TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Namba ngapi mpendwa mteja
Mita namba 24213664451,nipo dar nimeenda Tanesco kibaoni wamesema hyo huduma kwa jiji la dar haipo kwa sasa kwa sababu haipo,kwa sababu watu wa mjini mkiwahamisha wote tariff shirika litakosa mapato,je hilo ni jibu la shirika au?
 
Nimepatwa na tatizo nimeshindwa kuongeza umeme meter namba tatu zimegoma kabisa battons hazifanyi kazi. Meter haijamaliza hata mwaka nipo Dodoma mjini. Suluhisho LA tatizo hili ni nini?
 
Kwanini hamtaki tupigie picha daraja la mtera?
mbn wenzetu wa manzese ni full kujiachia,ndio kwanza na wapiga picha tayari wapo pale,na sisi wa mkoani tukienda Dar bila kwenda kupiga picha juu ya lile daraja hauaminiki kama kweli ulifika Dar,sasa kwanini na pale bwawani darajani msituruhusu na sisi tujimwaemwae?
majibu tafadhali..
 
Kuna hili tangazo kwenye website yenu kuwa mtakata umeme jiji la Dar kila jnne na jtano asubuhi hadi jioni kuanzia jnne ijayo sept 18 hadi november mwanzo I sababu ya marekebisho fulani.
Ndugu zetu hadi lini sisi wananchi tutaendelea kuteseka na kuharibu biashara zetu sababu ya kazi zenu?Kazi ikiharibu kazi nyingine kuna faida gani hapo?Teknolojia gani wenzenu wanatumia nchi nyingine na kufanya maintenance bila kukatia watu umeme?
Hizi sio emergence,ni scheduled maintenance ambazo haziishi katika mitambo zipo siku zote,sasa mtakata umeme hadi lini?miaka nenda miaka rudi hambadiliki Tanesco.
Hebu tafuteni njia ya kufanya kazi zenu bila kuharibu kazi za wenzenu bwana,hii imepitwa na wakati.Yaani miezi miwili mnakata umeme two days every week hatufanyi kazi?mnatuua jamani!
 
hakuna kitu kinaniudhi kama ili swala la tariff
Niko mtaa mmoja na jirani yangu matumizi ya umeme karibu yanafanana Mimi na yeye lakini yeye amejaza fomu amebadilishiwa Tariff hivi sasa ananunua umeme wa shs elfu Tisa (9 ,000 anapata unit 72
Mimi nanunua umeme wa shs 10,000 napata unit 28
Sasa haya mashirika ya umeme hapa Tanzania yapo mawili au hizi tariff zinatolewa kwa rushwa
Kama ni kukosa tukose wote au kupata tupate wote
hii taarifa nitafanya juu chini mbaka imfikie mh RAIS MAGUFULI
sisi sote ni watanzania haiwezekani wengine wapewe unafuu wa maisha sijui ni kwa rushwa ? Wengine tunyimwe hii ni double standard hatuwezi kuendesha shirika kwa stahili hii
huyo mkurugenzi wa Tanesco afanye maamuzi hama wateja wote wa mjini warudishwe tariff 1 au atuondolee huu ujinga wateja tupo mtaa mmoja vigezo na masharti matumizi chini ya unit 70 alafu mwingine apewe mwingine anyimwe ili aliwezekani kunyamaziwa ..
 
Ulilipia huduma gani na namba yako ya simu
nilinunua umeme kwa mara ya kwanza kwa ajili ya LUKU mpya...
niliuliza humu kiasi kinachopaswa kununuliwa ukanijibu 17500...ila nilivyoenda kwa muuzaji akaniambia nilipe 30000! na hapo bado haukupatikana umeme wa unit 40 kama ulivyoniambia bali wa unit 33.

na cha kushangaza imeandikiwa (kwenye karatasi ya mauzo) kuwa LUKU ni ya tarrif 1 ilhali matumizi kwa siku hayafiki hata unit 1!
 
hakuna kitu kinaniudhi kama ili swala la tariff
Niko mtaa mmoja na jirani yangu matumizi ya umeme karibu yanafanana Mimi na yeye lakini yeye amejaza fomu amebadilishiwa Tariff hivi sasa ananunua umeme wa shs elfu Tisa (9 ,000 anapata unit 72
Mimi nanunua umeme wa shs 10,000 napata unit 28
Sasa haya mashirika ya umeme hapa Tanzania yapo mawili au hizi tariff zinatolewa kwa rushwa
Kama ni kukosa tukose wote au kupata tupate wote
hii taarifa nitafanya juu chini mbaka imfikie mh RAIS MAGUFULI
sisi sote ni watanzania haiwezekani wengine wapewe unafuu wa maisha sijui ni kwa rushwa ? Wengine tunyimwe hii ni double standard hatuwezi kuendesha shirika kwa stahili hii
huyo mkurugenzi wa Tanesco afanye maamuzi hama wateja wote wa mjini warudishwe tariff 1 au atuondolee huu ujinga wateja tupo mtaa mmoja vigezo na masharti matumizi chini ya unit 70 alafu mwingine apewe mwingine anyimwe ili aliwezekani kunyamaziwa ..
Mkuu hili swali nimeuliza karibia mara kumi hapa sipati jibu,inabidi tukusanye maoni tumpelekee Rais Magufuli maana shirika zima halina majibu ya suala hili,
 
  • Thanks
Reactions: ADK
Mkuu hili swali nimeuliza karibia mara kumi hapa sipati jibu,inabidi tukusanye maoni tumpelekee Rais Magufuli maana shirika zima halina majibu ya suala hili,
Mkurugenzi wa Tanesco kwa ili swala la Tariff 1: sijui Tariff 4
Mara utasikia D1 D2 na kuendelea
Mnaonyesha kuyumba tena mnayumba sana
Maelezo yenu mnatupigia sim wateja cha maana hakuna ni porojo tu
hakuna cha matumizi ya majumbani wala viwandani
aliyetunga Sera matumizi chini ya unit 75 mteja anatakiwa awe tariff 4
huyu mtu yuko hai au kafa
Kama ili swala aliwezekani futeni matangazo yenu humu,sisi tunasoma matangazo yenu humu ndio maana tunahamasika.
 
Kuna tatizo hivi sasa la umeme wilaya ya mufindi hususani mji wa Mafinga mjini,umeme hauna nguvu, toka jana usiku umeme unakuja halafu unakata, ni bora ungezimwa Kwanza kuliko hivi, vitu vinaungua jamani.
 
Tanesco
Mteja anawekewa nguzo bila kuungwa wire wiki mbili
Huu ni utaratibu wenu?
Imagine unalipa huduma tangu May mpaka sasa hujapata umeme!
Ajabu kubwa kuna waliolipa July wameunganishwa na huduma.
Jamani sote ni watanzania.

Tanesco ya Mbezi ya Kimara

kuna customer care ya hovyo, majibu mabaya sana kwa wateja wapendwa hasa kwa afisa mahusiano pale Kontena na Chumba namba 8.
 
Asee Tanesco naomba mkaniwekee nguzo kwenye nyumba yangu Magu nmelpia toka may hadi leo hakuna umeme....afu ictoshe n nguzo moja 2...mbona naona wengne wakiwekewa umeme bila tatizo.....au hadi tupite mlango wa nyuma ambao Diwani Athumani anausimamia?
 
Kuna tatizo hivi sasa la umeme wilaya ya mufindi hususani mji wa Mafinga mjini,umeme hauna nguvu, toka jana usiku umeme unakuja halafu unakata, ni bora ungezimwa Kwanza kuliko hivi, vitu vinaungua jamani.
Je bado tatizo linaendelea kwaki? Tunakmba namba yako ya simu
 
Tanesco
Mteja anawekewa nguzo bila kuungwa wire wiki mbili
Huu ni utaratibu wenu?
Imagine unalipa huduma tangu May mpaka sasa hujapata umeme!
Ajabu kubwa kuna waliolipa July wameunganishwa na huduma.
Jamani sote ni watanzania.

Tanesco ya Mbezi ya Kimara

kuna customer care ya hovyo, majibu mabaya sana kwa wateja wapendwa hasa kwa afisa mahusiano pale Kontena na Chumba namba 8.
Tunaomba namba yako ya simu tufatilie swala lako mpendwa mteja
 
Kikubwa fuatilieni kuona tatizo ni nini hasa, ndio mtupatie jawabu hapa ndugu zanguni.
Inakatisha sana tamaa, to be fair.
 
Kikubwa fuatilieni kuona tatizo ni nini hasa, ndio mtupatie jawabu hapa ndugu zanguni.
Inakatisha sana tamaa, to be fair.
Tunapokuomba taarifa ndio njia moja wapo ya Makao Makuu kufatilia tatizo la mteja
 
Back
Top Bottom