Halmashauri ya Jiji inafikiria kuzidisha umbali tena hadi Mbezi, inawafikiriaje abiria hawa wa Kipato cha chini?

Kwa mtazamo wangu, badala ya Halmashauri ya Jiji kuihamisha Ubungo Bus Stand kupisha Dart, DART ndio wahamishiwe Mbezi baada ya kufanya ujenzi mdogo wa dharula wa ofisi na gereji na kuiacha Ubungo Stand ikiendelea kuhudumia abiria wa mikoani.

Kama ni makosa yalikwishafanyika ya kuliingizia hasara Taifa. Na ikumbukwe kuwa moto hauzimwi kwa moto bali maji. Hivyo hatua za haraka zinazokusudiwa katika utatuzi wa suala la DART halitakuwa na afya kwa watumiaji wengine.

Nashauri DART wahamie Mbezi na Ubungo Stand ibaki kwa ajili ya mabasi ya mikoani, ila ifanyiwe ukarabati mkubwa wa kuiboresha.
NAWASILISHA.
 
kwahiyo zile pesa zilzio tumika kujengea ule mradi pale. jangwani " tuhesabu kuwa ni hasara ...""aiseee Hawa viongozi wangekuwa ni raia wa China wangeshanyongwa

period "" wanatumia pesa za wananchi hovyo sijui huwa wanatumia makalio kufikiri
 
Mkuu wwe huoni kuna mianya inatengenezwa hapo watu waishi
Jiulize ujenzi wa huu mradi ulianza lini
Hawakuwa na uchambuz yakinifu juu ya eneo la jangwani
Nani aliizinisha ujengaji wa yard bila kufata ushauri

Hizi ni janja janja za upotevu wa pesa
hatari sana "" haya majizi ya taifa ..yaani mradi umedumu miaka miwili na nusu tu "" Tayari umeshalipatia taifa hasara...hiiiiiii
 
Nani alitamka haya maneno mkuu?
 
tuache siasa tuijenge nchi ...huku yeye na pole pole wanapita mikoani nakufanya mikutano ya kichama tena sometimes katika msafara wa kiserikali....

huyu mzee iko namna
 
daaahh ukiona hadi wew unalalamika means kweli hii serikali nimtihani "" yaani mpka mtoto umeamua kumkosoa mzazi "" hii ndio nchi Yetu bwana ..mazingaombwe ndio kwao
 
Acha tu waendelee kuchezea pesa, ila mm nawalaum wale wa mwanzo. Serikali iliwafukuza raia maeneo karibu na pale kuwa ni hatarishi. Iweje wao wajenge pale,?????
Sipati picha garama zake mana kuhama tu sio suluhisho, pale Jangwani maji yanapita juu. Huo ni mziki mwingine .
 
Watanzania hatunaga mipango endelevu siku zote.......

Ova
 
Ingefaa injinia wa jiji wakati wa upanuzi wa MTO msimbazi abuni mchoro kama wa Suez canal..

ili huo mfereji ubaki kuwa njia ya usafiri kwa boti na..

moja kwa moja uchafuzi wake utakoma kwa wananchi kuutunza na utalipendezesha zaidi jiji [emoji89]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…