TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

IMG_wsbfxd.jpeg
IMG_-e0gmyi.jpeg
IMG_-xoimji.jpeg
IMG-20181118-WA0025.jpeg
 
TANESCO kwa nini mteja akihitaji huduma ya kuunganishwa umeme sehemu ambayo hakuna transformer mnamtaka anunue kwa gharama zake na kisha kuwa mali ya Tanesco na kuunganisha wateja wengine?

Easy...kusanya risiti zako zote , pata wakili mzuri asiyependa rushwa then naamini utalipwa vizuri tu
 
TANESCO kwa nini mteja akihitaji huduma ya kuunganishwa umeme sehemu ambayo hakuna transformer mnamtaka anunue kwa gharama zake na kisha kuwa mali ya Tanesco na kuunganisha wateja wengine?
Ndugu mpendwa wetu mteja hawezi kulazimishwa kununua transfoma bali kwa hiyari yake maeneo ambayo bado hakuna transfoma au ana uhitaji wa haraka anaweza kuchangia kwa kujiwekea.transfoma inatumiwa na wateja wengine wa eneo hilo poa na hata ikiharibika sisi tunabadili bila kumchagi mteja tena.itakumbukwa kuwa kina transfoma inauwezo fulani hivyo hatuwezi kumuunga mteja mwingine kama imefikia uwezo wa mwisho.
 
Easy...kusanya risiti zako zote , pata wakili mzuri asiyependa rushwa then naamini utalipwa vizuri tu
Hatujiandae kushindana na wateja wetu bali kuwasikiliza na kila kitu kina taratibu hili ni shirika la uma hivyo zipo taratibu zilizowazi kwa swala hili
 
Wastani wa matumizi yako ni unit 78 kwa mwezi upo kindi la t1 matumizi ya nyumbani
Nimepata muda mzuri wa kuweka data zangu hapa, nimefungiwa umeme tokea tarehe 5/9/2015 unit ambazo nishatumia ni 1610 hadi sasa. Kwa hiyo Jumla ya miezi ambapo nishatumia umeme itakua miezi 38 hivyo basi miezi tajwa na units zilizotumika hadi sasa ni wastani wa unit 42.36 kwa mwezi hiyo calculation yenu ambayo imewapa unit 78 nakushauri tu ni afadhali usingeandika ukakaa kimya. Hii itajenga dhana ya kuwa huduma zenu za kutatua matatizo mnavutia upande wenu kuridhisha watumiaji kwa majibu mepesi mepesi. Nawasilisha rudieni mahesabu yenu.


Hili limekosa jibu??
 
Upo eneo gani haswa na namba yako ya simu mpendwa mteja
Niko eneo la MKUZO SONGEA MJINI....Tatizo la umeme ni kukatika katika bila utaratibu maalumu....Mngeweka utaratibu mzuri kama kuna tatizo linashuhulikiwa..Ila umeme unakatika mpaka keroo..unakaa dakika 10 unardi..then unakatiaka...
 
Niko eneo la MKUZO SONGEA MJINI....Tatizo la umeme ni kukatika katika bila utaratibu maalumu....Mngeweka utaratibu mzuri kama kuna tatizo linashuhulikiwa..Ila umeme unakatika mpaka keroo..unakaa dakika 10 unardi..then unakatiaka...
Namba yako ya simu tafadhali
 
Tanesco kama na kesho mtakata umeme umtupe taarifa mapema . manake mlisema mwisho wa kukata ni tareh 7/11 ila tarehe 13 na 14 mlitukatia tena wakazi wa mikoa ya temeke n ukonga.

Mseme mapema ili tuchome mafuta asubuhi kabisa tukwepe foleni ili tutafute umeme sehem zingine
 
Kwa kuwa kesho ni maulidi hawata kata umeme mkuu, ikitokea wamekata kusanya nguo zako uwapelekee Ofisini kwao wakakunyooshee.😀😀😀😀
 
Huu ni utapeli. Tena nguzo zenyewe wanaweka barabarani. Barabara ikiwa inafanyiwa ujenzi tunapata adha ya kukosa umeme
Mteja halipi nguzo bali anachangia gharama ya nguzo.nguzo.hiyo inabaki kuwa ya uma kupitia TANESCO ili kuruhusu wateja wengine kufungiwaul umeme na hata ukarabati iliharibika ndio maana hakuna mteja aliyewahi kulipishwa nguzo ikioza au kuanguka.jiulize kama kila aliyelipia nguzo ingekuwa yake akigoma wengine wasifungiwe kwa nguzo hiyo tunafanyaje hapo.
 
Back
Top Bottom