TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Je vigezo gani mtu anaingia kwenye Tarrif 4? Binafsi nimejaribu kupunguza matumizi ya umeme ili niweze kuingia kwenye tarrif 4.

Nilienda ofisi za Tanesco kuwaeleza kwamba nimebana matumizi ambapo sasa natumia unit 72 mpka 74 lakini walikataa kuwa sina vigezo kwasababu huwa nanunua umeme mwingi.

Kweli sikuridhika ni hili jibu naomba ufafanuzi.

Ne ni sahihi mtu anayenunua unit nyingi hawezi kuwa kwenye tarifu 4?
 
Yaani haiwezekani yanapita masaa zaidi ya 18 hamjarudisha umeme. Hivi mnajua hasara mnazotuletea nyie watu? TANESCO

Umeme umekatika tangu jana saa sita mpaka muda huu haujarudi. Yaani mmekua kero sana. Kama hamuwezi kuendesha mashirika nyeti kama hayo, si mtangaze tenda kuwe na ushindani.! Maana hizi kero zimezidi sasa kwa kujiendesha kwenu kwa mazoea huko
 
Code:
JPEG_20210209_174841_1894777457328338884.jpg
 
Mtu akitaka kuunganisha kwenye nguzo uliyo nunua tanesco unafanyaje?
 
Mtu akitaka kuunganisha kwenye nguzo uliyo nunua tanesco unafanyaje?
Nguzo ni mali ya TANESCO na sio ya mteja. Mtu akitaka kuunganisha umeme kutoka kwenye nguzo yoyote ile, inabidi awasiliane na TANESCO na afuate taratibu zao za kuunganishiwa umeme.
Maelezo zaidi watatatoa TANESCO wenyewe, na kama nimepotosha watasahihisha.
 
Mtu akitaka kuunganisha kwenye nguzo uliyo nunua tanesco unafanyaje?
Nguzo ukishailipia, na kusimikwa tayari sio mali yako tena, inakuwa ni mali ya tanesco, kama unaogopa hilo, kabla hujaenda kuilipia, washirikishe, majirani zako, ili mchangie gharama ya nguzo hiyo/hizo.halafu mmoja ndio akalipie.tofauti na hivyo hakuna namna unaweza kuwazuia wasichukue umeme hapo.
 
Je vigezo gani mtu anaingia kwenye Tarrif 4? Binafsi nimejaribu kupunguza matumizi ya umeme ili niweze kuingia kwenye tarrif 4.

Nilienda ofisi za Tanesco kuwaeleza kwamba nimebana matumizi ambapo sasa natumia unit 72 mpka 74 lakini walikataa kuwa sina vigezo kwasababu huwa nanunua umeme mwingi.

Kweli sikuridhika ni hili jibu naomba ufafanuziS
Kigezo kikubwa cha kuweza kuwa tarrif 4, ni lazima uwe na matumizi madogo sana kwa mwezi!!wastani wa unit 2.5 kwa siku.Na nilazima uwe na matumizi hayo angau si chini ya miezi mitatu mfululizo!!ila kama una cheza kwenye 72-74 kuwa tarrifu 4, una kidhi lakini hawawezi kubali kwani unacheza kwenye mstari mwekundu!!punguza angalau ufike kwenye units 40-50 kwa mwezi!!japo ni ngumu kama una vitu vingi!!kwani kwa mwezi lazima ununue units 77tu kwa sh.10, 000!!
 
Tatizo ni nini haswa mpendwa mteja wetu

Upo eneo gani

Wilaya gani
Matatizo yangu nimesha waambia huko juu mkaniomba no yangu ya simu inakuwaje tena sahivi mnaniuliza tatizo nini? Ok tatizo hasa ni mita yenu inakula umeme kama kiwanda emagin umeme wa elfu 50 haumalizi siku 10 na nina tv na fridge taa 9 tu,
 
Kigezo kikubwa cha kuweza kuwa tarrif 4, ni lazima uwe na matumizi madogo sana kwa mwezi!!wastani wa unit 2.5 kwa siku.Na nilazima uwe na matumizi hayo angau si chini ya miezi mitatu mfululizo!!ila kama una cheza kwenye 72-74 kuwa tarrifu 4, una kidhi lakini hawawezi kubali kwani unacheza kwenye mstari mwekundu!!punguza angalau ufike kwenye units 40-50 kwa mwezi!!japo ni ngumu kama una vitu vingi!!kwani kwa mwezi lazima ununue units 77tu kwa sh.10, 000!!
Asante mkuu
 
Mmeniunguzia vitu jana..utaratibu ukoje tanesco wa complaints..au ndo kalagabaho
 
Mmeniunguzia vitu jana..utaratibu ukoje tanesco wa complaints..au ndo kalagabaho
Unapaswa kutoa taarifa ofisi za eneo lako

Uchunguzi utafanyika kugundua chanzo cha tatizo na kama umekiuka matakwa ya maombi uliombea kisha taarifa itaonyesha chanzo na kama unastahili fidia au laa
 
Back
Top Bottom