TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1.ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2.NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3.KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4.JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5.MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6.KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7.KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

NAMBA ZA SIMU ZA MADAWATI YA DHARURA YA TANESCO MIKOA YOTE

1. Ilala

0222133330/ 0784 768586/ 0715 768586.

2.Kinondoni Kusini (Magomeni)

0784271461/ 0715271461

3. Kinondoni Kasikazini(Mikocheni)

0784 768584/ 0716 768584

4. Temeke

0222138352/ 0732 997361/ 0758881055/ 0712 052720

5. Pwani
078 5122020/065 7108782/023 2402386

6. Mbeya
0759 777781/0787 023422


7.Arusha
0758174343/
0622612501/
+255 27 2506110

8.Tanga
0658 122 412/0687 677 667/ 027 2646 779

9. Kilimanjaro
0765 397 925/0682 771 310/ (+255) 272 755 007/8

10 Manyara
0689 795 599/ 0627938951

11. Mwanza
0759 777 786/0687 910 202/
(+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

12. Geita
0744 085 696/(+255) 28 2520330

13.Kagera
078 5 787 898 / 075 3 120 701/(+255) 282 220 061

14.Mara
0788 950 688/
028 262 2020/
0762 165 087

15.Simiyu
+255 282 700 180/0626383440/0745044072

16. Dodoma
0782 161 643/(+255) 262 321 728

17. Morogoro
068 4889272 /065 4829046/ (+255) 232 613 501/2

18 Singida
071 4 477 445 /0732 960 924 / 0689 373 757/(+255) 262 502 133

19. Tabora
0786 558 510 /0763 162 868

20. Shinyanga
0754 521 070/(+255) 28 2762120 /
0783 521 070

21. Kigoma
078 3720598/(+255) 2988226

22. Katavi
0688345200

23. Rukwa
0252161120/0768879813
24. Songwe
0684 611716/0763 430381.

25. Ruvuma
0252602281/0763 194 979/0787 758 986

26. Njombe
0744703988

27. Mtwara:
0789 999942/023 2333902

28. Iringa 0262702019/0739203015

29. Lindi
0752518247/0685692786


Kituo cha Miito ya simu/Call Centre Makao Makuu

0768 985 100/0222194400

Facebook
www.facebook.com/tanescoyetu

Twitter
www.twitter.com/tanescoyetu

Tovuti
www.tanesco.co.tz

Barua pepe
Customer.service@tanesco.co.tz

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu


NIna swali moja tuu. Mimi niko eneo ambalo linahudumiwa na umeme wa REA. Nyumba yangu nimefanya wiring kila kitu tayari, wakaja watu wa Tanesco kupima, wakaondoka na vipimo vyao, baada ya wiki nikatumiwa ujumbe nikalipie. Nikaenda nimelipia ili kuwekewa huduma ya umeme ambapo haihitajiki nguzo. Ni waya tuu kutoka kwenye nguzo na kuingiza kwangu.

Leo ni siku kumi zimepita tangu nilipie naona kimya, nikiwafuata maofisini huko naambiwa kisheria ni ndani ya siku 30. Sasa nauliza hizo siku 30 ndo tuseme mnatafuta nini ambacho hamna nyie? Yaani waya wa mita 30 tuu na mita ndo nisubiri siku 30? Nina hasira mimi. Nikadadisi kwa wenzangu mtaani ndo nikachoka kabisa, yaani naambiwa kuna watu wamekaa miezi miwili baada ya kulipia bado hawajawekewa umeme. Huu ukiritimba utaisha lini?

Au tutoe taarifa kwa viongozi wa kisiasa kama mawaziri na wakuu wa mikoa ndo mje mtuhudumie?
 
Tanesco, nimekosea kuandika namba ya mita yangu wakati wa kununua umeme, na nimeshapewa unit ambazo haziingii kuingia kwenye mita yangu, utaratibu wa kupata unit zinazoweza kuingia kwenye mita yangu upoje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NIna swali moja tuu. Mimi niko eneo ambalo linahudumiwa na umeme wa REA. Nyumba yangu nimefanya wiring kila kitu tayari, wakaja watu wa Tanesco kupima, wakaondoka na vipimo vyao, baada ya wiki nikatumiwa ujumbe nikalipie. Nikaenda nimelipia ili kuwekewa huduma ya umeme ambapo haihitajiki nguzo. Ni waya tuu kutoka kwenye nguzo na kuingiza kwangu.

Leo ni siku kumi zimepita tangu nilipie naona kimya, nikiwafuata maofisini huko naambiwa kisheria ni ndani ya siku 30. Sasa nauliza hizo siku 30 ndo tuseme mnatafuta nini ambacho hamna nyie? Yaani waya wa mita 30 tuu na mita ndo nisubiri siku 30? Nina hasira mimi. Nikadadisi kwa wenzangu mtaani ndo nikachoka kabisa, yaani naambiwa kuna watu wamekaa miezi miwili baada ya kulipia bado hawajawekewa umeme. Huu ukiritimba utaisha lini?

Au tutoe taarifa kwa viongozi wa kisiasa kama mawaziri na wakuu wa mikoa ndo mje mtuhudumie?
Mkuu

Bora ww siku kumi.. Sisi Wengine tokea tumefanyiwa survey ni wiki nne zimepita...

Hatujui ni lini tutaambiwa tukalipe na Hatujui ni lini tutawekewa umeme


Tanesco Kisarawe imezidiwa kabisa... Inahitaji kusaidiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari,mimi mkazi wa Mbezi-Mpiji Magohe -Kibesa naomba kuuliza je lini TANESCO mtatuletea umeme katika kijiji chetu ukitazama idadi ya wakaazi inaongezeka kwa kasi na ni miaka imepita tokea TANESCO wapite kufanya survey ya mahitaji katika kijiji chetu. Kwa sasa umeme unaishia Mpiji Magoe mwisho na ni takribani kilometers 2 toka unapoishia umeme na upande wa Mabwepande unapoishia umeme(transformer-HT) ni 1km.Kwa sasa idadi ya nyumba zenye kukaliwa na watu si chini ya 1200.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dawati la Dharura Temeke wafanyakazi wengi ni wapuuzi sana,yaani unawapigia simu nyumba ina tatizo la umeme wanakuuliza maswali wakiona hawawezi kupata posho kutoka kwa mteja hawaji lakini kuna maeneo kama vile Bar,Lodge na maeneo mengine yanayofanana na hayo wakiitwa wanaenda haraka sana coz huwa wanapigwa bia mbili tatu.
Kuna dada mmoja yupo dawati la dharura huyu akiwa zamu ni kheri usipige simu maana ana maswali ya kipuuzi kweli kweli ukiwa na roho ndogo unaweza kumtukana.Nyumba yetu inatatizo la umeme lakini leo ni siku ya tano hawataki kuja.Unapewa namba ya kupata huduma lakini ukiwapigia ukiwaambia mbona hamji wanakwambia fundi yuko njiani atakupiagia mnasubiri weee mpaka saa tano usiku mkiona maumivu ya kuliwa na mbu yanaongezeka mnaingia ndani kupambana na joto.Siwatukani ila dawati la dharura wilaya ya temeke limejaa wapuuzi
 
Mkuu

Bora ww siku kumi.. Sisi Wengine tokea tumefanyiwa survey ni wiki nne zimepita...

Hatujui ni lini tutaambiwa tukalipe na Hatujui ni lini tutawekewa umeme


Tanesco Kisarawe imezidiwa kabisa... Inahitaji kusaidiwa

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu kwa hiyo na mimi nijiandae kisaikolojia kusota kumbe? Looooh, yaani nilivyojipinda kufanya wiring na kupiga mbao za dari mpaka tunashindia milo miwili badala ya tatu nimeshawishi familia kuwa mwezi hauishi tutakuwa na umeme. Kweli walihamasika ila kwa mwendo huu naanza kujuta kiaina
 
Mkuu kwa hiyo na mimi nijiandae kisaikolojia kusota kumbe? Looooh, yaani nilivyojipinda kufanya wiring na kupiga mbao za dari mpaka tunashindia milo miwili badala ya tatu nimeshawishi familia kuwa mwezi hauishi tutakuwa na umeme. Kweli walihamasika ila kwa mwendo huu naanza kujuta kiaina
Ukitaka kuwajua tanesco ni waksti huu wa kuomba kuvuta umeme. Mi nimechoka hata kwenda kwenye ofisi zao hawana customer experiance kwa wateja wao kila anayeomba ndo uwa nafasi ya kuteseka kisaikolojia. Zimepita siku za huduma lakini sijafungiwa umeme. Tanesco hii takukuru wakae karibu wachunguze.
 
Ukitaka kuwajua tanesco ni waksti huu wa kuomba kuvuta umeme. Mi nimechoka hata kwenda kwenye ofisi zao hawana customer experiance kwa wateja wao kila anayeomba ndo uwa nafasi ya kuteseka kisaikolojia. Zimepita siku za huduma lakini sijafungiwa umeme. Tanesco hii takukuru wakae karibu wachunguze.

Tafuta elfu 50 alafu uone kama kuna mkate mgumu mbele ya chai.
Kuna mtu ameniambia hivyo leo mpaka imebidi nikae kitako kwanza.
 
Dawati la Dharura Temeke wafanyakazi wengi ni wapuuzi sana,yaani unawapigia simu nyumba ina tatizo la umeme wanakuuliza maswali wakiona hawawezi kupata posho kutoka kwa mteja hawaji lakini kuna maeneo kama vile Bar,Lodge na maeneo mengine yanayofanana na hayo wakiitwa wanaenda haraka sana coz huwa wanapigwa bia mbili tatu.
Kuna dada mmoja yupo dawati la dharura huyu akiwa zamu ni kheri usipige simu maana ana maswali ya kipuuzi kweli kweli ukiwa na roho ndogo unaweza kumtukana.Nyumba yetu inatatizo la umeme lakini leo ni siku ya tano hawataki kuja.Unapewa namba ya kupata huduma lakini ukiwapigia ukiwaambia mbona hamji wanakwambia fundi yuko njiani atakupiagia mnasubiri weee mpaka saa tano usiku mkiona maumivu ya kuliwa na mbu yanaongezeka mnaingia ndani kupambana na joto.Siwatukani ila dawati la dharura wilaya ya temeke limejaa wapuuzi
Tunaomba namba yako ya simu tafadhali na nani amekuomba rushwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari,mimi mkazi wa Mbezi-Mpiji Magohe -Kibesa naomba kuuliza je lini TANESCO mtatuletea umeme katika kijiji chetu ukitazama idadi ya wakaazi inaongezeka kwa kasi na ni miaka imepita tokea TANESCO wapite kufanya survey ya mahitaji katika kijiji chetu. Kwa sasa umeme unaishia Mpiji Magoe mwisho na ni takribani kilometers 2 toka unapoishia umeme na upande wa Mabwepande unapoishia umeme(transformer-HT) ni 1km.Kwa sasa idadi ya nyumba zenye kukaliwa na watu si chini ya 1200.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tunaomba namba yako ya simu tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari nilinunua umeme kwa mara ya kwanza meter namba 54182472701 Sasa unit zangu 40 bado sijapewa mpk leo nilikuwa naomba msaada wa kuzipata. eneo kibamba hondogo jina Bernard Bakari Lingowe
 
Habari nilinunua umeme kwa mara ya kwanza meter namba 54182472701 Sasa unit zangu 40 bado sijapewa mpk leo nilikuwa naomba msaada wa kuzipata. eneo kibamba hondogo jina Bernard Bakari Lingowe
Kwani hizo Unit 40 Zinatolewa Burr Mkuu? Maelezo Tafadhali.
 
hahahahahaha siyo bure mkuu ukinunua umeme kwa mara ya kwanza wanakata unit 50 sasa wakati wananiunganishia walinipa unit 10 hivyo katika 50 nawadai unit 40 sasa walisema watanitumia baada ya wiki moja lakini wapi siku zinasonga tu mpk nimechoka kusubiri.
 
Tupende kufata taratibu mpendwa mteja wetu hakuna kutoa rushwa

Sent using Jamii Forums mobile app

Acheni kujishebedua huku mitandaoni na kwenye TV kusema hakuna kutoa rushwa, mandumilakuwili nyie. AU mnataka tuanze kuwaanika tena kwa majina ili mtumbuliwe? Leo hii nimeongea na fundi wangu aliyenifanyia wiring tena ni miongoni mwa mafundi ambao ni recognized contractor na Tanesco. Alinipigia simu kuuliza kama nimewekewa umeme? Nikajibu hapana, bado hawajaja. Akaniambia you cant be serious. Maana kuna mtu amelipia umeme juzi, leo ameshawekewa.. Nilipomdadisi akaniambia ila inabidi kama una chochote kesho tukafanyie kazi, kesho kutwa utapata umeme.

Tunajua picha kamili inayochezwa... msidhani watanzania ni wajinga kiasi hicho. Huyo mteja aliyewekewa ndani ya siku 2 amefuata taratibu zipi ambazo mimi sijafuata? Haki ya nani natafuta namba ya waziri mkatumbuliwe mmoja baada ya mwingine. Naongea kwa uchungu kwa sababu ya ubaguzi wa dhati unaofanyika Tanesco, mabosi wote na maengineer wao lao moja.
 
Tupende kufata taratibu mpendwa mteja wetu hakuna kutoa rushwa

Sent using Jamii Forums mobile app


Mteja ambaye eneo lake halihitaji nguzo, yaani yupo ndani ya mita 30. kinachohitajika ni mita, na waya tu mje kuunganisha, mnamwambia asubiri siku 30, kama siyo kutengeneza mazingira ya rushwa ni nini? Hiyo sheria ya kusema ndani ya siku 30 tafsiri yake siyo baada ya siku 30. Ni ndani ya siku 30, ikiwemo hata kesho yake mara baada ya kulipa. Sasa panafanyika delay techniques za makusudi. Kuna rafiki yangu aliambiwa eti mita zimeisha, imebaki moja tuu na inatakiwa iende sehemu nyingine. Jamaa kwa pressure akaingia kingi kwa kutoa rushwa ili hiyo mita ipelekwe kwake na ikawa hivyo. Japo hakuna ushahidi kama kweli mita imebaki moja.

Nyie ngojeni tu mimi nitawapa hela za moto
 
Hivi kwanini nguzo za umeme msiwe mnaziweka bure kupeleka umeme kwa wateja wenu?

Sent using Jamii Forums mobile app

Hiyo ni disaster. Kuna mtu aliweka umeme katumia nguzo 9. Mbaya zaidi wakamfanyia uhuni wanaweka zig zag ili nguzo ziwe nyingi kuliko umbali. Mwisho wa siku watu wengine wakija kujenga eneo husika zile nguzo ulizoweka ni mali ya tanesco siyo mali yako. Yaani utawaona majirani zako wanasherehekea kuweka umeme bila kutumia nguzo, na hakuna utakachoambulia.


Ingekuwa akili yangu, wateja wanaohitaji umeme wangewekewa hiyo huduma bure alafu baada ya mteja kupata hiyo huduma, akawa analipa deni la hizo gharama kidogo kidogo kwa mfumo ambao tanesco watakuwa wametengeneza. Mbona bodi ya mikopo inasomesha wanachuo na baadaye inarejesha fedha zake tena kwa riba?
 
Back
Top Bottom