Taja mwiko, mila au desturi za kabila lenu au mahali ulipokulia

Taja mwiko, mila au desturi za kabila lenu au mahali ulipokulia

Daah kwetu ni mwiko

Kuingia chumbani kwa wazazi wako bila hodi

Ni mwiko kuua jongoo

Ni mwiko Kuitikia usiku ispokuwa anayekuita akuite mara tatu

Ni mwiko kukataa kula huku wenzanko wanakula(kama hauli ondoka eneo hilo)

Ni mwiko kupuliza chakula

Kwetu ni mwiko mke kumuita mama

Yapo mengi sana
 
janaba sio zuri, mama na baba hawamharibu mtoto ispokua mkishatombana mkamalizakama mnaona uvivu kuoga msimruke mtoto kitandani, anabemendeka ikiwa wazaz halisi wa huyo mtoto mmoja wapo akizini bila kuoga janaba
Ahaa kwa hiyo ishu ni janaba na si manii tena? Maana tulikaririshwa kua shahawa zikimuingia mama mtoto zinaenda moja kwa moja hadi kwenye maziwa ya mama. Mtoto anaponyonya hunyonya maziwa yaliyochanganyika na shahawa hivyo kumfanya adumae.
Tunahitaji uzi wa hii kitu ili tupate ufafanuzi kutoka kwa wachangiaji.
 
Ahaa kwa hiyo ishu ni janaba na si manii tena? Maana tulikaririshwa kua shahawa zikimuingia mama mtoto zinaenda moja kwa moja hadi kwenye maziwa ya mama. Mtoto anaponyonya hunyonya maziwa yaliyochanganyika na shahawa hivyo kumfanya adumae.
Tunahitaji uzi wa hii kitu ili tupate ufafanuzi kutoka kwa wachangiaji.
manii yanasafiri vipi kupitia uke na kufikia maziwa? umeona haiwezekani eh bas si kweli, umeshawahi kujaribu kulala baada ya kufanya mapenzi bila kuoga? of course mwili unakua mwepesi usingizi mzito lakini ukiamka unakuaje?? unakua unakuuma viungo sababu janaba lina mtindo huo ndio mana tunatakiwa kuoga baada ya tendo
 
Desturi ya nyumbani kwetu ukisonga ugali ukimaliza mwiko lazima uuoshe. Marufuku kuacha mwiko mchafu. Hata sijui ina maana gani ila nimekua nayo mpaka leo nikimaliza kusonga ugali lazima nioshe mwiko kabla hata chakula hakijafika mezani.
Hahaha😂😂😂, sio mwiko huo watu wanajua kutumia tafsida
 
Kwenye kabila letu:
1. Ni mwiko mwanamke aliyejifungua kula nyama ya kuku. Inasemekana akila kuku maziwa yatakuwa hayatoki.
2. Ni marufuku mjamzito kula mayai. Ikiwa atakula mayai, atamzaa mtoto kipara (asiyekuwa na nywele).
Na ukienda kuomba huku umebeba sukari, ikirudishwa inakuwa mkosi
 
Desturi ya nyumbani kwetu ukisonga ugali ukimaliza mwiko lazima uuoshe. Marufuku kuacha mwiko mchafu. Hata sijui ina maana gani ila nimekua nayo mpaka leo nikimaliza kusonga ugali lazima nioshe mwiko kabla hata chakula hakijafika mezani.
Vitu vingine viliwekewa vitisho tu ili kiwajengea tabia njema..kama hii ilikuwa ni kwa ajili ya afya na usafi...ukifanya hivyo huwezi kuwa na vyombo vichafu.
 
Hii thread nimeipitia yote sijaona wasukuma wenzangu ngoja niwaite waje waseme miiko kutoka usukumani ni ipi.
Kiranga, Nyani Ngabu, Ntuzu, Shimba ya Buyenze, Pascal Mayalla, Ng'wanamalundi, Ng'wanamangilingili ng'wanankamba NG'WANENE Manjagata G'taxiMashimba Son
Hahaha,

Umenikumbusha kuna siku moja miaka mingi iliyopita nilipost picha social media kutoka nyumbani kwangu Marekani nakaangiza vitu jikoni. Siku za ujana.

Ebwana wee, kuna country cousin mmoja alikuja juu sana akinishambulia kwamba nimevunja mwiko mkubwa sana hata kuingia jikoni!

Akaniambia sitakiwi hata kuingia jikoni.

Akasema "Bebe nang'hwe, ole nsumba ntale gete gete ahene!"

Sasa nilijishauri sana, mwiko huu nautekeleza vipi ikiwa nyumba yangu ina living room na morning room na jiko lipo katikati? Nikitaka kutoka living room kwenda morning room (which is really like a second living room) lazima nipitie jikoni?
 
1. Ni mwiko kuingia shamba la mtu la miwa au mahindi na kuvunja Kisha kuondoka nayo, inaruhusiwa kama ni miwa basi ikate kdhaa, kaa humohumo shambani kula Kisha uondoke au kama ni mahindi unaruhusiwa kuwasha moto kwenye hilo shamba Kisha kata mahindi yanayokutosheleza kula na kushiba Kisha choma kula maliza, zima moto na uondoke.

2. Mwiko kuhadithia hadithi mchana, utaota mkia.

3. Kwenye ukoo wetu kula utumbo wa mnyama yeyote mwenye miguu minne ni mwiko.

4. Ni mwiko Kupuliza moto kwa pamoja na ikitokea mmepuliza pamoja mmoja anatakiwa kutema mate juu na mwingine chini. Inaaminika msipofanya hivyo basi mtakuja kufa kwa siku moja.

5. Kuna mchezo mmoja tunauita 'buriburi' mnaketi chini kwa mzunguko kunakuwa na kimkaa au kijiwe unakificha kwa mikono nyuma na unaitoa mbele anayekufuatia anaonesha umekificha mkono gani, akipata unampa anaendelea yeye na anayemfuata hivyohivyo. Akikosa basi unakuwa ni ushindi na unaendelea kucheza. Sasa mkitaka kuanza kucheza ni lazima aanzishe mtu ambaye baba yake au mama yake alishatangulia mbele ya haki. Kama wote Wana wazazi basi mtoto wa mwisho kuzaliwa aliyepo hapo ndio huanzisha huo mchezo. Kwahiyo ni mwiko kwa mtu yeyote tu kuanzisha huo mchezo.

6. Kusonta kaburi na kidole ni mwiko.

7. Mwiko kulima usiku yaani jua likizama huruhusiwi kulima.

8. Kupanda mbegu shambani kwa kifaa chenye masizi ni mwiko, huashiria mbegu kutokuota maana ni kama unapanda mbegu zilizokaangwa.

9. Ni mwiko kumruka mtu, ikitokea inabidi urudi kwa kumruka kuelekea ulikotoka (kurudisha mruko [emoji4])

Ipo miiko mingi sana sana. Naweza Andika Kitabu.
 
Kwetu mtoto wa kwanza kwenye familia lazima atafutiwe mtu wakumuoa/kuolewa na bibi/babu mimi kila siku nampiga chenga bibi yangu nikienda bush namdanganyaga sijamalizia nyumba nadem nimemuona nayeye anatangaza kijijini uko mi mmewe
 
Back
Top Bottom