Moshi (V)
Mabogini
Kitongoji shabaha na sanya line b hakuna umeme tangia asubhi hadi mda huu saa 3 kasoro usiku.

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Kwanini sisi wateja wa REA tunabaguliwa hususani katika kuunganishiwa umeme, mfano mimi mkazi wa kata ya Lwanhima-- Mwanza nimelipia kuunganishiwa umeme tangu mwezi wa 8 ila mpaka leo ni mwezi wakumi na moja sijaunganishiwa, nikifatilia naambiwa vifaa hamna!
 
Tafadhali onyesha

Jina

Eneo

Wilaya

Simu

Tatizo

Toka lini

Kwa hatua zaidi
 
Tafadhali onyesha

Jina

Eneo

Wilaya

Simu

Tatizo

Toka lini

Kwa hatua zaidi
Natumia Unit chini ya 70 kwanini meter haijibadilish tariff automaticaly?

nahitaji kubadilisha tariff ni kwann ni lazima nifike huko maofisi kwenu?

namba za luku yangu hazitoshi nyie kunibadilishia au ndio mpaka nikajaze

ile form yenu? what if mtu ni mlemavu hawezi tembea au kufika ofisini kwenu?

sometimes mnafanya mambo yawe magumu ili mpige watu hela kwenye umeme...sio!?
 
Reactions: SIM
Mimi Tarakwa (0621149433), mkazi wa wilaya ya Kilindi mkoani Tanga.Tafadhali naomba msaada wa mawasiliano ya manager wa TANESCO wilaya ya Kilindi. Nahitaji huduma ya umeme na nilijaza fomu Tangu mwezi wa sita Hadi Leo sijapata huduma ya umeme. Awali nilikuwa nikiwasiliana na mamlaka ya TANESCO wilaya ya Kilindi kwa namba hii 0718 851 650, ambayo kwa muda mrefu Sasa haipo hewani. Ahsante
 
Ninaitwa Kessy nipo wilaya ya Busega mkoa wa Simiyu jirani kabisa na ofisi yenu ya wilaya. Nimenunua umeme wa Tsh. 8000 kwa njia ya NMB Mkononi. Nimetumiwa token. Nimeshajaribu kuziingiza mara nyingi zinakataa. Remote ya meter inaniandikia "reject" Nimeenda ofisi ya wilaya ya Busega nilipo tatizo linaonekana lipo nje ya uwezo wao. Nimejaribu kununua wa 1000 umekubali. Namba ya meter ni 24213579527. Naomba msaada wenu.
 
Je ulipatiwa maelezo gani?namba ya simu tafadhali
 
Ahsante kwa taarifa tunaifanyia kazi
 
Je ulipatiwa maelezo gani?namba ya simu tafadhali
Maelezo niliyopewa ni kwamba wanafuatili ili niandaliwe token mpya na IT wenu. Hapa kwenye ofisi yenu ya wilaya hawana uwezo huo. Namba yangu 0767151519. Nisaidieni
 
Maelezo niliyopewa ni kwamba wanafuatili ili niandaliwe token mpya na IT wenu. Hapa kwenye ofisi yenu ya wilaya hawana uwezo huo. Namba yangu 0767151519. Nisaidieni
Inafanyiwa kazi
 
Tanesco Mbezi: Hapa mbezi Mshikamano mtaa was Peramiho / Kwa Matembo, Luna Fault INA miezi mitano sasa.
Luna guzo inaelekea mafundi wenu hawalitengenezi vizuri, kwa makusudi ama kwa kutojua.
Kila Mara inaponyesha mvua yenye Upepo mkali nyuma kama kumi zinazozunguka nguzo hiyo zinapata Shot na Umeme kuzima kwenye nyumba zao.
Mbezi mwisho nzima inaweza kuwa na umeme lakini eneo hill lokawa gizani.
Mafundi wenu wanapokuja wanafunga funga na kukaza nyaya na wakazi wanapata Umeme.
Lakini inapotokea mvua yenye upepo ikanyesha Sikh hiyo hiyo, tatizo linajirudia!
Leo tar 11/11/2020 SAA Tano Kamili niuandikapo ujumbe huu eneo hill lipo gizani toka Jana usiku iliponyesha mvua ndogo tu iliyoandamana na Upepo Umeme kukatika SAA 11 Alfajiri, had I sasa!
Tufanyeje, ili tatizo hili lipatiwe Ufumbuzi?
 
Mimi mbona nikiweka umeme unawahi kuisha na sina Taa za ndani Tatizo ni lipi?
 
Tafadhali onyesha namba ya simu kwa hatua zaidi
 
Je ulipatiwa maelezo gani?namba ya simu tafadhali
Nina tatizo sasa ni zaidi ya miezi miwili tangu nimeliripoti. Reference namba yangu ni 2171. Umeme umepungua nguvu na siwezi kutumia micro-wave oven. Siyo mara ya kwanza tatizo hili kutokea, na huwa linatokea pale tu umeme unapokatioka. Ninaishi kwa maisha ya microwave oven zaidi ya miaka 10 sasa. Kila nikipiga simu naambiwa kuna watu watakuja walishughulikie, halafu hawaji. Hatimaye nimeamua kukaa kimya.
 
Tafadhali onyesha

Jina

Eneo

Wilaya

Simu

Tatizo

Toka lini

Kwa hatua zaidi
 
Tanesco Tanesco kunani hukooo!!! Naomba niwekewe umeme vijamaa vinajifanya kuniwia vikali,vibane ofsini eti anajifanya hataki kuongea politely na mteja kwa kushukiwa anawaka kutokiwa humble asistukiwe...mwizi mwizi tu
Tafadhali onyesha

Jina

Eneo

Wilaya

Simu

Tatizo

Umelipia lini

Kwa hatua zaidi
 
Hodi TANESCO.
Nawashauri kusambaza umeme kwa wananchi wa Robanda SERENGETI pia na siyo kuupeleka kwenye kambi za watalii peke yake.
Hivi hamjaelewa JPM anawapenda wanyonge hao?
Kuelekeza nguzo mbugani kwenye kambi ya Ikoma bush camp, KEMANG'ORE, Mapito Camp na kuviacha vitongoji line za umeme zilikopita siyo sahihi.
Hiyo ni hujuma na wananchi wameomba mara nyingi sana kwenu.

Sent from my LG-F800S using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…