Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Kuna vipindi kibao ambavyo kila jumapili bbc inaonesha matokeo kanisani, edher rejea mazishi ya Prince Phillip mchana kutwa kanisani.

Ktk tukio la dini ambalo waziri mkuu anahudhuria sioni kosa kituo cha tv ku cover hilo tukio.
Kwanza ulinukuu katiba ukasema tbc waliendesha shughuli ya Dini.
Nikakuambia uendesha ni tafauti na kureport.

Jitahidiuwe open minded achana na chuki za kilokole Mama
 
Tunazungumzia Asili ya hayo maneno kuwa yametoka kwenye lugha za mataifa mengine kabisa na mengine yamebaki na maaana ileile.
 
ila nyimbo zisizokuwa na maadil ni ruksa.kinachuupq faraja roho ni tenzi za rohoni.Dini ziwepo kutupa faraja
 
Maadili yapi?
Kama hazina maadili iambieni serikali izifungie
ila nyimbo zisizokuwa na maadil ni ruksa.kinachuupq faraja roho ni tenzi za rohoni.Dini ziwepo kutupa faraja
 
Usiwe kama ngumbaru kuhamishia mjadala kwenye imani fulani ili ionekane uzi ni kwa ajili ya kupinga dini fulani. Suala ni vyombo vya habari vya taifa visiwe jukwaa la mahubiri kwa dini YOYOTE.
Tatizo unaweza kuwa ni kijana mdogo usiyeielewa hii nchi vizuri. Ungeielewa ungejua kuwa hayo mawazo yako ni njozi zisizoweza kuja kutimizwa pengine wewe ukiwa hai.
 
Tuvumiliane: Kwa kutumia mwongozo gani?
Mwongozo uliopo sasa. Mawaidha ya kiislam kama yanakukwaza badilisha chanel mkuu. Hautapungikiwa chochote.

Mwongozo wa kuvumiliana na kuishi kama watanzania wenye dini, mila, malezi na mitazamo tofauti.
 
Sijwahi kusikia waislamu au Wakristo wakilalamika nyimbo za bongo fleva kupigwa TBC. Waislamu na Wakristo wote wanzipenda sana na huzitumia hata katika harusi zao, maulid, kipaimara, arobaini n.k
Wanajielewa sana ndio maana hawababaiki.
 
Taasisi za serikali kutumika kama majukwaa ya dini ni matumizi mabaya sana ya pesa za walipakodi. Wote tupinge huu utaratibu.
Kuna madaktari wanafanya kazi kwenye hospitali za mashirika ya dini je nao waondolewe?
 
Bado sijaona ubaya wa TV ya serikali kurusha vipindi vya dini tena kwa dakika chache za siku za ibada zao, kuna maeneo hizo TV za kisekta hazifiki, lakini vilevile kuna wakati hizo TV za kisekta zinarusha vipindi vya serikali kama hotuba za viongozi je nalo ni baya?
 
Nimekuwa nikipinga kuchanganya shughuli za kidini kwenye shughuli, mifumo na taasisi za serikali bila kujali mfalme ni nani.
Mkuu, kule Bungeni huwa wanafanya sala kila waanzapo session, na hata kwenye matukio makubwa ya kitaifa kama sherehe za maadhimisho mbalimbali huwa wanaalikwa viongozi wa dini zote kufanya sala, je ina maana kumtaja Mungu katika sehemu kama hizo ni matumizi mabaya ya nafasi/muda wa umma?
 
Thanks
 
Sala ya bungeni huwa ni ya dini gani?
 
Nimeyaona haya leo
Samahani... we mwenzetu ni mgeni nchi hii? Au unataka kutuambia umeanza kutazama tiibiisii wakati huu wa SSH? wakati wa Mwendazake, JK, BM havikuwepo hivyo vipindi au enzi za AHM na JKN hukuwahi kusikiliza RTD vitu kama "inueni mioyo... Quran tukufu?"
JE WADHANI KWANINI RAIS SSH KAJA NA SALAAM MPYA YA KITAIFA? JE WADHANI KWANINI HIYO SALAAM YAKE BAADHI WANAIPINGA? Je kwanini wapo viongozi bado wanatoa salaam za kidini kwenye mikutano au vikao vya serikali ilhali serikali haina dini?
 
maelezo meengi kisa inakuuma kwa maudhui ya kiislam kutumia siku ya ijumaa.mbona hupingi wakristo kutumia siku ya jumaa pili? acha chuki za hovyo hizo.
vile vile mbona huja hoji kwani ccm wanatumia TBC katika mambo yao? chukulia mfano kipindi cha kampeni kila sehemu mwenda zake alipokuwa ccm walirusha live, na hata sehemu akihutubia njiani nao walikuwa wanarusha live hizo ni kampeni za chama kimoja mbona hukuhoji hilo?
Hata jana tu katibu wa ccm na sekretariet yake walivyopokelewa hapo Lumumba TBC walirusha live.mbona husemi kwamba ccm inabidi watumie tv yao ya channel ten.Acha chuki ndugu kazi iendelee
 
mwendazake mkatoliki mwenzao kila akienda kanisani TBC ilirusha live mbona hawakusema?
 
Naona hujaelewa wazo langu. Basi twende kwa mtindo wa point counter point namna hii:

1. Nilichokisema mimi ni kwamba dini/imani ni sehemu ya utamaduni wa watu/walipakodi.

Jibu: neno dini lina maana nyingi: Kuna dini ambayo ni sehemu ya utamadni wa Kitaifa, dini ambayo ni sehemu ya utamadni wa kikabila, dini ambayo ni sehemu ya utamadni wa Wakristo, dini ambayo ni sehemu ya utamadni wa Waislamu, dini ambayo ni sehemu ya utamadni waWahindu, dini ambayo ni sehemu ya utamadni wa Wabuda, nk. Unaongelea dini gani na utamaduni gani?

2. Kama kipindi kinachorushwa kinahusu dini/imani (sehemu ya utamaduni wa watu), kama kinavyoweza (kurushwa kikiwa na maudhui) kuhusu uchumi, siasa na jamii, kwa kuzingatia taaluma ya uhandishi wa habari kwa namna ambayo haivunji maadili au sheria za nchi,

Jibu: Dokezo kuu la hoja inayojadiliwa hapa linaanzia kwenye ibara ya 4(1) na 19(2) za Katiba ya Tanzania (1977). Ibara hizi haziongelei uchumi, siasa wala jamii. Zinaongelea kutenganisha shughuliza serikali na shuguli za dini. Hiyo ndiyo fokasi ya hoja.

3. Na kwa vile baadhi ya walipakodi ni waumini pia katika hiyo dini/imani,

JIbu: TBC inatumia kodi ya walipa kodi wote, wakiwemo watu wasio na dini. Haitumii kodi ya baadhi ya walipa kodi.

4(i) Basi, hakiwezi kukiuka utaratibu wa kawaida wa kurusha vipindi vya TV au radio na

Jibu: Hitimisho hilo halitokani na madokezo sahihi, kama nilivyoonyesha hapo juu, na kwa hiyo halina uhalali.

4(ii) hivyo (kwa maoni yangu) hakuna utata wowote katika hili.

Jibu: Hitimisho hilo halitokani na madokezo sahihi, kama nilivyoonyesha hapo juu, na kwa hiyo halina uhalali. Utata upo kama nilivyoonyesha hapo juu.

5. Labada wewe mwenyewe uonyeshe urushaji wa hivyo vipindi vinavyosemwa ulikuwa na utata gani au ulikiuka utaratibu gani wa urushaji wa vipindi.

Jibu: Bandiko langu limeonyesha vema utata. Linao muundo ufuatao: matarajio, uhalisia, ufa kati ya matarajio na uhalisia, mapendekezo ya kuziba ufa, na majibu ya pingamizi tarajiwa. Soma kwa kutulia

6. Kama urushaji wa hivyo vipindi una tatizo, basi tujadili hilo tatizo kuliko kujadili jambo la jumla hivyo.

Jibu: Tatizo ni urushaji wa vipindi vya kidini kupitia TBC kuvunja kanuni ya 4(1) na 19(2) ya Katiba ya Tanzania (1977), na bandiko langu limeonyesha vizuri tatizo hili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…