Taarifa Kwa Umma: Fact Finding Mission-Jimbo la Kigamboni

Taarifa Kwa Umma: Fact Finding Mission-Jimbo la Kigamboni

Jitambulishe tukujue we ni nani na uchunguzi wako utasaidia vipi wamanchi au mamalaka za juu.
Shida yako ni hiyo tu au kuna kingine?Nispojitambulisha na kama utafiti wangu ni kwa ajili ya kjifunza tu basi niache kujifunza?
 
Ninapenda kuwajulisha kuwa kuanzia Jumapili tarehe 9 mwezi wa nane,2020 hadi Jummane tarehe 11 Mwezi wa 8,2020 kutafanyika shughuli ya ukusanyaji wa taarifa na maoni ya wananchi wakazi wa wilaya ya Kigamboni Juu ya matamanio yao maoni, na matarajioi yao kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.

Baada ya kibano cha wajumbe kuna kiunzi kingine cha umangi-meza wa serikali ya CCM kubana kazi kama yako ya kitafiti / maoni. Sheria zingine mnazotunga CCM hamkujua zitakuja kuwa pia kikwazo kwenu.

Kibali unaocho au ufahamu kuwa chini ya utawala wenu wa CCM Mpya zoezi kama hili ni batili na haramu.

Tafiti, social science survey na maoni yanahitaji ruhusa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu NBS kwa mujibu wa sheria iliyopitishwa kwa wingi na wabunge wa CCM.
Sheria ya takwimu kuwabana watafiti? Mtakwimu mkuu wa Serikali atoa ufafanuzi

11 Sep 2018
Baadhi ya watafiti nchini wamepaza sauti na kudai mabadiliko ya sheria ya takwimu yanayotarajiwa kupitishwa na bunge yatawanyima fursa ya kufanya tafiti na kuzichapisha. Lakini mtakwimu mkuu wa Serikali ametolea ufafanuzi sheria hiyo na mengineyo. Wasikilize wote
Source : azam tv

Maoni kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Takwimu :: Matangazo ...
28 Sep 2018 · Msimamo wa Asasi za Kiraia kuhusu Mapendekezo ya ... waitaka serikali kutekeleza Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa ...
Maoni kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Takwimu :: Matangazo :: Vyombo vya habari :: Twaweza.org
 
Ndugu wakazi wa Wilaya ya Kigamboni;

Ninapenda kuwajulisha kuwa kuanzia Jumapili tarehe 9 mwezi wa nane,2020 hadi Jummane tarehe 11 Mwezi wa 8,2020 kutafanyika shughuli ya ukusanyaji wa taarifa na maoni ya wananchi wakazi wa wilaya ya Kigamboni Juu ya matamanio yao maoni, na matarajioi yao kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.

Zoezi hili litahusisha kata zote za wilaya ya Kigamboni na linalenga kuwafikia wakazi wapatao 4000 kwa ajili ya kukusanya maoni yao juu ya maeneo ambayo wangependa yapewe kipaumbele na uongozi utakaochaguliwa na matarajio yao kwa miaka mitano ijayo

Maoni yote na ushauri wa mambo ambayo ungependa yawe kipaumbele katika uchaguzi huu yatapokelewa kwa njia ya Email:
mbungekigamboni20@gmail.com. au kwa kuzungumza na wakusanya taarifa ambao watapita katika maeneo mbalimbali katika wilaya yetu kupata taarifa za wananchi.
Kumbuka zoezi hili ni muhimu katika katika maendele.

Zoezi halina uhusiano na chama chochote cha siasa wala taasisi yoyote bali ni jitihada za Wana Kigamboni katika kutaka kuweka malengo ya pamoja kwa miaka mitano na kujua vipaumbele katika kila kata

Zoezi hili ni muhimu kwani litasaidia kuwawezesha wanakigamboni kushiriki katika kupanga sera na mipango ya maendeleo kwa kata zao na mitaa yao.Ripoti kamili ya zoezi hili itatolewa Ijumaa Tarehe 21 August 2020

Maoni yatumwe kwenda kwa EMAIL.mbungekigamboni20@gmail.com
Kumbuka kutaja mtaa ulipo katika kutoa maoni yako ili kusaidia katika ufuatiliaji.

Asanteni Sana kwa ushiriki wenu.

Taarifa Imetolewa,

Gwakisa M.J
Mdau wa Maendeleo Wilaya ya Kigamboni
(1) Hebu malizia kwanza hiyo M na J kwenye jina lako na uweke mawasiliano yako.

(2) Kampeni zimesharuhusiwa kuanza?
 
Angalau wewe umeanza kuelewa...Wengine naona wana sentiments.Kama wewe ni kazi wa Kigamboni unaweza leta maoni yako pia

Mkuu naona unalazimisha kumalizia nyumba yako kwa pesa za Bashite. Unakuja na Id fake unajifanya kukusanya maoni ww ni nani? Kwani hakuna mikutano ya mitaa mpaka uweke email yako ukusanye maoni? Acheni utapeli wa kijinga.
 
Mbona watu wana hofu za namna hii,Mimi nafahamu ninachokifanya sijui kama wewe unaelewa ulichokisema

Unafahamu unachokifanya? Huo ndio utaratibu wa kukusanya maoni ya wananchi? Nyie ndio wale matapeli wa hiyo pesa tuma kwenye namba hii.
 
Mmedhamiria kukusanya maswali ili kummaliza aliopo kuwa hajui changamoto za kg.
Mipango ya kuleta maji ya 1.Dawasco tuondokane na maji chumvi.
2.Soko la samaki.mapato ya samaki yanaenda ilala peke ake ingawa sehemu kubw ya uvuvi Dsm inayovuliwa ni bahari ya kigamboni.
3.Ahadi ya rais wakati wa uzinduzi wa daraja.alisema ole njia imeanzia buyuni inaenda mpaka pugu.Basi barabara ya kibada buyuni ikamilike na kisha buyunivpajengwe soko kubwa la mnada wa samaki.
 
Pili pale tulipompora manji gezaulole pajengwe michezo complex yaani viwanja vya michezo yote kuanzia uogeleaji,riadha zote,netball,kikap,football.badala ya kuja na hoja ya kizamani za kugawa kwa wananchi.natumai panatosha pamoja na kuwa ofisi za serikali zimeshakaa lakini patatosha tu.
 
(1) Hebu malizia kwanza hiyo M na J kwenye jina lako na uweke mawasiliano yako.

(2) Kampeni zimesharuhusiwa kuanza?
Mkuu,natamani nifanye hivyo ila wakati muafaka ukifika nitaweka ila kwa sasa wana Kigamboni wanweza kutoa maoni yao ili tuandae mipango nakuhakikisha wagombea wote wanatambua matarajio yetu ili kama wakijipima wakiona hawatoshi wajue kwamba kazi ni nzito.
 
Ndugu wakazi wa Wilaya ya Kigamboni;

Ninapenda kuwajulisha kuwa kuanzia Jumapili tarehe 9 mwezi wa nane,2020 hadi Jummane tarehe 11 Mwezi wa 8,2020 kutafanyika shughuli ya ukusanyaji wa taarifa na maoni ya wananchi wakazi wa wilaya ya Kigamboni Juu ya matamanio yao maoni, na matarajioi yao kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.

Zoezi hili litahusisha kata zote za wilaya ya Kigamboni na linalenga kuwafikia wakazi wapatao 4000 kwa ajili ya kukusanya maoni yao juu ya maeneo ambayo wangependa yapewe kipaumbele na uongozi utakaochaguliwa na matarajio yao kwa miaka mitano ijayo

Maoni yote na ushauri wa mambo ambayo ungependa yawe kipaumbele katika uchaguzi huu yatapokelewa kwa njia ya Email:
mbungekigamboni20@gmail.com. au kwa kuzungumza na wakusanya taarifa ambao watapita katika maeneo mbalimbali katika wilaya yetu kupata taarifa za wananchi.
Kumbuka zoezi hili ni muhimu katika katika maendele.

Zoezi halina uhusiano na chama chochote cha siasa wala taasisi yoyote bali ni jitihada za Wana Kigamboni katika kutaka kuweka malengo ya pamoja kwa miaka mitano na kujua vipaumbele katika kila kata

Zoezi hili ni muhimu kwani litasaidia kuwawezesha wanakigamboni kushiriki katika kupanga sera na mipango ya maendeleo kwa kata zao na mitaa yao.Ripoti kamili ya zoezi hili itatolewa Ijumaa Tarehe 21 August 2020

Maoni yatumwe kwenda kwa EMAIL.mbungekigamboni20@gmail.com
Kumbuka kutaja mtaa ulipo katika kutoa maoni yako ili kusaidia katika ufuatiliaji.

Asanteni Sana kwa ushiriki wenu.

Taarifa Imetolewa,

Gwakisa M.J
Mdau wa Maendeleo Wilaya ya Kigamboni
Weka kibali cha ruhusa ambacho kimetolewa na tume ya uchaguzi, vinginevyo ni zoezi haramu.
 
Pili pale tulipompora manji gezaulole pajengwe michezo complex yaani viwanja vya michezo yote kuanzia uogeleaji,riadha zote,netball,kikap,football.badala ya kuja na hoja ya kizamani za kugawa kwa wananchi.natumai panatosha pamoja na kuwa ofisi za serikali zimeshakaa lakini patatosha tu.
Asante sana ndugu yangu wewe ni mwanakigamboni kweli.Tuendelee kutoa maoni ili tupate viongozi bora wanaojua kile tunachotaka kwa maendeleo ya kigamboni.Tunataka wananchi nao wawe na sauti sio wagombea kuja na ahadi hewa na rushwa na kupotea baada y uchaguzi kwenda kukusanya faida.Mabadiliko yataanzia Kigamboni.
 
Matatizo na mahitaji yote muhimu ya watanzania yanajulikana na yanafanana,acha kupoteza muda.
Ikifika wakati wa kampeni itakuwa kampeni ila kwa sasa ni fact finding tu.
 
Weka kibali cha ruhusa ambacho kimetolewa na tume ya uchaguzi, vinginevyo ni zoezi haramu.
Uharamu wa hili zoezi ni upi,Kibali cha tume kitalipa zoezi uhalali?Usiwe na uchungu moyoni na kushindwa kufikiri kama mzalendo.Kama vyama vvyote vingetumia mfumo huu wa maoni kwa hakika wananchi wengi wangshiriki na tungepata maoni ambayo yanaakisi mahitaji ya wananchi
 
Matatizo na mahitaji yote muhimu ya watanzania yanajulikana na yanafanana,acha kupoteza muda.
Mkuu,hakuna kitu kama hicho,ila kama umechagua kuamini sishangai kwa nini miaka 50+ baada ya uhuru bado tuna watu wenye fikra kama zako.Ni uthibitisho kwamba kuna tatizo katika mfumo wetu wa elimu na uongozi
 
Umeshindwa hata kudesign email yenye mvuto, yaani email ilivyokaa tu inaonyesha kitu unachofanya siyo formal na obviously haupo serious nacho
 
Back
Top Bottom