Nimesoma malalamiko mbalimbali ya wateja wa UMEME! mm pia nikapata mstuko na kujaribu kufuatilia! Lkn pia nikasikia majibu yenu juu ya KILICHOITWA - unit za umeme kuisha kwa HARAKA -
Hii hali imetokea hivi karibuni, majibu yenu yalikuwa " hali hiyo inatokea kipindi hiki kwa kuwa wananchi wengi msimu huu wapo MAJUMBANI.
NILINUNUA umeme tarehe 19/12/2023 kwa tsh 20,000/= nikapata unit 51.9 KWH .matumizi ya hapa nyumbani ni
1 - rice cooker
2- pasi ( mara mojamoja jumapili)
3- feni vyumba 2 usiku kucha na mchana .
4- fridge
5- taa za kwenye ukuta ( fensi)
6- Tv
Umeme huu ulidumu siku 8.
Tarehe 27/12/2023 saa 20:32nilinunua tena umeme kwa tsh 20,000/= nikapata unit 42.1KWH
Matumizi yangu yamezidi kidogo kwani nimeongeza FENI jingine hivyo feni ziko 3 zinazokesha.
Fridge nilikuwa nalizima wakati wa mchana sababu ya joto kali lkn hivi sasa linafanya kazi muda WOTE.
Matumizi mengine yamebaki kama kawaida. Leo ni siku ya 10 umeme bado upo.
Tarehe hiyo hiyo 27/12/2023 saa 19:58 nilinunua umeme kwa tsh 20,000/= nikapata unit 56.1 KWH ( huu niliponunua sikuuona nilidhani umeshindikana nimeuona leo kwenye simu)
Kwanini 20 , 000/= unit 51.9 KWH
Kwanini 20 ,000/= unit 56.1 KWH
Iweje 51.9 unit Zitumike siku 8
Halafu 42.1 unit zitumike zaidi ya siku 10
NAWASILISHA