Mimi kero yangu ni hiii umeme unakatika sana huku ukerewe nansio ,watu tunaka siku 3 bila umeme..maeneo ya kakukuru na viunga vyake.. Jamani hii inakera sana
Tunaomba namba yako ya simu na je hauna umeme leo?
 
Tanesco, kuna nini Gongolamboto? Kwa nini kila siku mnakata umeme kwa Massa zaidi ya 8? Kwa nini mnakata umeme Masaa ambayo watu wanafanya shughuli za kiuchumi?
Tulitoa ratiba ya mwezi mzima kwani kuna ujenzi wa laini mpya eneo husika
 
Bado muda hajafika siku 30. Siku 30 za kazi yaani unatoa jumapili na jumamosi
Wewe unaridhika kwa utaratibu huo? Viwanda vitakwenda kweli kwa mfumo huo mbovu?Nashauri kama hamuwezi kufunga umeme ndani ya siku saba tangu mteja kulipa ni vema msichukue fedha za wateja.Huo ni utapeli na uhuni na kufanyakazi kizamani na kwa ukiritimba.Inasikitisha sana!!!!
 
Tafadhali pitia mkataba wa huduma kwa wateja kuona muda sahihi wa kufungiwa umeme.upo www.tanesco.co.tz
 
Salaam, narudi tena kwa Mara ya tatu hapa. Mm ni mkaazi Wa eneo la mradi Mkokozi wilayani Mkuranga.

25/7/2018 nililipia mita 2, lkn walipokuja kufunga wakaniletea mita 1, kwa Maelezo kuwa kuna makosa yamefanyika nifuatilie MKURANGA TANESCO.

Nimefanya hivyo ,na kupewa no ya simu kwa mawasiliano. Lkn kila nikipiga no hiyo Maelezo huwa hayohayo ' TUNASHUGHULIKIA' baya zaidi kila inapopokelewa inakuwa unaulizwa kama unaanza upya.

Mliniomba no ya simu nikawapa lkn mko kimyaa niliamini humu ningepata jibu ambalo hata kama utekelezaji ungefanyika 2019 NINGERIDHIKA sababu nimepata jibu.

Maana TUNASHUGHULIKIA sio jibu. Inatakiwa liwe na deadline 0789443736
 
Tafadhali pitia mkataba wa huduma kwa wateja kuona muda sahihi wa kufungiwa umeme.upo www.tanesco.co.tz
Utaratibu wa mkataba huo mbovu upitiwe upya na kurekebishwa ili uendane na kasi ya awamu ya tano.Au mpaka mletewe wanajeshi kuja kurekebisha mikataba hiyo iliyopitwa na wakati? Mitambo ya kidato mlikuwa hamnunui na kutunza vipuri vya matengenezo ya mitambo husika hadi waziri wa nishati kuwasimamia kwa karibu na ndipo mmeweza kutekeleza hilo.Mambo ya siku 30 sijui 60 hayana nafasi katika awamu hii,badilikeni kabla hamjabadilishwa.
 
Najua mlishatoa ratiba ya kukata na kurudisha umeme kwenye baadhi ya maeneo ya tabata na gongo LA mbota,tatizo ni kwamba hiyo latiba imeshaisha muda wake ila kwa bahati mbaya nyinyi bado nmakati umeme tatizo ni nini mipango yetu inakwama big time wakuu..twambieni kwa uhakika mwisho Wa katakata hii ni lini?
 
*TUNAKUMBUSHA TUNAKUMBUSHA*

*SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)*

*TAARIFA YA MABORESHO YA MIUNDOMBINU YA UMEME*

Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa mkoa wa ilala kuwa, kutakuwa na kazi ya maboresho ya miundombinu ya umeme ili kuendana na ongezeko la matumizi ya umeme, ili kupisha maboresho hayo umeme utazimwa kama ifuatavyo;

*Muda:* 01:30 asubuhi mpaka 12:00 jioni
*Tarehe:*

*Novemba- 13, 14, 20 na 21/11/2018*

SABABU: *Kuvuta waya wa umeme wa msongo wa kilovolti 132 kutoka kituo cha ubungo mpaka kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Kipawa*

*MAENEO YATAKAYOATHIRIKA NI;*
Gongo la mboto yote, namera group of industries, Kampala university, Mombasa, Mazizini, Moshi bar, ukonga yote, kitunda yote, kivule yote, Msongola yote, Mongola, Ulongoni yote, stakishari, Said Mwema, Gongo zembe, Kisarawe yote, Majohe, FQ hotel, na maeneo jirani.

Tafadhari usisogelee, usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka, toa taarifa kwenye Dawati la dharura mkoa wa ILALA: 0784768586,0715768586,022-2133330,Viwandani 0684001066,0715768587 ,Tabata 0684001068 0715768589 , Gongo la Mboto- 0688001071, 0715 768 584
au kituo cha miito ya simu makao makuu:+255768985100

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

*Imetolewa na:* Ofisi ya uhusiano na huduma kwa wateja.
TANESCO- ILALA
 
Ndugu mteja pole kwa usumbufu unaopata..tunaweza kupata namba yako ya simu na wilaya yako pamoja na eneo lako kwa hatua zaidi.

Po
Okay nipo wilaya ya Tarime mji wa Nyamongo na namba yangu ya simu ni 0755-922096.
 
Tumepokea taarifa mpendwa mteja
Okay ntashukuru sana maana siku ya nne saivi hatuna umeme kisa mita ndogo ikiingizwa units hazisomi hadi fundi wa tanesco anatuambia imeshaharibika kwamba anayo nyingine anauza elfu 50.
 
Okay ntashukuru sana maana siku ya nne saivi hatuna umeme kisa mita ndogo ikiingizwa units hazisomi hadi fundi wa tanesco anatuambia imeshaharibika kwamba anayo nyingine anauza elfu 50.


Usikubali kutoa hio hela kwa sababu kubadilisha mita ni kazi ya shirika na ni bureee!!
 
Huu mgao wenu dar unaisha lini? Mbona unaendelea tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…