TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Tumepokea taarifa kwa hatua zaidi
WATUMIAJI WA UMEME WA LUKU CHUKUENI TAHADHARI MAPEMA
Wakuu natumaini mmeshinda salama.
Kwa habari nilizozipata leo ni kuws mkataba kati ya Tanesco na Maxcom (MaxMalipo) wa kuuza token za umeme (LUKU) utakwisha mwisho wa wezi huu na hakuna dalili kwamba wataongeza mkataba siku za karibuni.Ikumbukwe kuwa Maxcom ndio wenye mkataba wa kuuza umeme kwa wateja wa Tanesco na hivyo wao pia wameingia ubia na makampuni ya simu kama Tigo, Voda n.k na hivyo kuisha kwa mkataba wa Maxcom ina maana hutaweza pia kununua kwenye simu.

Hii ina maana kuwa, baada ya tarehe 31 March ukitaka umeme lazima uende katika office ya Tanesco ili kupata huduma hii. Hata wale vendors maarufu wa Tanesco waliopo mitaani hawatakuwa na uwezo wa kuuza umeme. Hivyo wakuu naomba kuwapa tahadhari kwa wale wenye sehemu za biashara wanaotumia LUKU na watumiaji wote wa LUKU hata wa majumbani mchukue tahadhari mapema kabla hali ya taharuki haijazuka ukizingatia sikukuu hii ya pasaka inakuja hakuna ambae angependa kukaa giza siku kadhaa kisa ameshindwa kununua LUKU.

Mpaka sasa hakuna suluhisho lililofikiwa zaidi ya kuwa LUKU itauzwa katika ofisi ya Tanesco na hivyo nawaasa ndugu zangu mnunue kuanzia leo na kesho umeme wa kutosha hata week kadhaa maana kuna kadhia inakuja hapa mbeleni.
Ukiupata ujumbe huu tafadhali usiwe mchoyo mshtue na jirani yako.

Mtag rafiki yako ili ajue asije kukuwekea jam nyumbani kwako kucharge simu au kupiga pasi.
Asanteni

Hii taarifa hapo juu ina ukweli? Tuambieni ukweli ili tuchukue tahadhari mapema
TANESCO
 
nimepata tetesi kua tanesco mnasitisha mkataba wenu na maxcom ambao waliingia mkataba ma makampun ya sim ikatuwezesha kununua kupitia tigo pesa au mpesa na nimepata taarifa za juu kwa juu kua mkimaliza mkataba hatutoweza tena kununua umeme kwenye cm hadi tuje tanesco je ni kweli tetes hizi au uzush naomba ufafanuz
 
*WATUMIAJI WA UMEME WA LUKU CHUKUENI TAHADHARI MAPEMA*
Wakuu natumaini mmeshinda salama.
Kwa habari nilizozipata leo ni kuws mkataba kati ya Tanesco na Maxcom (MaxMalipo) wa kuuza token za umeme (LUKU) utakwisha mwisho wa wezi huu na hakuna dalili kwamba wataongeza mkataba siku za karibuni.Ikumbukwe kuwa Maxcom ndio wenye mkataba wa kuuza umeme kwa wateja wa Tanesco na hivyo wao pia wameingia ubia na makampuni ya simu kama Tigo, Voda n.k na hivyo kuisha kwa mkataba wa Maxcom ina maana hutaweza pia kununua kwenye simu.
Hii ina maana kuwa, baada ya tarehe 31 March ukitaka umeme lazima uende katika office ya Tanesco ili kupata huduma hii. Hata wale vendors maarufu wa Tanesco waliopo mitaani hawatakuwa na uwezo wa kuuza umeme. Hivyo wakuu naomba kuwapa tahadhari kwa wale wenye sehemu za biashara wanaotumia LUKU na watumiaji wote wa LUKU hata wa majumbani mchukue tahadhari mapema kabla hali ya taharuki haijazuka ukizingatia sikukuu hii ya pasaka inakuja hakuna ambae angependa kukaa giza siku kadhaa kisa ameshindwa kununua LUKU. Mpaka sasa hakuna suluhisho lililofikiwa zaidi ya kuwa LUKU itauzwa katika ofisi ya Tanesco na hivyo nawaasa ndugu zangu mnunue kuanzia leo na kesho umeme wa kutosha hata week kadhaa maana kuna kadhia inakuja hapa mbeleni.
Ukiupata ujumbe huu tafadhali usiwe mchoyo mshtue na jirani yako. Mtag rafiki yako ili ajue asije kukuwekea jam nyumbani kwako kucharge simu au kupiga pasi.
Asanteni

Hii taarifa hapo juu ina ukweli? Tuambieni ukweli ili tuchukue tahadhari mapema
TANESCO
Ndugu mpendwa mteja taarifa yenye ukweli inatoka kwetu na hii taarifa hatujui umeitoa wapi, tafadhali zingatia taarifa zetu na kuacha kusambaza hizi
 
nimepata tetesi kua tanesco mnasitisha mkataba wenu na maxcom ambao waliingia mkataba ma makampun ya sim ikatuwezesha kununua kupitia tigo pesa au mpesa na nimepata taarifa za juu kwa juu kua mkimaliza mkataba hatutoweza tena kununua umeme kwenye cm hadi tuje tanesco je ni kweli tetes hizi au uzush naomba ufafanuz
Ndugu mpendwa mteja endelea kufurahia huduma zetu na taarifa zote zinazohusu manunuzi ya umeme au Tanesco zinatolewa na ofisi yetu ya Uhusiano hivyo hiyo sio yetu
 
Wilaya ya Ubungo inatatizo kubwa sana la Umeme. Kila Siku Umeme unakatika.. Watu wanapoteza muda mwingi sana pale kusubilia Huduma. Mfano.

Vitambulisho vya taifa na huduma nyingine za namna hiyo. Naiomba Wilaya na Tanesco mumalize hili tatizo. Ni shida kwa wananchi.
 
Mekata umeme tangia jana asubuhi, jana siku nzima hakuna umeme, usiku mzima hamjaleta, la leo tena hakuna, hata taarifa hakuna, au mmejisahau kua mmekata umeme huku baruti? Fanyeni mchakato mturudishie umeme.
 
Wilaya ya Ubungo inatatizo kubwa sana la Umeme. Kila Siku Umeme unakatika.. Watu wanapoteza muda mwingi sana pale kusubilia Huduma. Mfano.. Vitambulisho vya taifa na huduma nyingine za namna hiyo. Naiomba Wilaya na Tanesco mumalize hili tatizo. Ni shida kwa wananchi.
Ndugu mpendwa mteja kulikuwa na tatizo kubwa jana hatua stahiki zimechululiwaa
 
Hatua zipi? Mnarudisha umeme kisha mnakata....mkipigiwa simu hamtaki kupokea. Mnatukwaza sana sisi wateja.

Tangu jana saa sita mchana mpaka sasa hivi umeme haujarudi majumbani kwetu sisi wakazi wa Mbezi Msuguri, Saranga, Malamba mawili
 
Tangu jana saa sita mchana mpaka sasa hivi umeme haujarudi majumbani kwetu sisi wakazi wa Mbezi Msuguri, Saranga, Malamba mawili
Tanesco wasanii na huyu kichaa anayetujibu humu hana akili. Anaona sisi watoto tunapoteza muda kumuuliza yeye anakuja na cheap response. Pumbavu kabisa
 
Tanesco wasanii na huyu kichaa anayetujibu humu hana akili. Anaona sisi watoto tunapoteza muda kumuuliza yeye anakuja na cheap response. Pumbavu kabisa
TAARIFA YA KUOMBA RADHI WATEJA WETU WA KIMARA, MBEZI, KIBAMBA NA KILUVYA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi Wateja wake wa maeneo ya Kimara, Mbezi, Kibamba na Kiluvya kwa kukosa huduma ya umeme.

*SABABU*
Ni kutokea kwa hitilafu katika njia zetu za umeme (Nordic 1 na Nordic 2).

*HATUA ZILIZOCHUKULIWA*

Kufanyiwa majaribio (Testing) kifaa cha kidhibiti mkondo (Breaker)

Kufanyiwa kwa majaribio kwa "cable" ya Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ubungo .

Imelazimu kuzimwa kwa njia hizi za umeme ili kazi hii ifanyike kwa ufanisi zaidi.

Wataalam wetu na mafundi wanaendelea na jitihada za kuhakikisha umeme unarejea katika hali yake ya kawaida kwa haraka.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Kwa mawasiliano

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz, mitandao ya kijamii:

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook Tanesco Yetu

IMETOLEWA NA:

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

MACHI 27, 2018
 
TAARIFA YA KUOMBA RADHI WATEJA WETU WA KIMARA, MBEZI, KIBAMBA NA KILUVYA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi Wateja wake wa maeneo ya Kimara, Mbezi, Kibamba na Kiluvya kwa kukosa huduma ya umeme.

*SABABU*
Ni kutokea kwa hitilafu katika njia zetu za umeme (Nordic 1 na Nordic 2).

*HATUA ZILIZOCHUKULIWA*

Kufanyiwa majaribio (Testing) kifaa cha kidhibiti mkondo (Breaker)

Kufanyiwa kwa majaribio kwa "cable" ya Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ubungo .

Imelazimu kuzimwa kwa njia hizi za umeme ili kazi hii ifanyike kwa ufanisi zaidi.

Wataalam wetu na mafundi wanaendelea na jitihada za kuhakikisha umeme unarejea katika hali yake ya kawaida kwa haraka.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Kwa mawasiliano

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz, mitandao ya kijamii:

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook Tanesco Yetu

IMETOLEWA NA:

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

MACHI 27, 2018
Sasa why hamtangazi mapema? Mnajua hasara mnayotuingiza kuharibu vyakula vyetu kwenye mafriji?
 
Alafu pia muache kuleta na kukata, umeme unakuja dakika 10 unakata, kama leo umesgakatika mara sita
 
*TAARIFA KWA UMMA*

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wote wanao tumia mita za malipo ya kabla yaani (LUKU) kuwa, kuanzia April 2, 2018 TANESCO itahamia rasmi katika mfumo wa malipo wa Serikali ujulikanao kama Government e-Payment Gateway (GePG) kama matakwa ya sheria kwa Taasisi za Serikali.

TANESCO ikiwa miongoni mwa Taasisi za Serikali, itaanza kutumia mfumo huu kwa kufanya mauzo ya LUKU kupitia ofisi za TANESCO, Kampuni za simu pamoja na Benki zote zinazofanya mauzo ya LUKU kupitia huduma za kibenki.

Serikali kwa kushirikiana na Wataalamu wa TANESCO itahakikisha kuwa mfumo huu unafanya kazi bila kuathiri manunuzi ya LUKU. Ifahamike kwamba, TANESCO ni miongoni mwa Taasisi za Serikali zitakazotumia mfumo huu mpya na hadi hivi sasa Taasisi nyingine za Serikali zimeshaanza kutumia kwa mafanikio, baadhi ya Taasisi hizo ni Polisi, Brella, Ardhi, TRA pamoja na Mamlaka za maji.

TANESCO inapenda kuwahakikishia wateja wote kuwa mbali na Kampuni za simu ofisi zote za Shirika na vituo vya mauzo ya LUKU vitaendelea kutoa huduma katika kipindi chote cha Sikukuu ya Pasaka.

TANESCO ‘‘Tunayaangaza Maisha yako’’

Kwa mawasiliano

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz, mitandao ya kijamii:

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook Tanesco Yetu

IMETOLEWA NA:

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

MACHI 27, 2018
 
TAARIFA YA KUOMBA RADHI WATEJA WETU WA KIMARA, MBEZI, KIBAMBA NA KILUVYA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi Wateja wake wa maeneo ya Kimara, Mbezi, Kibamba na Kiluvya kwa kukosa huduma ya umeme.

*SABABU*
Ni kutokea kwa hitilafu katika njia zetu za umeme (Nordic 1 na Nordic 2).

*HATUA ZILIZOCHUKULIWA*

Kufanyiwa majaribio (Testing) kifaa cha kidhibiti mkondo (Breaker)

Kufanyiwa kwa majaribio kwa "cable" ya Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ubungo .

Imelazimu kuzimwa kwa njia hizi za umeme ili kazi hii ifanyike kwa ufanisi zaidi.

Wataalam wetu na mafundi wanaendelea na jitihada za kuhakikisha umeme unarejea katika hali yake ya kawaida kwa haraka.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Kwa mawasiliano

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz, mitandao ya kijamii:

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook Tanesco Yetu

IMETOLEWA NA:

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

MACHI 27, 2018
lakini huku mbezi hili tatizo huwa haliishi tu maana mmeanza kutukatia umeme kitambo sana tunawavumilia tu......
 
Mekata umeme tangia jana asubuhi, jana siku nzima hakuna umeme, usiku mzima hamjaleta, la leo tena hakuna, hata taarifa hakuna, au mmejisahau kua mmekata umeme huku baruti? Fanyeni mchakato mturudishie umeme.
Ngoja nikusaidie kuwaita, TANESCO njooni huku mnaitwa
 
TAARIFA KWA UMMA

Jana nimeleta uzi hapa kutoa taarifa muhimu lakini moderators wa Jamii Forum kwa utashi wao wakipumbavu wakaona waufute.

Sasa leo naleta taarifa rasmi kutoka Tanesco kuhusiana na nilicholeta jana na naomba ndugu zangu muwaambie hawa mods wa JF waurudishe uzi ule nilioleta jana haraka sana na ikiwezekana kuunganisha na huu. Asanteni

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake wote wanao tumia mita za malipo ya kabla yaani (LUKU) kuwa, kuanzia April 2, 2018 TANESCO itahamia rasmi katika mfumo wa malipo wa Serikali ujulikanao kama Government e-Payment Gateway (GePG) kama matakwa ya sheria kwa Taasisi za Serikali.

TANESCO ikiwa miongoni mwa Taasisi za Serikali, itaanza kutumia mfumo huu kwa kufanya mauzo ya LUKU kupitia ofisi za TANESCO, Kampuni za simu pamoja na Benki zote zinazofanya mauzo ya LUKU kupitia huduma za kibenki.

Serikali kwa kushirikiana na Wataalamu wa TANESCO itahakikisha kuwa mfumo huu unafanya kazi bila kuathiri manunuzi ya LUKU. Ifahamike kwamba, TANESCO ni miongoni mwa Taasisi za Serikali zitakazotumia mfumo huu mpya na hadi hivi sasa Taasisi nyingine za Serikali zimeshaanza kutumia kwa mafanikio, baadhi ya Taasisi hizo ni Polisi, Brella, Ardhi, TRA pamoja na Mamlaka za maji.

TANESCO inapenda kuwahakikishia wateja wote kuwa mbali na Kampuni za simu ofisi zote za Shirika na vituo vya mauzo ya LUKU vitaendelea kutoa huduma katika kipindi chote cha Sikukuu ya Pasaka.

TANESCO ‘‘Tunayaangaza Maisha yako’’

Kwa mawasiliano

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz, mitandao ya kijamii:

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook Tanesco Yetu

IMETOLEWA NA:

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

MACHI 27, 2018
 
Back
Top Bottom