Namba uliweka haipokelewiJINA: KIVUYO
ENEO: KIJIJI CHA USUNYAI KARIBU NA JANE WILLY GARDEN
SIMU: 0657-258818
TATIZO: BILL YANGU HAIENDANI NA ENEO NILIPO WENZANGU WOTE (MAJIRANI) WAMEFUNGIWA UMEME WA REA.NIPO ARUSHA DC LAKIN KWENYE BILL MNASEMA NIPO ARUSHA MJINI.
Je eneo ganiWatumishi poleni na kazi, hongereni na kazi pia.
Nina tatizo linanikabili nyumbani kwangu ambalo limekuwa likijirudia rudia. Usiku wa kuamkia jana Jumatano tarehe 16 Septemba 2020 umeme ulikatika na uliporudi, asubuhi yake nikakuta Microwave yangu haiwezi kuchemsha chochote, inaunguruma tu. Si mara ya kwanza kukumbana na tatizo la namna hii, kuna kipindi tena liliwahi kutokea na niliripoti na hatimaye nikapata msaada uliohitajika kutoka kwenu. Tatizo lenyewe liko kitaalamu kidogo kwamba unakuta Jiko lina umeme wa kutosha, na vitu vingine vyote vinafanya kazi, lakini kitu kidogo tu tuseme kama mashine ya kunyolea nywele inakuwa haiwezi kufanya kazi. Kwa safari hii vitu vyote viko kawaida vinafanya kazi, isipokuwa Microwave tu ndiyo haipati umeme wa kutosha. Naomba nisisitize kuwa tatizo la namna hii si mara ya kwanza kujitokeza, na uhakika ni kuwa Microwave ni nzima na haina tatizo lolote. Hata hivyo jana usiku nilibahatika kuongea na wahusika na wakasema wanakuja kulishughulikia leo. Ombi langu hapa sasa ni kuwa naomba walishughulikie kwa ujumla ili lisiwe linajirudia rudia. Pia naomba kuwajluisha kuwa maisha yangu yanategemea Microwave kwa zaidi asilimia 97, na hivyo inapokuwa haifanyi kazi, maisha yanakuwa hayaendi kabisa. Nazidi kusisitiza kuwa Microwave ni nzima, tatizo ni umeme. Nimekaa kwenye nyumba hiyo kwa zaidi ya miaka 16, sasa na haina tatizo lolote la umeme. Ni nyumba ya umma.
MUBARIKIWE TENA NA BWANA
KuJe eneo gani
Wilaya
Simu
Namba ya taarifa
Kuna watu tayari wameshanipigia simu wapo site wameshafika. details niliwapatia jana ila eneo ni getini UDSM mkabala na Ardhi University. Kuna maghorofa yako kushoto mwa barabara na kuna Transfoma pembezoni mwa barabara. Ubarikiwe sana kwa kujali!Je eneo gani
Wilaya
Simu
Namba ya taarifa
Karibu sanaKu
Kuna watu tayari wameshanipigia simu wapo site wameshafika. details niliwapatia jana ila eneo ni getini UDSM mkabala na Ardhi University. Kuna maghorofa yako kushoto mwa barabara na kuna Transfoma pembezoni mwa barabara. Ubarikiwe sana kwa kujali!
Tunaomba namba ya mita
Tafadhali onyeshaKuna nyumba imedondokewa na nguzo yenu na inatoa cheche muda wote, nawapigia magomeni wanasema wapo mbali hawawezi kuja sasa hivi. Eneo ni mabibo Azimio (luhanga) mbele ya shule ya kawawa nyuma ya Bar inaitwa small world View attachment 1572380View attachment 1572381View attachment 1572382View attachment 1572383
Nimepita hapo sio midaNjoo hapa kwetu pazuri
Habari za kazi? Samahani kumbe niliwalisha maneno. Walinipigia mimi nikadhani kuwa tayari wako site, kumbe hapana. Vile vile hawakuniambia kama walikuwa site, wainipigia tu kuulizia details za tatizo.Karibu sana
Tafadhali onyesha namba ya simu na wilaya husikaHabari Tanesco,
Ni mwaka umepita tangu muweke nguzo na nyaya eneo la Saccos--Mabwepande,tukifatilia kutaka kuwekewa umeme tunaambiwa mradi bado haujakamilika,umeme unatoka kinondo wameweka nguzo za kuweka transformer ambalo ndio lita supply wakazi wa saccos ni miezi mitatu imepita tangu waziweke hizo nguzo na chuma za kuweka transformer.
Tunaomba kujua ni kitu gani kinachelewesha kutuletea hilo transformer? Mnaweka nguzo mwaka mzima zinakaa tu maana yake nini?
Kama mmeshindwa ni bora mtuambie wananchi tujichange tununue transformer letu tuwakabidhi ili mliweke.