TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;


LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO
Tanesco naomba kufaham ikiwa nimekosea kununua umeme nikaweka naomba ya mita tofauti lakini umeme nikapata je naweza kuweka kwenye mita yangu ukafanya kazi??
 
Tanesco naomba kufaham ikiwa nimekosea kununua umeme nikaweka naomba ya mita tofauti lakini umeme nikapata je naweza kuweka kwenye mita yangu ukafanya kazi??

asante,
huwezi kuweka umeme ambao sio wa mita yako na kuingia.
 
asante,
huwezi kuweka umeme ambao sio wa mita yako na kuingia.
Naomba kujua baada ya kukosea katika kuingiza namba ya mita wakati wa manunuzi kama nimenunua LUKU kupitia mtandao wa simu nasaidiwa vipi...
 
Naomba kujua baada ya kukosea katika kuingiza namba ya mita wakati wa manunuzi kama nimenunua LUKU kupitia mtandao wa simu nasaidiwa vipi...
Shilingi ngapi na mita namba ya uliokosea ili tuweze kujua mita ipo wapi. Kama tutapata namba ya simu ya mteja uliokosea namba yake baada ya kuiona kwenye system zetu tutawasiliana nae kama atakuwa tayari kulipia hicho kiasi ili akufidie wewe au kufanya utaratibu mwingine
 
Eneo lenu la kazi kimamlaka ni lipi? Maana mnachagua maeneo ya kutoa Maelezo.
Kama mko kwa majibu ya Tanzania nzima naombeni JIBU.
 
Eneo lenu la kazi kimamlaka ni lipi? Maana mnachagua maeneo ya kutoa Maelezo.
Kama mko kwa majibu ya Tanzania nzima naombeni JIBU.
Nchi nzima

MFUMO WA KUTUPATIA TAARIFA/LALAMIKO

1.JINA.....................................

2.SIMU....................................

3.MKOA...................................

4.WILAYA................................

5.MTAA/KIJIJI/KATA.........

6.JINSI YA KUFIKA................

7.KITU/ALAMA/MTU MAARUFU.............................

8.NAMBA YA MITA................

9.TATIZO LAKO.....................


"TANESCO TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO"
 
Nchi nzima

MFUMO WA KUTUPATIA TAARIFA/LALAMIKO

1.JINA.....................................

2.SIMU....................................

3.MKOA...................................

4.WILAYA................................

5.MTAA/KIJIJI/KATA.........

6.JINSI YA KUFIKA................

7.KITU/ALAMA/MTU MAARUFU.............................

8.NAMBA YA MITA................

9.TATIZO LAKO.....................


"TANESCO TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO"
Mfumo huu sins tatizo nao na ni bora kabisa. Tatizo langu.

Mimi naishi kitongoji cha MKOKOZI wilaya ya Mkuranga tumepakana na wilaya ya Temeke. Kuna nyumba ziko upande wa MKOKOZI kiramani lkn zimewekewa umeme toka Temeke sasa kwann eneo lots lisihudumiwe na Temeke ili kurahisisha Huduma kwa Wananchi?

Kuna gharama zingine uko uwezekano wakazi tukihamasishwa tukajitolea kwa hali na mali
 
Mfumo huu sins tatizo nao na ni bora kabisa. Tatizo langu.
Mimi naishi kitongoji cha MKOKOZI wilaya ya Mkuranga tumepakana na wilaya ya Temeke. Kuna nyumba ziko upande wa MKOKOZI kiramani lkn zimewekewa umeme toka Temeke sasa kwann eneo lots lisihudumiwe na Temeke ili kurahisisha Huduma kwa Wananchi?
Kuna gharama zingine uko uwezekano wakazi tukihamasishwa tukajitolea kwa hali na mali
Tunaweza kupata namba ya mawasiliano yako
 
Habari TANESCO ... Umeme Kigamboni umekua kero kwa miezi ya hivi karibuni. Umeme unakatika muda mrefu sana na pia ukirudi unacheza cheza au unakua mdogo then unakatika tena.

Sikumbuki siku ambayo nimekaa na umeme bila kukatwa kwa siku nzima katika miezi ya April, May na June...
 
Tanesco Iringa> Sisi wakazi wa kijiji cha Igingilanyi tunaomba Tanesco itusaidie kupata umeme baadhi ya maeneo wale wakandalasi walipokuwa wanasambaza hawakusambaza kote mfano upande wa juu kutokea mjini na baada ya kambi ya wachina hawakusamabaza nguzo wakati baadhi tulishafanya wiring na matokeo yake hatujafungiwa hadi leo.

Tunaomba jibu ni lini tunafungiwa kwani umeme. Asante
 
naomba msaada mtupatie umeme,sisi wakazi Wa kata ya Itende mbeya mjini,nyuma ya jeshi la Jkt-itende!

Nguzo zimesambazwa mtaa mmoja tu Wa kata hiyo!mitaa mingine nguzo hazijasambazwa kwenye makaz ya watu bali zmepita kando ya barabara kuu ya kata as if wananch wote tunaishi along the road!

Tunaomba msaada wenu,tumejikussanya tumefika wananchi 102,tunaohitaji nguzo ili tufungiwe umeme!

kata IPO km 3 from mbeya city center ukipita jkt-itende
 
naomba msaada mtupatie umeme,sisi wakazi Wa kata ya Itende mbeya mjini,nyuma ya jeshi la Jkt-itende!

Nguzo zimesambazwa mtaa mmoja tu Wa kata hiyo!mitaa mingine nguzo hazijasambazwa kwenye makaz ya watu bali zmepita kando ya barabara kuu ya kata as if wananch wote tunaishi along the road!

Tunaomba msaada wenu,tumejikussanya tumefika wananchi 102,tunaohitaji nguzo ili tufungiwe umeme!

kata IPO km 3 from mbeya city center ukipita jkt-itende
Tumeipokea mpendwa mteja
 
Aisee mi mwezi uliopita nimekuta tanesco wamepitisha Umeme kwenye kiwanja changu katikati eti kwa sababu kuna mama Fulani pale mtaani alikua ana hitaji Umeme yani nilishangaa hawa tanesco sana nimesha peleka malalamiko yangu lakini huu ni mwezi wa 2 sasa sijasaidiwa na nahitaji kujenga kwenye kiwanja changu
 
TANESCO IRINGA jamani naombeni jibu kijijini Igingilanyi ni lini mtasambaza nguzo za umeme kote maana tulidanganywa tutandaze nyaya majumbani matokeo yake wasambazaji wakasambaza sehemu chache wengine tukakosa tunaona miaka inaenda tumebaki na nyaya majumbani sasa hatuelewi kwanini tulitumia pesa zetu kwa kitu ambacho hakina maana?

Maana tunaona miaka inaenda tu wenzetu wachache waliofungiwa wakifaidi maisha ya mwanga wa umeme sisi wengine tukibaki na vibatari. Tulipofuatilia mlisema mkandalasi aliyepaswa kusambaza nguzo hakumaliza. Sasa kama yule hakusambaza kote ndio sisi tuendelee kukaa gizani hadi lini wakati yeye kaishia na mlishamlipa.

Sisi tunachotaka ni umeme hayo mengine mtajuana huko huko ofisini kama mlivyopeana kazi. Jamani tuleteeni umeme manavyokuwa na wateja wengi ndivyo mnavyopata pesa zaidi labda mtwambie umeme umekwisha!
 
Kibaya Nyie Interview zenu ni za kubebana kama mlizozifanya Mtwara Juzi aisee dhahiri na waziwazi bora msingeita wengine mngesema tu mnawaweka watu wenu wa mikataba kazini.

Sio mnaitwa watu wanachoma nauli zao alafu mnachokifanya ni dhuluma ya wazi wazi.


Nawashauri wakati mwingine msiwaite watu wala msitangaze hata hizo nafasi waajiri hao mliowaweka kwa mikataba sio kuwachosha vijana wa masikini kwa dhuluma zenu.

Na kumbukeni Mungu yupo na anawaona ipo ck yenu
 
Asante sana kwa uzi huu,kuna shida sana ya wizi wa mita za LUKU unaofanywa na vishoka cha kushangaza hizi mita hufungiwa wateja wengine hii inamaanisha kuna baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco wanashiriki hushiriki ndio maana huingizwa kwenye mfumo na kuendelea kutumika je Tanesco mnatueleza nini kwenye hili?

kwa nini mita iliyoibiwa ikinunuliwa umeme mhusika asikamatwe either kwa details zilizotumika kununulia umeme?
 
Asante sana kwa uzi huu,kuna shida sana ya wizi wa mita za LUKU unaofanywa na vishoka cha kushangaza hizi mita hufungiwa wateja wengine hii inamaanisha kuna baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco wanashiriki hushiriki ndio maana huingizwa kwenye mfumo na kuendelea kutumika je Tanesco mnatueleza nini kwenye hili?kwa nini mita iliyoibiwa ikinunuliwa umeme mhusika asikamatwe either kwa details zilizotumika kununulia umeme?

Asante ndugu mteja, katika kupambana n hili tanesco tunawahimiza kila siku kuwa watejanwetu wafike wao wenyewe ofisi zetu na kupata huduma ndani ya ofisi bili kutumia mtu wa kati na malipo yote ya shirikamhutolewa na risiti ya tanesco ikionyesha kiasi alicholipia chote bila upungufu.

Pia tunawahimiza sana kutojihusisha sana wizi wa umeme au miundo mbinu ya shirika kwani hatua kali dhiti yao zitachukuliwa ikigundulika,

Pamoj na hilo tunawaomba sana kutoa taarifa za wizi wa umeme katika ofisi ya tanesco iliopo karibu nayo au kwa namba ya simu 0768985100 ambapo taarifa yako itapokelewa kwa usiri mkubwa sana au unaweza kutumia ukarasa huu kutumanujumbe kwenye meseji au inbox na sisi tutaanza kuifanyia kazi mara moja


TANESCO
 
Back
Top Bottom