TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Rimoti ya kujazia umeme ya mita Namba hii 24214235368, imealibika. Siwezi kujaza umeme, je kunanjia ingine ya kuingiza umeme bila Rimoti?
 
Ujumbe namba ngapi mpendwa mteja

Nimelipia nguzo moja kuanzia 8/02/2018 nikaambiwa ndani ya siku 60 nitakuwa na umeme, nikavaa vazi la uvumilivu. Siku 60 zimeisha nimerejea wilaya ya Tegeta naambiwa hakuna nguzo.
Swali dogo lisilohitaji elimu ya shule "ni kitu gani kinachofanya Tanesco mnashindwa kutoa huduma kwa wakati ilihali huduma yenyewe imeshalipiwa?? Au haya malipo tunayofanya kuna biashara nje ya umeme yanafanya ikishaleta faida ndipo tunafungiwa umeme?
Halafu ni kitu gani kinafanya vifaa/nguzo kuchelewa zaidi ya siku 60 wakati pesa zimeshalipwa?
Au je hakuna supplier ambaye ni reliable katika kuwaletea nguzo??
Serikali inakosa mapato kwa kutokutuungia umeme ambao tungelipia na kuwaongezea mapato.
 
Unapoteza mdawako kuwaeleza hawa viziwi wataaram wakuomba namba za simu.hawana msaada hata kidogo kama vp vumilia,ikishindikana potezea.
 
Unapoteza mdawako kuwaeleza hawa viziwi wataaram wakuomba namba za simu.hawana msaada hata kidogo kama vp vumilia,ikishindikana potezea.
Yaaani waziri anasema hv na huyu Tanesco anasema hv hawa wakutandika bakora ofisini kwao hapo ,,haiwezekani mtu katoa pesa ya nguzo afu anapewa siku 60 ina maana siku 60 hazitoshi kwa nguzo kupatikana???

Basi Tanesco kama hazitoshi hzo siku 60 basi ongezeni hata siku 30 ziwe jumla siku 90.
 
Ndugu,nimda toka tutoe Malalamiko yetu kupitia jukwaa hili, kuhusu huduma hafifu na ukosefu wa Mita za Njia Tatu, Maarufu Meter za Three phase Mkoa wa Geita na Wilaya zake, tunaomba VIONGOZI na Wahusika Mtusaidie jamani mwezi watatu huu Watu tumelipia Umeme, hutujaunganishiwa isitoshe hatuhitaji nguzo, kila tukiuliza tunaambiwa Mita zimeagizwa ulaya zikifika tutafungiwa, Sasa sisi tumekopa fedha za Watu, tunataka Umeme tuendelee na biashara ili turejeshe mikopo ya Watu, tutafilisiwa. VIONGOZI wetu saidieni. Bukombe [emoji23]
 
Ndugu,nimda toka tutoe Malalamiko yetu kupitia jukwaa hili, kuhusu huduma hafifu na ukosefu wa Mita za Njia Tatu, Maarufu Meter za Three phase Mkoa wa Geita na Wilaya zake, tunaomba VIONGOZI na Wahusika Mtusaidie jamani mwezi watatu huu Watu tumelipia Umeme, hutujaunganishiwa isitoshe hatuhitaji nguzo, kila tukiuliza tunaambiwa Mita zimeagizwa ulaya zikifika tutafungiwa, Sasa sisi tumekopa fedha za Watu, tunataka Umeme tuendelee na biashara ili turejeshe mikopo ya Watu, tutafilisiwa. VIONGOZI wetu saidieni. Bukombe [emoji23]
Wacha "muisome namba". Kifupi baada ya mfumo wa malipo ya luku kubadilika fedha zote zipo mikononi mwa Magufuri. Tanesco kwa sasa haina uwezo wa kununua kifaa chochote mpaka ipige goti na kuonyesha bakuri kwa magufuri iwe kununua vifaa vya mahitaji ya kawaida wala dharura. Na kwa miundombinu ya Tanesco ilivyo mibovu tusubiri kulia chozi la damu ila kumbuka kutolaumu Uongozi wake mlaumu huyo wa kunyumba aliye magogoni
 
Tanesco, hivi utaratibu kubadilishiwa mita ya luku,ukoje?,maana ni wiki sasa nimetoa taharifa na nazidi kulala giza.
 
Ndugu zangu niasaidieni maji yako shingoni nimenunua umeme kimakosa badala ya 50000tzs nikanunu 500000tzs Nasaidiwaje kwa hilo??
 
Tanesco naomba mnifafanulie hili jambo, nimenunua umeme mara mbili lkn napata units pungufu kulingana na pesa niliyolipa! nimelipa Sh. 2000 nimepata unit 2.9 badala ya 5.7 baadae nikanunua wa Sh. 1000 nikapata unit 1.5 badala ya unit 2.9. Naomba ufafanuzi tafadhali
 
nyie TANESCOOOOOOOO,kwanini mnakata umemeeeeeeeeee?kuna nini now na mmetoka nduki humu hamjibu?
njoo utujibu hapa!Lione!
mnasababisha viwanda vyetu havifanyi kazi.
 
Ndugu zangu niasaidieni maji yako shingoni nimenunua umeme kimakosa badala ya 50000tzs nikanunu 500000tzs Nasaidiwaje kwa hilo??

Nenda selcom au maxmalipo watakupa form ambayo utaenda nayo ofisi za tanesco
 
Nahitaji kujua umeme wa bei nafuu naupataje kwa sisi wenye matumizi yasiozidi unit 75 kwa mwezi
 
Tanesco Kusini umeme ulishawashinda kabisa, huu umeme umekuwa kama undicator za gari ni hovyo kabisa halafu mnahubiri viwanda.

"I wish I kould be bosi wenu ningesimamisha wote kazi".
 
Nimepitia uzi wenu wa 'zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na Tanesco'. Kwenye huo uzi mmesisitiza baada ya surveyor kupita, malipo ili kuvutiwa umeme yatafanyika bank tu. Pale Himo ofisi ya Tanesco, ukifika hawakupi hiyo reference number ya kwenda kulipia bank. Wanakwambia hivi sasa network imekata, so inabidi ulipie palepale Tanesco. Then wanakuandikia risiti wao, wanaigonga muhuri. Hili swala limekaaje kwa ofisi zenu za mikoani. Sababu kwa jinsi mlivyotoa msisitizo wa kulipia bank, hapa naona kuna kitu si cha kawaida. Kunawatu huko mikoani wanajipigia tu hela ya serikali na wananchi. Pale himo fomu ya maombi unauziwa, pia unatakiwa utoe na hela ya surveyor. Funny enough surveyor akija anakuomba pesa ya nauli. Anakuja na pikipiki ya kukodi. Ila ukiangalia vizuri hakuna dalili za kukodi, ni mradi wake au wanagawana pesa na yule kijana anayeendesha ile pikipiki. Vitu vitu vyote hivyo ni kinyume na maelezo yenu.
Hii post mbona hamtaki kuijibu na unakwenda mwezi wa pili sasa. Ni bora mngebadili heading ya huu uzi wenu, kuliko kutuhadaa watanzania kwamba tutoe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri. Ila sitachoka, naenda ngazi kwa ngazi, na hii ni moja ra reference zilizopo. Asanteni sana.
 
Back
Top Bottom