Pre GE2025 Sugu hata akishinda Ubunge, asitangazwe, haiwezekani tupoteze heshima ya nchi kwa kumpoteza Rais wa IPU?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hivi ile issue ya kugawanya Jimbo iliishia vipi?
Msaada wa pekee kwa Tulia ni huu tu....vinginevyo nikujidanganya,msako ni mkali mno toka atangazwe mbunge,Hawezi kumshinda Sugu kama atagombea naye tena,hata kama Samia na Kinana watahamishia ofisi kule.
 
MOJA YA WATU WAJINGA NA WAPUMBAVU KUWAHI KUTOKEA NCHI HII BASI NI WEWE JAMAA, TAKATAKA KABISA WEWE
 
Kama vipi jimbo livunjwe pande mbili kila mtu agombee upande tofauti
 
Aisee wewe ni taira tena mbumbumbu pro max. Kwa kweli nimejitahidi sana kutumia lugha ya ustaarabu kwenye kuandika hii caption. Tena bila ya aibu umeandika huu uzi kwa ustadi na kuzingatia kanuni zote za uandishi kuthibitisha kuwa to some extent you're educated. Wapuuzi kama wewe ndio mlioshinikiza Job Ndugai kupokwa wadhifa kwa kuikosoa serikali ilhali hili ni jukumu la spika wa bunge kikatiba kabisaaa. Tanzania ni nchi yenye demokrasia, it is a democratic Republic of tz na sio familia kuongozwa kama unavyofikiria. Kwanza mtu kama wewe unatakiwa kufungwa kwa kuushawishi uma kuivunja sheria ya nchi kibepari. Bila shaka ushauri wa watu kama nyinyi mwishowe utaliingiza taifa kwenye majanga kama majirani zetu wa +254.
 
Kwa tume hii? Spika akose jimbo? Itakuwa ni maajabu
 
Hii pointi niliisahau chief
Ubunge wa nusu mkate sio ubunge wa kujitosheleza, kwa mfano,huko Kenya wabunge viti maalumu wanawake waliunga mkono pad za kike ziongezwe kodi,japo wabunge wanaume walipinga.Kwa ufupi ni wabunge wanaojipendekeza kwa chama au taasisi iliowateuwa.hawako kwenye ballot box.
 
Kwa tume hii? Spika kose jimbo? Itakuwa ni maajabu
Hilo halitawezekana kamwe, na ili kulinda heshima ya spika ni lazima majimbo yawe mawili. Vinginevyo spika atatangazwa katika mazingira ambayo yatamchafulia taswira yake, na hilo CCM wanalitambua na hawatoliruhusu. Mambo yanabadilika kwa kasi sana na lazima CCM wabadili mbinu kwenye majimbo yenye ushindani kama hili
 
Uraisi wake uko IPU unalinufaishaje hili taifa hasa hiyo Mbeya yenyewe zaidi ya kuuza nchi yetu kwa Mashoga zake na Mama ake?
 

Kwani huo uspika wa IPU una faida gani ya moja kwa moja kwa wananchi wa Mbeya?

Kama Dr Tulia ³anaupenda ubunge, ashauriwe akagombee jimbo mojawapo la mkoa wa Dodoma.
Mwaka 2020 Tulia hakuchaguliwa na yeyote. Hivyo ni muhimu kwake safari hii kutafuta mahali pa kwenda kuchaguliwa.
 
Heshima na faida ya IPU ni yake binafsi na familia yake .
Watanzania hatunufaiki chochote na huo Urais wake wa mabunge.
 
Sasa kwa nini kutumike njia za panya, hapa ni kucheza kidikiteta tu mkuu
Tunatakiwa tujenge Tanzania ambayo watu wote ni waadilifu na tutaheshimiana.
Wote tuamini viongozi, tume na mahakama kwa kuona haki ikitendeka kwa mustakabali mwema wa taifa (hasa wananchi na vizazi vijavyo).
Kiongozi anapita kwa muda huu mfupi, taifa, wananchi na vizazi vijavyo vitaendelea kuwepo.
 
Hivi Tz inanufaika nini na huo u Rais wa Tulia huko IPU. Au ni ujiko tu kama ilivyokawaida yetu kujinasibu kuwa tunasifiwa sana.
 
Watanzania mnaipenda sana democracy lakini hampendi matokeo yake. Hivi Nini maana ya uchaguzi? Kampeni zinafanyika ili iweje??

Hakika kwa style hii tutachelewa sana kufika. Watu wanamng'oa Rais alieko madarakani kwa njia ya kura sembuse Tullia anaezulula bila manufaa yoyote kwa nchi???

Haya sasa nikuulize mtoa mada tangu tulia amechaguliwa kuwa spika wa kuzunguka ulimwengu mzima wewe kama mwananchi umefaidika na Nini??? Sisi kama nchi je tumefaidika na Nini mpaka sasa??
MKUU UNAABISHA WOSOMI.
 
Huo Urais wa Mabunge hua wanafanya kazi gani? Yani nikuulize hao Wabunge sijui wa dunia nzima wanafaida gani kwa Tanzania? Hadi muufanye kitu cha kuharibu Demokrasia nchini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…