Pre GE2025 Tamaa ya Tundu Antipas Lissu, Kuutaka uwenyekiti wa CHADEMA taifa ni utashi wake binafsi au shinikizo kutoka nje ya nchi kwa wanao mbackup!

Pre GE2025 Tamaa ya Tundu Antipas Lissu, Kuutaka uwenyekiti wa CHADEMA taifa ni utashi wake binafsi au shinikizo kutoka nje ya nchi kwa wanao mbackup!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Chairman wa sasa wa Chadema Taifa, Freeman Aikaeli Mbowe, akizungumzia kusudio la Tundu Antipas Mughwai Lisu kugombea uenyekiti wa Chadema Taifa, kwa namna yoyote ile atakua ameingia kwenye trap au mtego wa kisayansi alotegwa na kukoleza au kuzidisha joto, uhasama na vita ya madaraka ndani ya chadema hususani dhidi ya nafasi ya uenyekiti wa Chadema Taifa.

Tundu Lisu akijibiwa azma yake hiyo na chairman Freeman Mbowe, atakua amefanikiwa kumuingiza mbowe mtegoni, na ndipo sasa mambo na madudu mengine mazito zaidi na muhimu sana dhidi ya chairman Mbowe yataibuliwa na kuwekwa hadharini.

Na hilo ndilo lengo hasa la Tundu Lisu. Na huo ndio utakua mwanzo wa safari ya kujiengua chadema na kuelekea kwingineko kula maisha au kupata nafasi na fursa ya kugombea urasi uchaguzi mkuu ujao Oct 2025, endapo hoja na tuhuma zake dhidi ya chairman Mbowe zitapanguliwa kwa ufasaha.

Nadhani Tundu Lisu ana mambo mengi mno moyoni dhidi ya uongozi wa chadema Taifa, hata hivyo, mpaka kufikia uamuzi wa kutaka awe mwenyekiti wa Chadema Taifa. Tundu Antipas Mughwai Lisu, anahitaji mambo mawili tu kwenye vita hii. Ni awe mwenyekiti wa Chadema Taifa, au kujiengua chadema na kutafuta fursa za kisiasa kwenye vyama vingine vya siasa nchini.

Na hili linaweza kua ni shinikizo kutoka nje ya nchi, hasa kutoka kwa wale wanao wanaombackup yeye na familia yake huko ughaibuni. Ni dhahiri awali alionekana hayupo serious.

Kukaa kimya kwa Freeman Aikaeli Mbowe, kutampasua kichwa na kutamdhoofisha sana Tundu Lisu anaetamani majibizano, na hapo mbowe atakua ameupiga mwingi zaidi, akiendelea na harakati zake za kutetea kiti chake cha uenyekiti wa Chadema Taifa, kadiri ya mipango mikakati yake na ratiba zake, bila kumzungumzia Lisu hata kidogo.

Kwa kufanya hivi, Freeman Mbowe atakua amemkwaza Lisu, na kumlazimisha amchokonoe zaidi zaidi au kujaribu kupaint uongozi wa Mbowe kama kitu ambacho kiliidumaza chadema na kwamba uongozi wake uligubikwa na sintofahamu nyingi sana.

Na Mbowe akiendelea kukaa kimya zaidi bila kujibu chochote, atakua amemchanganya zaidi Lisu na kumjaza hofu ambayo itamfanya atathmini upya mpango na mtego wake huu wa kumchefua chairman Mbowe ili eti yeye aonekane bora zaidi.

Kiufupi,
katika mpambano na mgawanyiko huu ndani ya chadema, kama wadau wa bobevu, tunajifunza na tutabaini wazi nani miongoni mwa mafahali hawa wawili ndani ya chadema, anatumia sayansi ya siasa kufanya siasa na nani anatumia mihemko, chuki na kukurupuka katika kutafuta uongozi wa kisiasa ndani ya chadema.

Unadhani ni nani aliemshinikiza Lisu kuachana na kugombea umakamu mwenyekiti wa Chadema Taifa, na kuamua kumendea uenyekiti wa Chadema Taifa?

Je, ni shinikizo kutoka ndani ya nchi au nje ya nchi?🐒

Mungu Ibariki Tanzania.
Jambo hili la uenyekiti wa Lisu limekivuruga sana chama chetu CCM
Naona thinktank wetu wa mitandaoni mnapoteana sasa
 
kumbe wakati mwingine huwa una maono ya maana kabisa kisiasa gentleman,dah!🐒

Kwani bila kupewa nafasi angejukanaje? Kila mtu anataka nafasi afanye yake hata chawa wote wanapigania nafasi kwa kukesha hapa waonekane kwa walipaji na wateuaji!
 
Chairman wa sasa wa Chadema Taifa, Freeman Aikaeli Mbowe, akizungumzia kusudio la Tundu Antipas Mughwai Lisu kugombea uenyekiti wa Chadema Taifa, kwa namna yoyote ile atakua ameingia kwenye trap au mtego wa kisayansi alotegwa na kukoleza au kuzidisha joto, uhasama na vita ya madaraka ndani ya chadema hususani dhidi ya nafasi ya uenyekiti wa Chadema Taifa.

Tundu Lisu akijibiwa azma yake hiyo na chairman Freeman Mbowe, atakua amefanikiwa kumuingiza mbowe mtegoni, na ndipo sasa mambo na madudu mengine mazito zaidi na muhimu sana dhidi ya chairman Mbowe yataibuliwa na kuwekwa hadharini.

Na hilo ndilo lengo hasa la Tundu Lisu. Na huo ndio utakua mwanzo wa safari ya kujiengua chadema na kuelekea kwingineko kula maisha au kupata nafasi na fursa ya kugombea urasi uchaguzi mkuu ujao Oct 2025, endapo hoja na tuhuma zake dhidi ya chairman Mbowe zitapanguliwa kwa ufasaha.

Nadhani Tundu Lisu ana mambo mengi mno moyoni dhidi ya uongozi wa chadema Taifa, hata hivyo, mpaka kufikia uamuzi wa kutaka awe mwenyekiti wa Chadema Taifa. Tundu Antipas Mughwai Lisu, anahitaji mambo mawili tu kwenye vita hii. Ni awe mwenyekiti wa Chadema Taifa, au kujiengua chadema na kutafuta fursa za kisiasa kwenye vyama vingine vya siasa nchini.

Na hili linaweza kua ni shinikizo kutoka nje ya nchi, hasa kutoka kwa wale wanao wanaombackup yeye na familia yake huko ughaibuni. Ni dhahiri awali alionekana hayupo serious.

Kukaa kimya kwa Freeman Aikaeli Mbowe, kutampasua kichwa na kutamdhoofisha sana Tundu Lisu anaetamani majibizano, na hapo mbowe atakua ameupiga mwingi zaidi, akiendelea na harakati zake za kutetea kiti chake cha uenyekiti wa Chadema Taifa, kadiri ya mipango mikakati yake na ratiba zake, bila kumzungumzia Lisu hata kidogo.

Kwa kufanya hivi, Freeman Mbowe atakua amemkwaza Lisu, na kumlazimisha amchokonoe zaidi zaidi au kujaribu kupaint uongozi wa Mbowe kama kitu ambacho kiliidumaza chadema na kwamba uongozi wake uligubikwa na sintofahamu nyingi sana.

Na Mbowe akiendelea kukaa kimya zaidi bila kujibu chochote, atakua amemchanganya zaidi Lisu na kumjaza hofu ambayo itamfanya atathmini upya mpango na mtego wake huu wa kumchefua chairman Mbowe ili eti yeye aonekane bora zaidi.

Kiufupi,
katika mpambano na mgawanyiko huu ndani ya chadema, kama wadau wa bobevu, tunajifunza na tutabaini wazi nani miongoni mwa mafahali hawa wawili ndani ya chadema, anatumia sayansi ya siasa kufanya siasa na nani anatumia mihemko, chuki na kukurupuka katika kutafuta uongozi wa kisiasa ndani ya chadema.

Unadhani ni nani aliemshinikiza Lisu kuachana na kugombea umakamu mwenyekiti wa Chadema Taifa, na kuamua kumendea uenyekiti wa Chadema Taifa?

Je, ni shinikizo kutoka ndani ya nchi au nje ya nchi?🐒

Mungu Ibariki Tanzania.

Umekuwa msemaji wa Tundu Lisu?
 
Yani tangu jana kila chawa anaanzisha angalau uzi mmoja au zaidi kwa siku na vijihoja vyake ishakuwa "ntoke vipi yani" mmepandishiwa dau nini?
kueleza ukweli bana hakuchoshi kabisa gentleman,

hivi nyie manyumbu,
ukurupukaji, mihemko na makasiriko dhidi ya maelezo ya ukweli kama ya kwenye hoja mezani hayawachoshi kweli?

Ila Lazima roho zitakua zinawauma sana dah. Pole 🐒
 
Hatari sn
Kila hoja na kila swali lina majibu ndio uzuri! Ulipata ile lecture ya jana lakini mkuu? Naamini uliondoka na kitu hata kama ni kidogo! Taifa zima lilibaki kimya linapata somo live toka mlimani city! Hata mama yetu alikuwa live anasikiliza Simba akifundisha namna ya kuunda taasisi na kufanya mifumo ifanye kazi!
 
Anajua lakin anachotaka?
umakamu mwenyekiti au uenyekiti Taifa au vyote kwa pamoja?

sio tamaa na shinikizo la mabwenyenye ya magharibi yanayombackup kama kibaraka wao Africa kwa mgongo wa Chadema Tanzania,kweli?🐒
Unafikiri Hao CCM Si vibaraka wa Uingereza na Marekani ? Mbona wanaikandia Zanzibar miaka yote toka uvamizi wa 1964
 
kueleza ukweli bana hakuchoshi kabisa gentleman,

hivi nyie manyumbu,
ukurupukaji, mihemko na makasiriko dhidi ya maelezo ya ukweli kama ya kwenye hoja mezani hayawachoshi kweli?

Ila Lazima roho zitakua zinawauma sana dah. Pole 🐒

Mkuu umetoa hoja gani mpya? Hebu rudia kusoma maandiko yako, halafu jipime ila usijibu!😀
 
Umekuwa msemaji wa Tundu Lisu?
kwanza,
ni kujifunza kati ya mafahali hawa wawili ana tamaa na uchu wa madaraka na vyeo.

Pili,
ni kujifunza nani kati ya mafahali hawa wawili anatumia bongo kali, sayansi ya siasa na nani amekurupuka tu.

Tatu na mwisho kwa uchache,
ni muhimu kujua tamaa hii ni utashi binafsi au shinikizo la mabwenyenye ya magharibi kujiingiza kwenye siasa za Tanzania.

Ni muhimu kufuatilia mambo haya bila mihemko gentleman. Focus in learning and understanding, itakusaidia sana 🐒
 
Unafikiri Hao CCM Si vibaraka wa Uingereza na Marekani ? Mbona wanaikandia Zanzibar miaka yote toka uvamizi wa 1964
Relax gentleman,
twende pole pole kamanda.

Ni muhimu kua makini na dhamira za huyu muungwana ambae mwili uko Tanzania, akili na moyo viko huko magharibi.

Surely,
Chairman wa Chadema wa sasa anaweza kuthubutu kuiacha Chadema mikononi mwa vibaraka wa mabwenyenye ya magharibi?

tuwe wakweli tu drugu zangu, can it real happen?🐒
 
Swali ni madongo aliyorusha je ni kweli ama si kweli?
Kuna genge ndani ya CDM wamejivika umwinyi na ndo wanapambana siku zote mwenyekiti abaki ili waendelee kutafuna asali ya chama.

Kumpokea EL TU 2015 ilitosha bwana Mbowe akae pembeni,hata safi yote ya CDM iliyokua moto kabaki yeye tu labda na lisu kwa mbaali. Sasa hivi CDM inaendeshwa kwa one man army na machawa wakifanya back up,watu wakibutuliwa kwenye local govt election wanaona wanaonewa kumbe uhuni ni mkubwa sana ndani ya CDM.
Kunya anye kuku,akinya bata kaharisha.

CCM-63yrs madarakani
Mbowe-20yrs uenyekiti.
Bado unainyooshea kidole chama tawala kitoke wakati tatzo lipo ndani humo
 
Relax gentleman,
twende pole pole kamanda.

Ni muhimu kua makini na dhamira za huyu muungwana ambae mwili uko Tanzania, akili na moyo viko huko magharibi.

Surely,
Chairman wa Chadema wa sasa anaweza kuthubutu kuiacha Chadema mikononi mwa vibaraka wa mabwenyenye ya magharibi?

tuwe wakweli tu drugu zangu, can it real happen?🐒
Hao mambwanyenye ndo wamemsanua kua chairman ni pazia pale,Akili ipo CCM mwili upon CDM, intelligence ya hao mabwanyenye bado ni ya kutilia shaka???
Chairman tangu 2015 wanachama na raia wengi wameendelea kutathmini huyu mtu ni WA aina gani,yupo sawa kweli?
 
Mkuu umetoa hoja gani mpya? Hebu rudia kusoma maandiko yako, halafu jipime ila usijibu!😀
Gentleman,
ni muhimu sana ukawa mtulivu na kwakweli mstahimilivu katika kupata elimu na kuongeza uelewa na ufahamu wa kibobevu kutoka kwenye hoja mahususi ninazowasilisha humu jukwaani kwa hiyari,

Muhimu ni kuacha uvivu katika kusoma na kupata content mahususi.

kwa kuhitimisha,
ni muhimu sana wadau wa JF kujua na kuelewa hii taama na uchu wa Lisu kuutaka uenyekiti wa Chadema Taifa hauna shinikizo la kimataifa hasa kutoka kwa mabwenyenye ya magharibi yanayombackup?

Lakini pia,
hii ni fursa muhimu sana kwa wadau kujifunza kati ya hawa mafahali wawili, nani anatumia sayansi ya siasa na nani anakurupuka katika kufikia azma zao za siasa?

mambo haya ni muhimu sana gentleman kuliko mihemko 🐒
 
Kila hoja na kila swali lina majibu ndio uzuri! Ulipata ile lecture ya jana lakini mkuu? Naamini uliondoka na kitu hata kama ni kidogo! Taifa zima lilibaki kimya linapata somo live toka mlimani city! Hata mama yetu alikuwa live anasikiliza Simba akifundisha namna ya kuunda taasisi na kufanya mifumo ifanye kazi!
Uhai wa chama kwanza
 
Back
Top Bottom