TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Hiyo ni disaster. Kuna mtu aliweka umeme katumia nguzo 9. Mbaya zaidi wakamfanyia uhuni wanaweka zig zag ili nguzo ziwe nyingi kuliko umbali. Mwisho wa siku watu wengine wakija kujenga eneo husika zile nguzo ulizoweka ni mali ya tanesco siyo mali yako. Yaani utawaona majirani zako wanasherehekea kuweka umeme bila kutumia nguzo, na hakuna utakachoambulia.


Ingekuwa akili yangu, wateja wanaohitaji umeme wangewekewa hiyo huduma bure alafu baada ya mteja kupata hiyo huduma, akawa analipa deni la hizo gharama kidogo kidogo kwa mfumo ambao tanesco watakuwa wametengeneza. Mbona bodi ya mikopo inasomesha wanachuo na baadaye inarejesha fedha zake tena kwa riba?
Tuhuma hizi unauhakika nazo? Umeme ni swala la kitaalamu hivyo sio kumsemea muhusika taratibu zipo na ofisi zetu zupo wazi penda kuzitumia kupata ufafanuzi sahihi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mteja ambaye eneo lake halihitaji nguzo, yaani yupo ndani ya mita 30. kinachohitajika ni mita, na waya tu mje kuunganisha, mnamwambia asubiri siku 30, kama siyo kutengeneza mazingira ya rushwa ni nini? Hiyo sheria ya kusema ndani ya siku 30 tafsiri yake siyo baada ya siku 30. Ni ndani ya siku 30, ikiwemo hata kesho yake mara baada ya kulipa. Sasa panafanyika delay techniques za makusudi. Kuna rafiki yangu aliambiwa eti mita zimeisha, imebaki moja tuu na inatakiwa iende sehemu nyingine. Jamaa kwa pressure akaingia kingi kwa kutoa rushwa ili hiyo mita ipelekwe kwake na ikawa hivyo. Japo hakuna ushahidi kama kweli mita imebaki moja.

Nyie ngojeni tu mimi nitawapa hela za moto
Alimpa nani hiyo rushwa? Kwanini hakutoa taarifa? Tusijenge mazingira ya muzusha mambo badala yake tusaidie kuwabainish mnaona wanaomba rushwa sio kuchafua shirika zima tena kwa taarifa zakusikia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acheni kujishebedua huku mitandaoni na kwenye TV kusema hakuna kutoa rushwa, mandumilakuwili nyie. AU mnataka tuanze kuwaanika tena kwa majina ili mtumbuliwe? Leo hii nimeongea na fundi wangu aliyenifanyia wiring tena ni miongoni mwa mafundi ambao ni recognized contractor na Tanesco. Alinipigia simu kuuliza kama nimewekewa umeme? Nikajibu hapana, bado hawajaja. Akaniambia you cant be serious. Maana kuna mtu amelipia umeme juzi, leo ameshawekewa.. Nilipomdadisi akaniambia ila inabidi kama una chochote kesho tukafanyie kazi, kesho kutwa utapata umeme.

Tunajua picha kamili inayochezwa... msidhani watanzania ni wajinga kiasi hicho. Huyo mteja aliyewekewa ndani ya siku 2 amefuata taratibu zipi ambazo mimi sijafuata? Haki ya nani natafuta namba ya waziri mkatumbuliwe mmoja baada ya mwingine. Naongea kwa uchungu kwa sababu ya ubaguzi wa dhati unaofanyika Tanesco, mabosi wote na maengineer wao lao moja.
Tafadhali tupatie taarifa za hawo unawatuhumu badala ya kutuhumu shirika zima.usitishie kuwaanika bali waanike ili shirie ichukue mkondo wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko TANESCO inaonekana kuna tatizo mahali,haiwezekani watu wengi humu tena hawa ni wachache kati ya waliopo huko nje wanalalamika changamoto ya kuvutiwa umeme, kwenye suala la nguzo hapo....Yote hayo nishayasikia pia hata mtaani watu wakilalamika........Ila siwezi sema mjirekebishe maana ni kama utaratibu wenu mliojiwekea
 
Tanesco madudu yamezid.. Toka jana saa tatu usiku hatuna umeme baada ya kupiga simu na kuwaambia tutampigia waziri husika wamerudisha ndani ya nusu saa wamekata.. Sijui hili shirika lina kasoro gani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafadhali tupatie taarifa za hawo unawatuhumu badala ya kutuhumu shirika zima.usitishie kuwaanika bali waanike ili shirie ichukue mkondo wake

Sent using Jamii Forums mobile app
Tanesco Nina nyumba nililipa January 2019 nyingine sikulipa ila control namba ninayo ya hii ambayo sijalipa nauliza he bado inakuwa active au mpaka nirudi kuihuisha? Nipo Mwanza na hii ya Kwanza mpaka Leo naambiwa nguzo hakuna nipe majibu yangu soon
 
Nina swali kwa Tanesco
Baada ya Survey inachukua muda gani kupewa control no ili ulipe kwa ajili ya kuunganishiwa umeme? Umbali wa nguzo ni mita 10 hadi ilipo nyumba.
 
Tanesco Nina nyumba nililipa January 2019 nyingine sikulipa ila control namba ninayo ya hii ambayo sijalipa nauliza he bado inakuwa active au mpaka nirudi kuihuisha? Nipo Mwanza na hii ya Kwanza mpaka Leo naambiwa nguzo hakuna nipe majibu yangu soon


hapana fika ofisi ya TANESCO kwa ajili ya kupata namba nyingine
 
Habari wanajamvi.

Jana umeme ulikatika hapa kijijini kwangu. Uliporudi kwangu haukurudi.
Remote inaonyesha error 30
Code walizonipa za tanesco hazifanyi kazi...

Unles kuna namna ya kuingiza ambayo mie siijui. (niliambiwa niingize tu zitafanya kazi)
Kuna anayefahamu namna ya kuingiza hizi namba??? (napewa ahadi ya kufika tu hawajafika)
Msaada tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanesco umeme kigamboni kunashida gani mbona unakatika na kuwaka zaidi ya mara nne sasa ndani ya masaa mawili.

Chunguzeni tafadhali mtatusababishia hasara katika malizetu please.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom