Tafadhali Rais Samia, Kikeke apewe Ukurugenzi TBC pengine ataleta mabadiliko

Tafadhali Rais Samia, Kikeke apewe Ukurugenzi TBC pengine ataleta mabadiliko

Aende ikulu akambadili greison,
ambaye amelewa madaraka
 
My friend!!! Lea chako. Usidanganywe na misemo ya zamani ya eti mpe mchawi akulelee mwanzo hatamdhuru.

Hiyo, haifanyi kazi siku hizi. Wachina wakipeleka watu wao kujifunza ng'ambo wanawawekea mapolisi wao huko huko wa kuwalinda na huku familia walizoziacha nyuma wanawekwa leani!!! Gadafi(R.I.P) naye alikuwa ameanza mtindo huo.
Huo mfumo unalipa!

Najua sauti ipo chini na msinitafute maneno eti niongeze sauti!
 
Mtangazaji mahiri Salim Kikeke siku ya jana aliaga rasmi, akitoa taarifa ya kuondoka katikaShirika la Habari la Uingereza baada ya kufanya kazi kwa kipindi cha miongo miwili (Miaka 20)

Kikeke kupitia matangazo ya Dira ya Dunia yanayorushwa na StarTV kwa hapa Tanzania aliaga rasmi kwamba matangazo ya jana ndiyo ya mwisho katika shirika hilo ambalo amefanya nalo kazi kwa miaka 20.

Kwa "experience" na "exposure" aliyoipata Kikeke kwa kipindi cha miaka 20 akiwa katika moja kati ya mashirika makubwa ya habari ulimwenguni nadhani ni muda wa Kikeke kurejea nyumbani, ni muda wa Taifa kufaidi matunda ya kijana wake, ni muda sahihi Rais Samia Suluhu afanye maamuzi yakayoleta mapinduzi pale TBC, ni muda sahihi KIKEKE AENDE KUHUDUMU KAMA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA HABARI TANZANIA (TBC).

Tumeona Zhura Yunus akipeleka ujuzi wake Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ya Tanzania na Charles Hillary akifanya hivyo kwa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Zanzibar, sasa tumtumia Kikeke pale TBC.

Haya ni maoni na mapendekezo yangu tu, wadau mnaonaje?
TBC ni Shirika la kumsifia Mwenyekiti wa CCM na serikali,kumbuka Tido alivyotaka kubadilisha Shirika Baba Kipara alivyokuja juu mpaka jamaa akaondoka.Nakumbuka wakati wa Tido tulikuwa tunaangalia ligi kuu ya England kama unakumbuka.
 
Kuacha kazi ya uhakika kwenye nchi zilizoendelea Ili uje kufanya kazi bongo inahitaji moyo sana
Ata Mimi huwa nashangaa,mtu unapiga mzigo ughaibuni na unavuta mshahara mrefu plus bonuses and insurance alafu unakuja Bongo kufanya kazi na vilaza.Kama yule Mfugale aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii, alikuwa Consultant kwenye kampuni kubwa kule Canada.
 
Aachane na TBC maana ilishapoteza uelekeo, ilishabaki kusifia uongozi na si kukosoa (balance story). Kikeke usiende TBC sifa yako itapungua.
 
Camera za TBC wakati wa ARDHIO kama vile wanatmia CAMERA ZA SIMU ZA TECNO. Watangazaji wanavyovaaa sasa hasa watangazaji wa kiume jamani kama wametoka kuazima makoti. Viatu vina vumbi. Masofa sijui wanachonga kwa fundi maiko. Huwa naangalia RWANDA TV jamani tukubali tupo usingizini TBC
Eti Fundi Maiko![emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Tatizo kubwa la TBC siyo Mkurugenzi na watangazaji.

Hata aende pale LISSU au Mbowe itabidi atangaze mambo ya CCM wanayotaka.

Ni aidha ukubaliane na maudhi yao au uache kazi.

  • Tunatekeleza
  • Kishindo Cha awamu ya 6
  • Safari ya Dodoma
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mtangazaji mahiri Salim Kikeke siku ya jana aliaga rasmi, akitoa taarifa ya kuondoka katikaShirika la Habari la Uingereza baada ya kufanya kazi kwa kipindi cha miongo miwili (Miaka 20)

Kikeke kupitia matangazo ya Dira ya Dunia yanayorushwa na StarTV kwa hapa Tanzania aliaga rasmi kwamba matangazo ya jana ndiyo ya mwisho katika shirika hilo ambalo amefanya nalo kazi kwa miaka 20.

Kwa "experience" na "exposure" aliyoipata Kikeke kwa kipindi cha miaka 20 akiwa katika moja kati ya mashirika makubwa ya habari ulimwenguni nadhani ni muda wa Kikeke kurejea nyumbani, ni muda wa Taifa kufaidi matunda ya kijana wake, ni muda sahihi Rais Samia Suluhu afanye maamuzi yakayoleta mapinduzi pale TBC, ni muda sahihi KIKEKE AENDE KUHUDUMU KAMA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA HABARI TANZANIA (TBC).

Tumeona Zhura Yunus akipeleka ujuzi wake Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ya Tanzania na Charles Hillary akifanya hivyo kwa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Zanzibar, sasa tumtumia Kikeke pale TBC.

Haya ni maoni na mapendekezo yangu tu, wadau mnaonaje?
Na ndo anakokwenda
 
Mawazo ya kijinga kabisa Ila Kwa vile ni muislamu mwenzake na mtoa mada fuvu lake Lina shida basi atapewa
Udini unakusumbua.Charles Hillary amepewa kazi Zanzibar ni muislamu?Hizo fikra muflis za kidini hazitakufikisha popote.Kikeke akiwa na sifa za kuajiriwa ana haki sawa na mtanzania yeyote yule.Ukiacha kutumia makamasi kufikiri utaelewa hivyo.
 
Mtangazaji mahiri Salim Kikeke siku ya jana aliaga rasmi, akitoa taarifa ya kuondoka katikaShirika la Habari la Uingereza baada ya kufanya kazi kwa kipindi cha miongo miwili (Miaka 20)

Kikeke kupitia matangazo ya Dira ya Dunia yanayorushwa na StarTV kwa hapa Tanzania aliaga rasmi kwamba matangazo ya jana ndiyo ya mwisho katika shirika hilo ambalo amefanya nalo kazi kwa miaka 20.

Kwa "experience" na "exposure" aliyoipata Kikeke kwa kipindi cha miaka 20 akiwa katika moja kati ya mashirika makubwa ya habari ulimwenguni nadhani ni muda wa Kikeke kurejea nyumbani, ni muda wa Taifa kufaidi matunda ya kijana wake, ni muda sahihi Rais Samia Suluhu afanye maamuzi yakayoleta mapinduzi pale TBC, ni muda sahihi KIKEKE AENDE KUHUDUMU KAMA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA HABARI TANZANIA (TBC).

Tumeona Zhura Yunus akipeleka ujuzi wake Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ya Tanzania na Charles Hillary akifanya hivyo kwa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Zanzibar, sasa tumtumia Kikeke pale TBC.

Haya ni maoni na mapendekezo yangu tu, wadau mnaonaje?
Kwani Mkurugenzi Mkuu wa TBC ametoka..kwanini unazungumzia sehem ambayo tayar Ina mtu na yeye ameshafanikiwa kulipaisha shirika Hilo sana....sijui unajua TBC imetoka wapi na Sasa ipo wapi..unaijua..?? Pia usidhan kukaa nje ndio assurance ya utendaji mzuri....hapana..it's subjective...uzoefu yes lakini pia na elimu kichwani
 
Hii inamaanisha Kila anaepitia BBC basi anafaa kuwa mkurugenzi!?....

Uongozi hasa wa ngazi ya juu ...unahitaji vipawa fulani specific si umaarufu....

Si kila mchezaji bora..ama mashuhuri...Anaweza kuwa kocha bora
Sure..!!! Nakubaliana nawe jomba
 
Hii inamaanisha Kila anaepitia BBC basi anafaa kuwa mkurugenzi!?....

Uongozi hasa wa ngazi ya juu ...unahitaji vipawa fulani specific si umaarufu....
Umemaliza.
Na ni aibu kama taifa.. yani tusubiri watu watoke BBC ndio wapate nyadhifa hizo .
Utaratibu wa hovyoo..
 
Back
Top Bottom