Tafuta mwanamke uoe, haya ndio maumbile tuliyoumbiwa

Tafuta mwanamke uoe, haya ndio maumbile tuliyoumbiwa

Huu uhamasishaji wako ungeenda sambamba na uhamasishaji wa kupunguza mahari ingekuwa bora zaidi ....mahari imekuwa kikwazo sana dada yangu......sio bara tu hata visiwani
Ukiona mahari imekushinda endelea kutafuta utakayomudu... Suala la mahari lipo chini ya mwanamke muolewaji... Yeye ndiye anayepanga aolewe au asiolewe... Na kwa kiasi gani...
 
Wanaopinga kuoa wengi Wana matatizo lazima tu hata kuwa vibaya kiuchumi pia ni tatizo japo sio dhambi😂😂
 
NIKUULIZE SWALI... Hivi akina lowasa na akina mzee wa vijisenti... Si mafisadi wale? Je ukiwauliza si watakwambia wanakula kutokana na utaalamu wao...

Kila mtu anaweza akapotosha maandiko ili mradi ajihalalishie kilichoharamishwa... Ila kimsingi wa kidini jambo hilo ni uovu mkubwa...

Mtumeﷺ alioa lakini hakuoa na kuacha acha... Japo uislaam unaruhusu kuacha... Lakini umeweka mipaka... Sio kuacha acha tu...
Mimi nimekulia kwenye mtaa wenye wa Islam wengi ,60% ya mabinti wa Kislam nilio cheza nao wameachwa na wamezalishwa. Najua unahamasha watu kuoa, ila ni vizuri kuwekeza nguvu kwenye kudumu kwenye ndoa na si kushindana kuoa sijui oa wawili au oa watatu mara wanne kesho unaanza kuwapiga chini mnawaumiza mabinti zenu kwani sio kwamba wote walio achwa labda wana tabia mbaya.
 
Ukiona mahari imekushinda endelea kutafuta utakayomudu... Suala la mahari lipo chini ya mwanamke muolewaji... Yeye ndiye anayepanga aolewe au asiolewe... Na kwa kiasi gani...
Aya wakina mawardat nyie endeleeni tuu kupamga mahari za million mzeeke kwa wazazi wenu🤣🤣🤣🤣
 
KWA JINSI ULIVYO ANDIKA UZI WAKO, NI KAMA WATU WANAOA KWA AJILI YA UNYUMBA.
UNYUMBA NI ASILIMIA 15 TU,YA MAISHA YA MAHUSIANO KUNA MAISHA MENGINE YENYE KUBEBA 85%

NAUNGA MKONO KAMPENI YA WANAUME KUACHA KUOA.
ZAMA ZETU HIZI KUOA NI KUJITAFUTIA MATATIZO YA KUJITAKIA
 
Ukiona mahari imekushinda endelea kutafuta utakayomudu... Suala la mahari lipo chini ya mwanamke muolewaji... Yeye ndiye anayepanga aolewe au asiolewe... Na kwa kiasi gani...
Kwa hiyo mimi nilieambiwa mahari kubwa nilitengenezewa mazingira ya kushindwa
 
Back
Top Bottom