TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Serkal inarekebisha miundombinu hasa katika kilindi hiki cha mvua ukiona waya umeanguka usiukanyage pia usisahau kilipia luku


State agent
 
Wakata umeme wako canada bana tusiongopeane hapa
 
Nini chanzo?

Nimemuuliza mtu hapa US nilipo, umeme umekatika mara ya mwisho lini hapa?

Akaniambia kulikuwa na kimbunga kilipita kama miaka mitatu au minne iliyopita. Hata kukumbuka ni shida.

Sababu ya umeme kukatika ilikuwa ni kimbunga kikubwa na mvua, a natural disaster.

Umeme ukikatika watoto wanaona this is a penomena kama kupatwa kwa jua.

Sisi tumekosea wapi?

I just copped this.

20191123_163923.jpeg
 
Nashukuru sana na umenijibu vizuri sana na nimekuelewa ndugu Tanesco, je km hilo eneo halimo kwenye mradi na Tanesco\REA hawana mpango wa kunifikishia umeme kwenye eneo hilo linalo hitaji nguzo 11 , na tayari umeniambia kuwa ikizid nguzo mbili huo unajulikana km mradi nifanyeje ili nipatiwe huduma ya umeme?
UTEKELEZAJI wa miradi ya usambazaji umeme inaenda kwa awamu hivyo ikiwa mbali na miundimbinu unashauriwa kusubiri awamu yako kukufikishia umeme
 
Nawashukru kwa huduma hii, Mi niko Mwanza nina tatizo kama la ndugu hapo juu nimelipia TANESCO-NYAKATO nguzo mbili tangu Tarehe 6 Septemba 2016 hadi leo sijaletewa nguzo, kila siku madai ni hakuna nguzo sasa mi kama mteja hamuoni kama mnanionea?

Ikumbukwe hadi kulipa hiyo pesa kuna huduma niliamua kutozifanya ili nipate huduma ya umeme, badala yake nimekosa huduma zote mpaka leo huku nyie pesa yangu mkiifanyia biashara.

Naomba nipewe ufafanuzi kuhusu jambo hili.

Natanguliza shukrani zangu.

Umelipia nguzo?mbona wanatangaza nguzo hazilipiwi
 
Sisi wakazi wa Mwananchi, Nyakato, Buzuruga, Igoma tumepata adha kubwa tangu jana saa moja na nusu usiku mpaka leo saa moja na nusu kwa kukatika kwa umeme. Mpaka sasa hakuna sababu iliyotolewa juu ya kukatika kwa umeme huo ambao umechukua muda mrefu sana kuweza kurudi. Busara itumike kutueleza ni kitu gani kilichosababisha umeme kukatika muda mrefu hivyo na suluhisho linalotakiwa kuchukuliwa ili tatizo kama hilo lisitokee tena.
 
Sisi wakazi wa Mwananchi, Nyakato, Buzuruga, Igoma tumepata adha kubwa tangu jana saa moja na nusu usiku mpaka leo saa moja na nusu kwa kukatika kwa umeme. Mpaka sasa hakuna sababu iliyotolewa juu ya kukatika kwa umeme huo ambao umechukua muda mrefu sana kuweza kurudi. Busara itumike kutueleza ni kitu gani kilichosababisha umeme kukatika muda mrefu hivyo na suluhisho linalotakiwa kuchukuliwa ili tatizo kama hilo lisitokee tena.
Tumepokea taarifa kwa hatua zaidi
 
Habari tanesco naomba niungwe kwenye group la whatsap tanesco wilaya ya kahama nimetuma namba ya simu pm
 
Ni vigezo vip vinatakavyo mfanya mteja kuweza kujitoa kwenye service charge? baada tu ya kuwekewa umeme, na mda gani? Anaweza kujitoa pia mchakato wke kwa ujumla upoje?
 
Vishoka Tanesco Dar es salaam (Kituo husika nakihifadhi kwa sasa) wanasumbua wateja. Huwezi kumpata surveyor bila kupitia kwa kishoka. Control number bila kupitia kwa kishoka utaambiwa mtandao unasumbua, ukipitia kwa kishoka ni siku moja tu unapata. Kuunganishwa umeme kawaida inachukua 30 hadi 60, ukipitia kwa kishoka siku mbili tu. Hivi huu mchezo mtaundekeza hadi lini?
 
Back
Top Bottom