TANESCO ANZENI KUKOPESHA LUKU

HAKUNA ATAKAE KIMBIA NYUMBA YAKE KWA LUKU YA ELFU KUMI

USUMBUFU ULIOJITOKEZA JUZI HII INGESAIDIA KUPUNGUZA TATIZO
 
Ahsante kwa taarifa tunaifanyia kazi.Jm
TANESCO ulisema unafanyia kazi suala la kukatika umeme maeneo ya Kimara mwisho.
Nakutaarifu tu juzi umeme ulikatwa jioni hadi usiku.

Jana ulikatika tena usiku.Na leo hivi ninavyokiandikia asubuhi hiii hamna umeme Kimara mwisho yote.
Ahsanteni sana.
 
Sasa ni saa saba mchana.tangu asubuhi shughuli zote za uchumi zinazotumia umeme zimesimama Kimara mwisho kote na si leo tu.
Wewe unayewasiliana nami kila siku humu kwa takribani miaka miwili sasa utakuwa shahidi wangu.
Kimara mwisho panawashinda nini wazee?kwanini hammalizi tatizo hili Kimara?Mimi nitaendelea kuwa kero humu hadi tatizo liishe.hamuwezi kutuonea kiasi hiki.Kila umeme ukikatika ntaripoti hapa na kwingine nnakokujua mimi hadi hili tatizo la Kimara liwe kubwa kwenu kama lilivyo kubwa kwetu wakazi wa Kimara.Hapo nadhani mtashughulika.
Baada ya masaa mawili kama umeme haujarudi nakuja tena kuandika humu maana sina shughuli ya kufanya now acha tuchati na wewe bwana TANESCO

Usiponiona tena ujue umeme umerudi.
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KATIZO LA DHARURA WILAYA YA KIMARA

Wapendwa wateja wetu tunasikitika kuwataarifu kwamba mnakosa huduma ya Umeme kuanzia saa 02:25 Asubuhi hii ya tarehe 21/05/2021

MAENEO YANAYOATHIRIKA
King'ong'o, Matosa, Kimara Baruti, Kimara B, baadhi ya maeneo ya Temboni, Kibanda cha mkaa, Mbezi, Tegeta A, Baadhi ya maeneo ya Goba, Msumi, Makabe, baadhi ya maeneo ya Stop over, Suka na maeneo ya Jirani.

Hii ni hitilafu ya dharura ambayo imejitokeza kwenye njia yetu ya kusafirisha Umeme hivyo wataalamu wetu tayari wanafanya jitihada za haraka kubaini chanzo na kuhakikisha huduma inarudi kwenye hali yake ya kawaida

KWA HUDUMA ZA DHARURA PIGA SIMU:- 0717379696, 0788379696

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano na Huduma kwa wateja
TANESCO- Kimara
21/05/2021
 
Nimelalamika juu ya kuunganishiwa umeme ...nikaombwa namba kwa mawasiliano mpaka leo sijapata mrejesho leo karibu siku ya tano kulikoni au ndio sakata la luku
 
Hivi, mtu aki iba umeme tangia labda tokea 2014 na endapo ikiwa ana matumizi ya kawaida anaweza kua amelipelakea shilika hasara kiasi gani?!
(Ni swali tu mfinifikilie vibaya)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Karibuni sana JF
KUNA TATIZO GANI LA UMEME MBEZI BEACH MAKONDE ENEO LA VIWANDA HAKUNA UMEME TANGU ASUBUHI,NAMNA HII KWELI NCHI
HII TUTAFIKA NA UCHUMI WA VIWANDA?MBWEMBWE NYINGI LAKINI HAMNA LA MAANA ENEO HILI TATIZO LA KATIZO LA UMEME AU LOW
VOLTAGE NI LA KAWAIDA KILA MARA SIUI LITAISHA LINI NA IWE KESHAONDOKA TUTARUDI KULE KULE KWENYE MGAO
 
Hivi, mtu aki iba umeme tangia labda tokea 2014 na endapo ikiwa ana matumizi ya kawaida anaweza kua amelipelakea shilika hasara kiasi gani?!
(Ni swali tu mfinifikilie vibaya)

Sent using Jamii Forums mobile app
Inatagemeana na meneja wa ene na mkadiliaji wa hasara wameamukaje au wana hasara ya sh. Ngapi kwenye eneo lao, ili iwasaidie kuziba mapengo ya upotevu walioufanya. Kifupi tunakujumulishia na vimeo vingine ili unaweza ukawa umetumia unit mia 500 tunakuambia umetumia unit milion zote ili uwe muhujumu uchumi kwelikweli mpaka nchi nzima ijue wewe ndo ulichangia tukachelewa kufika uchumi wakati tunakupeleka mahakamani na eskoti ya magari ya police sita kama kuna sehemu tulipiga hela basi tunakuunganishia humohumo

NB: hii ni kwa nchi ya VENEZUELA sijui kwa TANZANIA msinikoti vibaya

Sent from my MI PLAY using JamiiForums mobile app
 
Issue ipo hizi, unapofungiwa umeme wanakuunganisha moja kwa moja kwenye Matumizi makubwa ya Umeme utatumia hivyo kwa miezi 6.

Baada ya hapo unatakiwa uende kwenye Ofisi ya TANESCO ya kwenu ukawaeleze hili, ukifika pale wataangalia kwenye mifumo yao kama utakidhi watakuhamisha,

***********
Tanesco napenda kuuliza hii kitu ni kweli, kwa nini wananchi hawana taarifa au elimu juu ya hili, wangapi tunaendelea kuumizwa kwenye hili bila ya kujua?

Naongea haya kwakuwa nimefungiwa umeme kama week moja iliyopita, zile unit 9 za mkopo (REA) ziliisha ndani ya siku 4 tu kwangu sina matumizi makubwa, just TV na TAA peke yake,
Nikanunua wa elfu kumi nikapewa units 18 nikaambiwa nimekatwa 3,700 nilizokopeshwa,
Juzi naangalia naona zimebaki unit 8 kumi zimeisha kwa siku chache tu nazo.

Shida ni nini? Naomba ufafanuzi na utatuzi juu ya hili
 
Tatizo wameacha kutujibu sijui Kuna nn au ndo ao waliosimamishwa (Ni mawazo tu)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…