Taarifa kwamba wapo wakuu wa wilaya wameomba kuacha kazi kwa ajili ya majukumu mengine binafsi zina ukweli?

Taarifa kwamba wapo wakuu wa wilaya wameomba kuacha kazi kwa ajili ya majukumu mengine binafsi zina ukweli?

Ukuu wa Wilaya zamani walipewa makada wa 45-50 kama maandalizi ya kustaafu. Leo unampa kijana wa 30 mwenye elimu yake nzuri kazi ya kwenda kukaa ma Wilayani huko wakati ana uwezo wa kupata kazi UNDP na CV ameisha ijenga.
Zama zimebadilika....

Kwa utandawazi huu....kuna ulazima gani wa kutowatumia vijana KULITUMIKIA TAIFA LAO katika nafasi hizo?!!!

Sensa ya 2012 ilionesha wenye umri chini ya miaka 35 ni 60%.....

My take: Kikatiba hakuna kipengele kuwa UDC wateuliwe wazee.

Hata huko zamani mh.SALIM AHMED SALIM akiteuliwa UBALOZI WA NCHI akiwa chini ya miaka 25 nini UDC ?!! Khaa😲🤣

Baba wa Taifa hayati JKN alikuwa WAZIRI MKUU akiwa chini ya miaka 40.....
 
Hamna kitu kama hicho asee, mtaani palivyo tight labda kama mtu kapata offer ya kwenda mamtoni kuishi vizuri
DC wana njaa kali sana labda hawa wa town na wilaya zilizo amka kidogo wanapiga vimi chongo vya hapa na pale.. ila sio kazi ile wamabaki na malaka ya kukuweka tu ndani ndio wanacho jivuniaga ila watu kuliko wewe
 
Zipo taarifa nimesoma kwenye group moja la WhatsApp kwamba baadhi ya wakuu wa Wilaya wamepata mchongo mpya na wameomba waruhusiwe kwenda kuimarisha carrier zao japo majibu hayajatoka. Rafiki wa karibu wa DC mmoja Kanda ya ziwa anaeleza kwamba rafiki yake ameshaomba na ametuma baadhi ya wazee wazungumze na mamlaka za uteuzi aruhusiwe kuacha kazi na kwenda kujiendeleza au kujiunga na Shirika moja huko nje.

Taarifa zinaeleza kwamba Hali ya vijana wengi walioteuliwa kuwa DC hawapo happy na nafasi hizo baada yakufika vituo vya kazi. Eti wanalalamika kwamba maeneo yao ya kazi hakuna kazi kwa sababu uwezi kwenda na mawazo mapya, watu wanataka uwasikilize wazee ambao wengi ni madiwani na viongozi wa chama. Lakini pia muundo wa halmashauri nyingi unakosa watu wenye upeo na hivyo kujikuta unapata ukinzani kufikia lengo. Anakubaliana na kauli kwamba hizi nafasi si za vijana maana zinadumaza ubongo.

Lakini changamoto kubwa inayopelekea watu kuomba kwenda kusoma au kupiga mchongo mwingine Ni maslahi kidogo wanayodhani kwa hadhi ya DC anapata lakini pia kukosekana Uhuru wa siasa na hivyo kazi ya DC kubaki kunyamazisha yeyote mwenye mawazo yenye mrengo tofauti na chama Tawala.

Endapo taarifa hizi Zina ukweli Basi akina Mayala wanaweza kupata uteuzi kuziba nafasi zitakazokuwa wazi.
Tanzania hakuna siasa,ila kipo kifananacho na siasa.
 
Umeumia, ulipenda waje wakuu kukupokea?
Kama Taifa tuna safari ndefu sana.
Nilitembelea mradi mmoja wa Wazungu hapa nchini.
Nikwa pale wakanunua mashine yenye thamani ya Bilioni 1.
Siku mashine imefika aliyeipokea ni kijana wa Stoo.

Mwezi uliofuata , mkoani kwetu kulikuwa na mradi wa maji wenye thamani ya milioni 200. Akaja waziri kuuzindua.
 
Ukuu wa Wilaya zamani walipewa makada wa 45-50 kama maandalizi ya kustaafu. Leo unampa kijana wa 30 mwenye elimu yake nzuri kazi ya kwenda kukaa ma Wilayani huko wakati ana uwezo wa kupata kazi UNDP na CV ameisha ijenga.
Naongeza Msisitizo
 
DC wana njaa kali sana labda hawa wa town na wilaya zilizo amka kidogo wanapiga vimi chongo vya hapa na pale.. ila sio kazi ile wamabaki na malaka ya kukuweka tu ndani ndio wanacho jivuniaga ila watu kuliko wewe
😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅 kazi kweri kwerii
 
Zipo taarifa nimesoma kwenye group moja la WhatsApp kwamba baadhi ya wakuu wa Wilaya wamepata mchongo mpya na wameomba waruhusiwe kwenda kuimarisha carrier zao japo majibu hayajatoka. Rafiki wa karibu wa DC mmoja Kanda ya ziwa anaeleza kwamba rafiki yake ameshaomba na ametuma baadhi ya wazee wazungumze na mamlaka za uteuzi aruhusiwe kuacha kazi na kwenda kujiendeleza au kujiunga na Shirika moja huko nje.

Taarifa zinaeleza kwamba Hali ya vijana wengi walioteuliwa kuwa DC hawapo happy na nafasi hizo baada yakufika vituo vya kazi. Eti wanalalamika kwamba maeneo yao ya kazi hakuna kazi kwa sababu uwezi kwenda na mawazo mapya, watu wanataka uwasikilize wazee ambao wengi ni madiwani na viongozi wa chama. Lakini pia muundo wa halmashauri nyingi unakosa watu wenye upeo na hivyo kujikuta unapata ukinzani kufikia lengo. Anakubaliana na kauli kwamba hizi nafasi si za vijana maana zinadumaza ubongo.

Lakini changamoto kubwa inayopelekea watu kuomba kwenda kusoma au kupiga mchongo mwingine Ni maslahi kidogo wanayodhani kwa hadhi ya DC anapata lakini pia kukosekana Uhuru wa siasa na hivyo kazi ya DC kubaki kunyamazisha yeyote mwenye mawazo yenye mrengo tofauti na chama Tawala.

Endapo taarifa hizi Zina ukweli Basi akina Mayala wanaweza kupata uteuzi kuziba nafasi zitakazokuwa wazi.
Hapo kwenye Mayala, unamuongelea huyuhuyu Pascal Mayalla wetu wa JamiiForums?
 
Ishu kubwa hapo ni maslai vingine ni visingizio tu.
Ukimuona mtu kaacha Kazi ishu huwa ni maslai
 
Zipo taarifa nimesoma kwenye group moja la WhatsApp kwamba baadhi ya wakuu wa Wilaya wamepata mchongo mpya na wameomba waruhusiwe kwenda kuimarisha carrier zao japo majibu hayajatoka. Rafiki wa karibu wa DC mmoja Kanda ya ziwa anaeleza kwamba rafiki yake ameshaomba na ametuma baadhi ya wazee wazungumze na mamlaka za uteuzi aruhusiwe kuacha kazi na kwenda kujiendeleza au kujiunga na Shirika moja huko nje.

Taarifa zinaeleza kwamba Hali ya vijana wengi walioteuliwa kuwa DC hawapo happy na nafasi hizo baada yakufika vituo vya kazi. Eti wanalalamika kwamba maeneo yao ya kazi hakuna kazi kwa sababu uwezi kwenda na mawazo mapya, watu wanataka uwasikilize wazee ambao wengi ni madiwani na viongozi wa chama. Lakini pia muundo wa halmashauri nyingi unakosa watu wenye upeo na hivyo kujikuta unapata ukinzani kufikia lengo. Anakubaliana na kauli kwamba hizi nafasi si za vijana maana zinadumaza ubongo.

Lakini changamoto kubwa inayopelekea watu kuomba kwenda kusoma au kupiga mchongo mwingine Ni maslahi kidogo wanayodhani kwa hadhi ya DC anapata lakini pia kukosekana Uhuru wa siasa na hivyo kazi ya DC kubaki kunyamazisha yeyote mwenye mawazo yenye mrengo tofauti na chama Tawala.

Endapo taarifa hizi Zina ukweli Basi akina Mayala wanaweza kupata uteuzi kuziba nafasi zitakazokuwa wazi.
Ubaya mamlaka zetu hazitakubali umeacha,utasikia katumbuliwa.
 
Back
Top Bottom