DOKEZO TAHADHARI: Afisa TRA ahatarisha maisha ya wakazi Mbezi Juu Kwa Sanya kwa kujenga ghorofa 4 bila kibali, kwenye msingi dhaifu wa nyumba ya chini

DOKEZO TAHADHARI: Afisa TRA ahatarisha maisha ya wakazi Mbezi Juu Kwa Sanya kwa kujenga ghorofa 4 bila kibali, kwenye msingi dhaifu wa nyumba ya chini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kwa Dar huu ni mtihani WA kwanza WA Mheshimiwa Mkuu WA Mkoa Chalamilla, hao polisi WA usalama waliongezwa mara kumi na Makonda, sasa ni Muda muafaka kuwapunguza Kwa kupangiwa Majukumu mengine, ila Rushwa ya Hawa Ndugu inatisha
Mwenye ile Video ya Makonda atuwekee hapa kuhusu polisi
Chalamila bado anashangaa kama Rais anaweza kufa.
 
Ulishawahi kuona mtoto wa bilionea anaajiriwa hovyo hovyo ?.

Ukiuliza huyo Bon anafanya biashara gani na analipa kodi iasi gani utabaki kushangaa na kusikitika.
Leo hii hakuna trafic asiyekuwa na usafiri wa uhakika,nyumba nzuri kwasababu ya rushwa za barabarani,jiulize kwanini askari anyelinda bank hana hata baskeli !.

Nchi yetu inahitaji viongozi watakao kuwa tayari kupambana na mifumo ya rushwa.
Ukiwa mkweli hivi utaambiwa una wivu mara watz hatupendani na vijimisemo vingine vya hovyo....
Ila kweli ni lazima uzungumzwe kuliokoa hili taifa.
 
Nyumba ya chini isiyo na nguzo inabebeshwaje floors tatu na isianguke au mie ndiye sijaelewa maana ya nyumba ya chini.

Au nyumba ya chini aliyonunua jamaa ina maana lilikuwa jengo lenye ramani ya ghorofa (nguzo&slab) ila jamaa kalibebesha floors nyingi kuliko strength ya msingi.

BTW:Jengo kukosa vibali vya manispaa pekee haimaanishi lipo chini ya kiwango.
 
Ukiwa mkweli hivi utaambiwa una wivu mara watz hatupendani na vijimisemo vingine vya hovyo....
Ila kweli ni lazima uzungumzwe kuliokoa hili taifa.
Last week niliondoka Dar kupitia Bagamoyo kwenda Arusha na baadae Namanga.

Safari ilianza saa 1 asubuhi tulifika Namanga saa 11 jioni.Njiani tulisimamishwa na Askari wa usalama barabarani mara 21. 1. Mbezi 2 Bagamoyo mjini karibu na roundabout 3. Fukayosi 4. Mizani 5. Mbwewe 6. Mkata 7. Kabuku 8. Michungwani 9. Segera very close to michingwani. 10. KwaKomambo near Dar Express Highway 11. Bwiko 12. Mwanga kidogo tuli enjoy long safari without Trafic harassment 13. Maeneo kabla haujafika njia panda. 14. Ukipita daraja la kikavu ( Kikafu) 15. KIA 16. Kikatiti 17. Maji ya chai 18. Tengeru karibu na makazi ya Mzee Mtei. 19. Kwa mrefu 20. Sakina karibu na Azimio 21. Longido

Huu uwekezaji wa kujaza police barabarani kwaajili ya kukusanya rushwaa unamsaidia nini mtanzania kiuchumi,kisiasa au kijamii.
 
Taratibu za ujenzi wa ghorofa ni tofauti na ujenzi wa nyumba za kawaida. Kiashiria kimojawapo cha mtu anaejenga ghorofa kihalali ni uwepo wa lile bango la project. Yale mabango sijui yanaitwaje, ila pale utakuta jina na mmiliki, archtect, consultant, engineer etc... na project nzima hadi inakamilika inakuwa chini ya usimamizi wa hao watu. Ikitokea limeanguka, wataulizwa wao sio mmiliki. huwezi kuamka tuu na fundi wako unaemwamini mkaanza kujenga ghorofa. Mpaka mleta maada analeta dokezo hili inamaana kuna mapungufu kayaona.

Kuhusu alama nyekundu labda wenye mamlaka hawajaliona ama wanapozwa na afisaa wa TRA. Kwani likija kuangua wao watakuwepo? Au watu wakifa wao wanawahusu nini? Hii nchi ni zaidi ya uijuavyo[emoji846]
Sio lazima kuweka unaweza kuwa na kibali ila bango usiliandike na ukaendelea na kazi kama kawaida
 
Mamlaka husika zifike eneo husika kujiridhisha ni kweli,kwa akili ya kawaida huwezi kupandisha Ghorofa Nne bila kuwa na vibali husika.....na bila kufuata viwango vinavyohitajika siamini kama inaweza kuingia akilini kikawaida,upoteze pesa kwenye Ghorofa Lisilokuwa imara hizo pesa bora ukazitupe baharini ziende na maji.
 
Huyo jamaa sijui anabwabwaja nini, udaktari haukimbiliwi hakuna kilaza anapeleka pua kule hata awe mtoto wa tajiri namna gani.
Tanzania ndio mnaukuza udaktari kwamba wenye akili ndio wanasoma udaktari.
Nenda us,uk, Sweden hiyo ni kozi ya kawaida tu kama kozi nyingine,mfano mtu yoyote US akitaka kusoma udaktari anasoma vzr tu na anamaliza.
Uku kwetu Tanzania kwenye elimu ya kukomoana na hao prof uchwara ndio wanasababisha hiyo kozi iwe ngumu.
Usisifie sana udaktari kwamba ni kozi ngumu
 
Oyaa mbona jengo limesimama vyema tu? Nauhakika mafundi wa mtaani hawana uwezo wa kunyoosha ukuta hivyo. Hapa kuna tatizo na walalamikaji.
Wewe huna uzoefu katika ujenzi,unafikiri hizo Ghorofa unazoziona zimesimama wanaojenga Tofari ni mainjinia!

Engineer wanatoa maelekezo ni jinsi Gani Kazi ifanyike na Kusoma ramani ya jengo husika......wanaojenga tofari ni hawa mafundi wa mtaani wasiokuwa na elimu ya darasani kijana.

Huyu jamaa watakuwa wana mchoma tu kwa chuki binafsi....kiakili ya kawaida huwezi kujenga Ghorofa 4 kiholela bila kufuata vibali na viwango husika.
 
Tanzania ndio mnaukuza udaktari kwamba wenye akili ndio wanasoma udaktari.
Nenda us,uk, Sweden hiyo ni kozi ya kawaida tu kama kozi nyingine,mfano mtu yoyote US akitaka kusoma udaktari anasoma vzr tu na anamaliza.
Uku kwetu Tanzania kwenye elimu ya kukomoana na hao prof uchwara ndio wanasababisha hiyo kozi iwe ngumu.
Usisifie sana udaktari kwamba ni kozi ngumu
Kwamba Marekani ukisoma HGL unaweza kuwa daktari?
 
Back
Top Bottom