Watumishi poleni na kazi, hongereni na kazi pia.
Nina tatizo linanikabili nyumbani kwangu ambalo limekuwa likijirudia rudia. Usiku wa kuamkia jana Jumatano tarehe 16 Septemba 2020 umeme ulikatika na uliporudi, asubuhi yake nikakuta Microwave yangu haiwezi kuchemsha chochote, inaunguruma tu. Si mara ya kwanza kukumbana na tatizo la namna hii, kuna kipindi tena liliwahi kutokea na niliripoti na hatimaye nikapata msaada uliohitajika kutoka kwenu. Tatizo lenyewe liko kitaalamu kidogo kwamba unakuta Jiko lina umeme wa kutosha, na vitu vingine vyote vinafanya kazi, lakini kitu kidogo tu tuseme kama mashine ya kunyolea nywele inakuwa haiwezi kufanya kazi. Kwa safari hii vitu vyote viko kawaida vinafanya kazi, isipokuwa Microwave tu ndiyo haipati umeme wa kutosha. Naomba nisisitize kuwa tatizo la namna hii si mara ya kwanza kujitokeza, na uhakika ni kuwa Microwave ni nzima na haina tatizo lolote. Hata hivyo jana usiku nilibahatika kuongea na wahusika na wakasema wanakuja kulishughulikia leo. Ombi langu hapa sasa ni kuwa naomba walishughulikie kwa ujumla ili lisiwe linajirudia rudia. Pia naomba kuwajluisha kuwa maisha yangu yanategemea Microwave kwa zaidi asilimia 97, na hivyo inapokuwa haifanyi kazi, maisha yanakuwa hayaendi kabisa. Nazidi kusisitiza kuwa Microwave ni nzima, tatizo ni umeme. Nimekaa kwenye nyumba hiyo kwa zaidi ya miaka 16, sasa na haina tatizo lolote la umeme. Ni nyumba ya umma.
MUBARIKIWE TENA NA BWANA