Taasisi ya Kidini ya Spirit Word Ministry yafutiwa usajili

Taasisi ya Kidini ya Spirit Word Ministry yafutiwa usajili

Shida yako wewe ni wivu baada ya kuona libiblia lako linadadavuliwa mauongo yake.

Mmezoea kuwadanganya watu kwa kutumia hilo libiblia na kuchuma fedha za udanganyifu na ujanja ujanja.

Tunataka makanisa yanayohoji, na sio makanisa ya makondoo yanayofuata libiblia.
Kama we tu divesheni foo utaelewa Nini sasa.
Upo wapi uongo wa Biblia
 
View attachment 2639633
Wizara ya Mambo ya Ndani imesitisha usajili wa Jumuiya ya kidini iitwayo Spirit Word Ministry iliyopo eneo la Stakishari Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam baada ya kubainika kutoa mahubiri na mafundisho yenye mwelekeo wa kuhamasisha vitendo vya mapenzi ya jinsia moja.

Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni ameyasema hayo leo Jumatatu wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2023/24.

Masauni amesema katika kudhibiti na kupambana na vitendo vya mmomonyoko wa maadili Ofisi ya Msajili wa Jumuiya imesitisha shughuli za Jumuiya ya kidini iitwayo Spirit Word Ministry iliyopo eneo la Stakishari Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam.

“Jumuiya hiyo imefutiwa usajili kwa sababu ya kutoa mahubiri na mafundisho yenye mwelekeo wa kuhamasisha vitendo vya mapenzi ya jinsia moja na kutoa ujumbe wenye kuhafifisha jitihada za kupambana na vitendo vya ushoga nchini,”amesema.

Aidha, Masauni amesema taarifa zimekusanywa zinazohusu idadi ya vituo vya kulea watoto na shule zinazotoa mafundisho ya dini kwa watoto wadogo.

Amesema lengo ni kutambua idadi ya vituo au shule za bweni zinazotoa mafunzo yenye mwelekeo unaokinzana na maadili ya nchi yetu ikiwemo vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, ambapo katika mwaka 2023/24 wizara imepanga kuandaa mwongozo wa taratibu za kuabudu na ithibati ya taasisi zinazotoa elimu ya dini, kuimarisha ufuatiliaji na utendaji wa Jumuiya za Kidini na zisizokuwa za Kidini.

Pia katika mwaka huo watafanya ukaguzi na tathmini ya vihatarishi vya kiusalama kwa kushirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na kutoa mafunzo kwa Viongozi wa Jumuiya yatakayochangia kudumisha amani na utulivu nchini.
kuna siku nilimuangalia huyu mwamba akihubiri na kujibu maswali sikumuelewa kabisa. alikuwa akisisitiza DHAMBI NI DHANA TU
Kuna mtu aliuliza mbona mwanae anayeitwa Grace anavaa visuruali vya kubana kanisa, akajibu kuwa huo ni ushamba wa kutojua nini kinaendelea ulimwenguni, akasema mbona wazungu wanavaa vinguo vifupi
kilikuwa kituo cha kuuza bidhaa za mwanaye zikiitwa Grace product za urembo na kukuksanya sadaka za wajinga
 
Hivi shoga huwa anazaa?
Atazaaje Sasa wakat washaua nguvu zake.
Wameshindwa kwenye uzazi wa mpango na mavidonge na sindano zao wameleta ushoga ili kupunguza idadi ya watu Duniani hasa waafrika nalo watafeli Kama walivyofeli kwenye uzazi wa mpango
 
Jamaa yuko deep vizuri sana kufundisha neno ila ana vitu kadhaa simuungi mkono...
Aliomba msamaha kwa serikali na wananchi kwa maneno kuhusu ushoga etc....kwanini serikali isingempa onyo kuliko kumfungia. Aliomba msamaha.


Hamna ajuacho huyo na kwa kuwa alimkufuru Roho Mtakatifu, sasa kaparalyse yupo kitandani. Mungu adhihakiwi
 
Kwahiyo waumini waende wapi? Wengine walikua vibaka, je warudie zama zao?
Unajuaje kuwa wengine walikuwa vibaka?Halafuu,unataka serikali ifanyie kazi mambo ya kufikirika.Ikiwa hivyo mkuu,nothing will ever be done.

Sasa wewe ulitakaje,waachwe waendelee kuhamasisha ushoga?
 
Deep ipi zaidi ya upotoshi,anajiita Mpinga Kristo atakuwaje vizur Sasa, mafundisho yake yanauponda Ukristo.
Ni muhuni tu Hana hata shule ya dini kajikurupukia tu na mke wake wakajianzia kanisa linaitwa club,Sasa kanisa na club wapi na wapi
Akili kama zako huwezi kumwelewa yule mwamba, hasa wakiwa na jamaa mmoja(Oscar Obed).
Inahitaji uelewa wa hali ya juu sana, binafsi nimefatilia jinsi alivyokuwa akifundisha hasa miaka 3-5 iliyopita alikuwa akifundisha vizuri zaidi.

Alipo anza kuzungumzia ushoga na kubishana na torati waziwazi ndipo serikali ikawa macho zaidi, In short waliomfungia ni wale ambao wapo kinyume na mafundisho yake ambayo kimsingi niya KWELI kabisa tena ni UZIMA.
 
Kwa hapa nimeamini sasa serikali inataka kutokomeza huu ujinga.

Fukuza kabisa hizo takataka zikitaka kutoa mafunzo ziende kwa hao mabwana zao huko Merican
Una amini serikali inao uwezo wa kutokomeza ushoga, kwa taarifa yako kila wanapoweka juhudi zao za kijinga badala ya kupunguza wataongeza maradufu.
 
Atazaaje Sasa wakat washaua nguvu zake.
Wameshindwa kwenye uzazi wa mpango na mavidonge na sindano zao wameleta ushoga ili kupunguza idadi ya watu Duniani hasa waafrika nalo watafeli Kama walivyofeli kwenye uzazi wa mpango
Aliyekudanganya shoga hazalishii nani?? Afande Rama unamjua??
 
Back
Top Bottom