Tabia ya kupiga simu zaidi ya mara mbili inakera sana

Tabia ya kupiga simu zaidi ya mara mbili inakera sana

Hii sio kweli mkuu, mimi tangu siku nilipoanza kumiliki simu sijawahi kuwa napenda kupokea simu, mara nyingi huwa napendelea mtu anitumie SMS inayojieleza hususani ikiwa ni namba ngeni, mara nyingi nikiona mtu ananipigia simu zaidi ya mara mbili bila kutuma ujumbe mfupi huwa na assume hamna jambo la msingi hapo
Yeah sure.....Ila mi binafsi labda nisiwe na simu mkononi....Ila huwa naheshimu Sana mtu anayenipigia
 
Nasapoti mawazo ya mtaoa mada ( ), mtu at least upige mara 2 kama hauna jambo la dharura ukiona simu haijapokelewa basi jiongeze labda mwenye simu yuko bize au mazingira ambayo si rafiki kuongea na simu , hapo kaa piga muda mwingine baadae.

Inakera unakuta missed call 4 , 6 au 10 halafu mtu hana jambo la dharura au muhimu ambalo linahitaji kufanyia ndani ya muda huo aliopiga simu.
 
Ndo maana wengi wenu bado maskini sana. Ukipigiwa simu usiache kupokea. Kama mtu anaongea upuuzi mchane na kumwambia awe anapiga kuongea vya maana. KUTOPOKEA SIMU NI TABIA YA KIMASKINI. Kuna wale kama namba ni mpya hawapokei kabisa.. huu ni ujinga uliokubuhu. Kwenye huu ulimwengu wa digital mawasiliano ya aina zote usipuuze. Kuna wale ukituma message anasema sijaona.. upuuzi mtupu. Binti wa dukani kwangu alikuwa ana tabia ya kutoona message nikamwambia achague kuona message au kuacha kazi siku hiyohiyo ndo ghafla akabadili tabia.
 
FB_IMG_1723742158564.jpg
 
Huwa situmii SMS watu wazima mfano awe ndugu yake mzee au mama mzazi, sasa kuna ambao huwa nawapigia siku zote hawapokei hivyo napiga mara moja leo napiga mara nyingine after 2 weeks. Napiga kwa interval hiyohiyo mwaka unakata, miaka miwili inakata na hawapokei. Ila ukituma SMS anajibu hata siku nne baadae.

Nikaacha kwa sasa tunakutana misibani.
 
Una kwenye shughuli yeyote inayokunyima uhuru wa kupokea simu

Upo kazini busy na kazi kiasi cha kuepuka kupokea simu binafsi kwa sababu ni muda wa kumtumikia mwajiri ukihudumia wateja wake

Umeamua kuchukua muda wa kupumzika, umechagua kutokusiliza yeyote ili uache akili yako ipate utulivu.

Kiufupi ni mazingira yeyote ambayo yanakufanya usipokee simu, kwa sababu una uhuru wa kutumia simu yako.

Lakini unakutana na mbongo ambaye hana kiasi. Yeye akili yake inamtuma akupigie simu mpaka upokee, anapiga simu hata mara 10. Ajabu ni kwamba hana hata jambo la dharura na kwamba angekupigia mara moja kisha baadae ukiwa free umpigie. Hata common sense tu ya kwamba ngoja niache sms imsaidie kujua kiasi kuhusu shida yangu.

Inakera sana kuona mtu anapiga simu nyingi mfululizo bila sababu ya msingi. Kama simu yako haipokelewi tulia, missed call moja au mbili zinatosha
Ni kweli muasibu/mhasibu/muhasibu😂😂
 
Mm naongoza hasa nikiwa kwenye relationship iliyonishika😂😂😂😂 yaani Huwa Sina kias ni kukugongea calls muda wowote niwe mkweli😂😂

ila Kwa pipo zingine hapana Huwa sipig sana naweza hata nisifungue missed call hata siku 2 Tena namba ngeni ndio sizipendi
 
Back
Top Bottom