TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Je zoezi LA REA kule chanika nyeburu limefika mwisho?
Naombeni kujulishwa tafadhali
 
Kuna tofauti gan ya kununua umeme kat ys mteja wa tarrif 0 na tarrif 1? Nawezaje uhama kutoka tarrif 1 to tarrif 0?

Ni kigezo gan mnatumia kuwagrade wateja wenu katika tarrifs 2 na 0?

NIPENI MAJIBU NINA HASIRA NA NYIE
 
Phase- means single/ 3phase!, Idadi ya waya zinazokuja kwa mteja. Kama ni mbili hiy ni single phase, kama nne hiyo ni 3phase supply!. Tarrif ni kundi la matumizi ya umeme!.

Ili Tanesco wawe kuuza umeme lazima wawagroup wateja wao kwenye tarif mbalimbali , wana tarif 1 mpaka 6 nafikiri!. Hapo tarif 1. Ni mteja wa kati ya unit 76- 7500kwh. Hawa wana bei yao per unit!, Tarf 4 ni 1-75kwh mtu anayetumia elfu 9 kwa mwezi, . T2 , t3, hao tunaambiwa ni viwanda Au mahotel makubwa!
Nawezaje kuwekwa kweny trf 1 mk 75 units
Maana nikinunua umeme 5000 napata unit 14, nina vyumba 6, TV, pas na radio
 
Naomba mawazo yenu kwa tatizo hili: natumia unit 8 kutwa.

Nina frigdge moja ndogo, taa energy saver kama 5 zinawaka saa 12 a day, tv mbili zinatumika kama saa 5 a day, . Nadhani unit 8 a day huu ni umeme mwingi ninao tumia.

Tatizo linaweza likawa wapi? Nimeleta fundi akacheki wiring akasema iko vizuri.

Ushauri tafadhali.

Asante
Mkuu lete fundi aangalie earthing yako kama haijakaa njema ni shida. Pia waya ulizotumia ni za kiwanda gani kama ni za kichina tegemea lolote, mwisho yawezekana mita ni mbovu so waje wakague mita kwanza.
 
Mkuu lete fundi aangalie earthing yako kama haijakaa njema ni shida. Pia waya ulizotumia ni za kiwanda gani kama ni za kichina tegemea lolote, mwisho yawezekana mita ni mbovu so waje wakague mita kwanza.
ok nitafanya hivyo
 
nishati ya Uhakika na viwango vya juu ni kichocheo muhimu sana ktk maendeleo ya viwanda.

Hivyo basi Tanesco mnao wajibu mkubwa wa kuboresha miundo mbinu ili kuwa na Umeme Wa uhakika na wenye nguvu.
 
Nimepewa karatasi ya kwenda kulipia bank kwa ajili ya kuunganishwa huu mwezi wa tatu sijaenda kulipa( hali ya maisha imekuwa ngumu), je nitapigwa penati?

Sidhani kama kuna penati kama siyo deni mkuu

Ok nashukuru kwa jibu.
Hakuna penalt yoyote hapo mkuu, ila nivizuri kabla ya kwenda kulipia ukarudi tena katika hizo ofisi kwa maelekezo zaidi, unajua mambo yanabadilika kila siku
 
Kuna tofauti gan ya kununua umeme kat ys mteja wa tarrif 0 na tarrif 1? Nawezaje uhama kutoka tarrif 1 to tarrif 0?
Ni kigezo gan mnatumia kuwagrade wateja wenu katika tarrifs 2 na 0?

NIPENI MAJIBU NINA HASIRA NA NYIE
Hakuna tarrif 0 mkuu, kuna Tarrif One, Two, Three na Four

Tarrif one na four ndio za watumiaji wa kawaida (majumbani) hizo nyingine mbili na tatu ni watumiaji wa viwanda na sehemu zenye mitambo mikubwa kiasi.

Tarrif one ni kwawatumiaji wadogo kabisa wa nishati ya umeme na mara nyingi hawa ni watu wa kijijini ambao huwa hawana matumizi makubwa, japo mijini wapo wasio na matumizi makubwa pia.

Hivyo basi, kama hutumii zaido ya unit 75 kwa mwezi unaweza kuhama tarrif one kwenda tarrif four, chakufanya ni kubalance matumizi yako usizidishe units 75 kwa mwezi ndani ya miezi mitatu, automatically system itakudetect na utabadalishiwa tarrif.

Utajuaje kama umehama tarrif? Ukienda kununua umeme kwa wakala itagoma na unatakiwa kufika office ya Tanesco kupata key change (nambari fulani za kuingiza kwenye meter yako) kisha unaweza kuendelea kutumia tarrif four ila unatakiwa ujichunge sana kwakuwa ukizidisha matumizi unapigwa penalt na utanunua kwa bei kubwa kuliko hata wa tarrif one.
 
Hakuna tarrif 0 mkuu, kuna Tarrif One, Two, Three na Four

Tarrif one na four ndio za watumiaji wa kawaida (majumbani) hizo nyingine mbili na tatu ni watumiaji wa viwanda na sehemu zenye mitambo mikubwa kiasi.

Tarrif one ni kwawatumiaji wadogo kabisa wa nishati ya umeme na mara nyingi hawa ni watu wa kijijini ambao huwa hawana matumizi makubwa, japo mijini wapo wasio na matumizi makubwa pia.

Hivyo basi, kama hutumii zaido ya unit 75 kwa mwezi unaweza kuhama tarrif one kwenda tarrif four, chakufanya ni kubalance matumizi yako usizidishe units 75 kwa mwezi ndani ya miezi mitatu, automatically system itakudetect na utabadalishiwa tarrif.

Utajuaje kama umehama tarrif? Ukienda kununua umeme kwa wakala itagoma na unatakiwa kufika office ya Tanesco kupata key change (nambari fulani za kuingiza kwenye meter yako) kisha unaweza kuendelea kutumia tarrif four ila unatakiwa ujichunge sana kwakuwa ukizidisha matumizi unapigwa penalt na utanunua kwa bei kubwa kuliko hata wa tarrif one.
Thanks!

Mkuu kwa wateja waliobadilishiwa mita za zamani inakuaje unapotaka kununua umeme kwa mara ya kwanza, wana charge kiasi gani mkuu
 
Thanks!

Mkuu kwa wateja waliobadilishiwa mita za zamani inakuaje unapotaka kununua umeme kwa mara ya kwanza, wana charge kiasi gani mkuu
Kubadilishiwa meter kivipi?

Kuna kubadilishiwa meter kutoka zile za kusoma bill kwenda za LUKU na kuna kubadilishiwa meter za LUKU kama uliyokuwa nayo imepata hitilafu.

Labda ungeeleza nijue situation.
 
Kubadilishiwa meter kivipi?

Kuna kubadilishiwa meter kutoka zile za kusoma bill kwenda za LUKU na kuna kubadilishiwa meter za LUKU kama uliyokuwa nayo imepata hitilafu.

Labda ungeeleza nijue situation.
Kutoka zile za kusoma bill kwenda LUKU mkuu! Asante
 
Jamani Tanesco mbona mnakera sana,Kwasie ambao tuna majengo huku maeneo ya Ilala ambao bili zetu zinaletwaga lakini matokeo yake mpaka leo tarehe 10 mwezi wa 5 bili zetu za mwezi wa 4 bado, kwanini jamani mnatufanyia ivyo hilihali waziri wa nishati alituaminisha yakuwa sasa tanesco ina mitambo ya kisasa ya usomaji wa bili za umeme, nitashangaa sana pindi nitakaposikia mapato yenu yameshuka ilihali hampo kibiashara.

Naombeni tanesco Ilala mbadilike jamani
 
Nimelipia nguzo toka mwezi wa 12 / 2016 hapa Sengerema - mwanza lkn mpaka leo hii hatujafungiwa nguzo eti nguzo zimeisha!!! Mara nyaya Hakuna!!! Je kwa namna hii kweli tutafika?
 
Jangwani feeder inayolisha kituo kipya cha Jangwani ilitoka saa 5 usiku, baada ya patrol tumekuta maeneo ya green acres nguzo ya chuma imegongwa na kupinda na waya kuchomoka na kujivingirisha.

Maeneo yanayokosa umeme ni Hoteli zote zilizopo upande wa packers, Kilongawima, baadhi ya maeneo ya Mbezi ya chini na Africana.Jitihada zinafanyika umeme urudi kwa haraka.
 
Kutoka zile za kusoma bill kwenda LUKU mkuu! Asante
Hizo unaandika barua Tanesco kuomba kubadilishiwa kutoka conventional meter kwenda kwenye meter ya LUKU.

Hii haina gharama, ila tu kama meter ina deni litahamishiwa kwenye meter yako ya LUKU hivyo kila utakapo nunua umeme utakuwa unakatwa percent kadhaa mpaka deni litakapoisha.
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;


LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO
Mimi nipo Tanga jiji maeneo ya Makorora tatizo langu hii ni Mara ya pili sasa nikiingiza umeme unaingia na kwny remote inaandika good na nikiangalia salio inaonyesha umeme umeingia lakini hauwaki nilijaribu kuwaambia Mara ya kwanza wakasema mita imejilock wakanitumia namba za kuanlock mita na umeme ukawaka, sasa naona imekuwa ni Tabia ya hizi mita kwani hamuwezi kuondoa moja kwa moja tatizo hili maana likitokea najua tuu nitalala kiza siku Tatu au mbili ukiwapigia simu wanasema wanashughulikia
 
Mpendwa Raisi Magufuli.....Tunakuomba kwa heshma na taadhima sisi wananchi wako tuliokuchagua kwa hiyari yetu.....
Tuondolee hili LITANESCO hapa nchini¥^¥

Kwa maana tangu nizaliwe sijawahi kuona Watanzania wakitokwa
na ule ushamba wa kuushangilia umeme SAA 2 YA USIKU
{ everyday } I HATE YOU TNC
 
Back
Top Bottom