Uchaguzi 2020 Tamaa za Wateule wa Rais kutia nia Ubunge zitawaponza wengi. Ushahidi huu hapa wa Rais Magufuli na Humphrey Polepole

Wahaya wana msemo "Mwanaume ana geuka kitandani lakini hageuki kauli"
Nini maana yake? Kwamba anayeigeuka kauli yake sio mwanaume bali ni mwanamke au shoga.
Nasubiri kama kwa bahati mbaya/nzuri jamaa akapewa tena kitu jee atakuwa mwanaume kama walivyo wahaya kuwa wanalinda kauli zao?
Maana walio kiuka kauli yake hiyo ni wengi akiwamo mwanae mpendwa
 
Uwingi na aina (confidence na view) ya watia nia wa chama tawala unaonyesha mwelekeo wa nchi hii kisiasa. Huo ndio ukweli kwa Karne hii, tuache kufarajiana
Umeandika point ambayo mataga na akili zao kiduchu hawawezi kuelewaa.... Great thinker
 
Asije akapotea kabla hajafika ukumbini... CCM bana!!
 
Ndugu salaam,

Kama mlivyoshuhudia kuwa Rais Magufuli alilieza taifa na chama chake kuwa akishamteua MTU cheo chochote basi aridhike na cheo hicho, kauli hiyo ilikuwa na lengo la kuwakataza wateule kutoingia majimboni kusaka ubunge.

Kufuatia agizo hilo baadhi wametii hasa wale waoga na ambao hawana ukaribu sana naye. Wale wenye ukaribu naye hawajatii tamko hilo kwani wamejitokeza majimboni na pia JPM kama anavyopenda kuitwa aliongeza kuwa kama mtu aliyemteua akikaidi agizo hilo basi aombe siku ya kupitisha majina akute siku hiyo ameamka vizuri la sivyo atakatwa jina.

Baada ya baadhi kukaidi si kwamba hawa waliokaidi wamepata baraka zake? Na kama hawajapata baraka zake watakatwa?na kama wakipita bika kukatwa hii haionyeshi kwamba huyu jpm ni mbaguzi? Mbaguzi Kwa maana wengine atakuwa amewaachia wajinafasi ili wengine amewafungia kwenye chupa.

Lakini pia, hawa watia nia waliodharau agizo la JPM wametia nia na makada wengine ambao sio wateule, ikitokea kada kamzidi mteuliwa jeuri je atapitishwa?na kama asipopitishwa atakubali kupigia tarumbeta chama miaka nenda rudi ili hali hathaminiki?

Achilia mbali Malaya wa kisiasa waliojiuza, nao atalazimisha wapitishwe walipwe fadhila? Na kama wakipitishwa kwa lazima, hawa makada waliojenga chama kwa jasho na damu wataridhika kukatwa sababu ya wahamiaji?

Naiona kauli halisi ya mwalimu Nyerere Kwa mbali ikijongea chamani kwenye kijani kuwa "Upinzani wa kweli utatoka ndani ya kijani"

CCM mtatoboa October 2020?

Swelana.
 
Imetendewa haki.

Your browser is not able to display this video.
 
Alisema itategemeana ataamkaje akiamka poa atawapitsha tu na hata onekana mbaguzi kwasababu hapo kaweka ooption mbili anaweza tumia option yoyote inategemeana kaamkaje tu!
 
Mkuu hawa wanatuchezea akili tu huyo makonda hajaenda kigamboni kwa bahwti mbaya ni mkakati huo
 
Kashachukua fomu na hawatamfanya chchte atashinda kwa kishindo
 
Utanifanyizia nini?

Kule ‘kwetu’ kuna misemo kama Usinipangie, mimi siambiwagi hivyo (natawilagwa iyeneyo)!

Mods mnajipa majukumu yasiyo yenu dadadeeki!
 
Mwisho wa siku ni nani atakayehamua hatma ya kugombea au kutogombea? Mwisho wa siku maamuzi ya mwisho yana nani?
 
Hiyo kanuni au ukipenda taratibu ipo kwaajili ya watu wengine si mtoto pendwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…