TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Namba zetu unachukua lakini hupigi wala hata hubip..unazingua sana.
Tanesco mnatuletea umaskini tu
 
Namba zetu unachukua lakini hupigi wala hata hubip..unazingua sana.
Tanesco mnatuletea umaskini tu
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tafadhali tusaidia taarifa kamili ili tuweze kufanyia kazi taarifa zako

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja, JM
 
Mi ni fundi umeme wa majumbani.
Nipo Karagwe Kayanga.

Nimekuwa nikifanya kazi zangu vijijini hata wilaya za jirani.
Lakini nimekutana na tatizo la wizi wa umeme/uhujumu.

Wananchi walifungiwa mita lakini hawajawahi kulipia chochote. Huu ni mwaka wa tatu hivi.
Wanahitaji kulipa lakini wamekosa pa kuanzia maana wakienda kulipoti wanaogopa faini. Hili hali walifunga kipindi cha REA.Labda niseme inawezekana kuna namna wizi ulipita kipindi hicho. Maana wengi vijijini hawana elimu sahihi juu ya ufingaji wa umeme.

Hawafahamu habari za wakandarasi wakiwaona wafanyakazi wa TANESCO wanawaomba wawafanyie mifumo yote matokeo unatokea uhujumu.


WIZI WA MITA

Pia kwa sasa kimekuwapo wizi wa mita hasa zinazo pachikwa kwenye nyumba.

Kuna matukio kama matano ambayo nimekwenda kufanya tasimini ya uharibifu. Na kwa tukio baya nimekuta mita zimen'golewa na watuhumiwa hawajulikani.

Wateja huwa nawaelekeza ofisini watoe taarifa .Lakini huwa hawahudumiwi kwa wakati maana kuna taratibu za kuitafuta uanza kufanyika. Labda hamjagundua jambo mi hawa wezi wengine hutumia akili na ndiyo maana huwa mafanikio ya kuwapata hawa wahujumu hayafanikiwi.

Naomba muwe na timu ya kufuatilia uhujumu nje ya mfumo wenu wa ofisi.

Fanyeni upelelezi hata wa kiteknolojia kama inawezekana mita zote ziwe na gps ili ziweze kufuatiliwa kwa ukaribu.
Pili watumie Wakandarasi waaminifu maana wanajuana na wafundi wengi waaminifu.

Hapa chini nitaambatanisha picha ya mita ambayo ilikuwa inakaribia kuibiwa na wahujumu huku amewapa jina la utani.(VISHOKA) Lakini majirani waliwakurupua hawakumaliza hadhira yao. Lakini inavyoonekana hawa wezi waliwahi kuwasiliana kwenye mfumo wenu ama wamo maana wanajua pamoja kuuza hizo mita waibazo.


Pia nawapongeza TANESCO wilaya ya Karagwe kwa utendaji wao wa kazi wakati huu.Kuanzia mapokezi, Mhasibu,Meneja na vijana ambao wanafanya kazi na meneja. Wanajitoa sana maana wateja wangu ambao huwa wanahitaji huduma wanazipa kwa wakati.
Emergency wanastahili kupewa nguvu zaidi maana wanafanya kazi katika mazingira hatari hasa nyakati za usiku. Maana wana maeneo makubwa mno.

Naomba pia kama mtaweza kuipatia nguvu kazi sehemu ya sarveh maana ana eneo kubwa mno na hana usafiri wa kumfikisha eneo la kazi yake kwa wakati.


Walau ofisi impatie usafiri wa pikipiki maana anatembea mwendo mrefu sana na huenda anatumia muda mwingi sana kutembea na miguu kuwasadia wateja wetu.Maana nakumbuka kuna kipindi niliwahi kumuomba amsaidie bibi yangu (SINA MAHUSIANO NAYE YA DAMU) ambaye alikuwa katika mazingira magumu kidogo na kampuni yetu huwa inatoa msaada hasa wa kiufundi na matengenezo ikiwemo na vifaa kwa wazee wazee kama eneo limepata mradi mpya wa umeme.
Lakini survey alitumia gharama zake mwenyewe kujisafisha tena wakati ambapo alikuwa amechoka na kazi ni kama ilikuwa imeisha muda wake anamsaidia bibi huyo.



KWA LEO NAISHIA HAPO ILA WAKATI UJAO NITAKUJA NA JAMBO LINGINE.(UPOTEVU WA MITA ZA WATEJA)

OFISI NINAZO FANYIA KAZI NI

JOSSEPH KOMBA(DANDU )

View attachment 1788380
Tunashukuru kwa ushauri na taarifa mpendwa mteja wetu.Tafadhali tupatie namba yako inbox tuongee na kuweza kufanyia kazi changamoto za eneo husika
 
E1FbZCfXEAElHLU.jpeg
 
Nimepita twitter nimekuta maelezo hayo..kipengele 'd' kipo poa sana...we kila siku unaomba taarifa zetu tu hufanyii kazi
 
Ni kama umeweka ka ' automated sms'..jina..namba..eneo etc
 
TANESCO hebu naomba tusaidieni wakazi wa Kimara mwisho.Kuna laini hii inayotoka Ubungo kupitia upande wa Dawasco hadi machinjioni.
Inasumbua sana kukatika umeme.Ninavyoandika hapa umekatwa.Ni kila wiki lazima nije hapa kulalamika nadhani utanizoea maana nina muda mrefu naandika humu lakini tatizo hili haliishi line hii ya dawasco.
Hii ni too much line hii.
Kimara pana line mbili kubwa za umeme.moja inakwenda mpaka Mbezi inapitia upande wa kushoto wa Moro road kama unakwenda Mbezi(upande wenye zile nguzo zenu kubwa za high tension toka kidatu).Nyingine ni line fupi inatokea Ubungo,inapitia kulia kwa moro road inalisha maeneo ya ebonite college,kam college,Mavurunza,Matangini,dawasco,tra,kimara sokoni,mpaka machinjioni inaishia pale.Hii ya pili ndio ina shida ya kukatika umeme sana.Wewe nifuatilie utaona post zangu kila wiki humu miaka na miaka.
Tusidieni jamani wengine tumewekeza huku mnatutia hasara.Tatizo gani hili lisiloosha miaka na miaka au walau kupungua?kiila wiki ni hivi.
 
TANESCO hebu naomba tusaidieni wakazi wa Kimara mwisho.Kuna laini hii inayotoka Ubungo kupitia upande wa Dawasco hadi machinjioni.
Inasumbua sana kukatika umeme.Ninavyoandika hapa umekatwa.Ni kila wiki lazima nije hapa kulalamika nadhani utanizoea maana nina muda mrefu naandika humu lakini tatizo hili haliishi line hii ya dawasco.
Hii ni too much line hii.
Kimara pana line mbili kubwa za umeme.moja inakwenda mpaka Mbezi inapitia upande wa kushoto wa Moro road kama unakwenda Mbezi(upande wenye zile nguzo zenu kubwa za high tension toka kidatu).Nyingine ni line fupi inatokea Ubungo,inapitia kulia kwa moro road inalisha maeneo ya ebonite college,kam college,Mavurunza,Matangini,dawasco,tra,kimara sokoni,mpaka machinjioni inaishia pale.Hii ya pili ndio ina shida ya kukatika umeme sana.Wewe nifuatilie utaona post zangu kila wiki humu miaka na miaka.
Tusidieni jamani wengine tumewekeza huku mnatutia hasara.Tatizo gani hili lisiloosha miaka na miaka au walau kupungua?kiila wiki ni hivi.
Ahsante kwa taarifa tunaifanyia kazi.Jm
 
Tanesco mnazingua sana tangu jana hakyuna huduma ya LUKU , ukinunua kwa simu zote inakataa , mara nyingine ikikubali mnaleta Token feki , yaani mmefeli sana , na ule utaratibu wenu wa kusema na kutoa taarifa kama kuna shida kutumia vyombo vya habari hamsemi tena yani mmeboa sana watu wamelala gizani ,usumbufu mkubwa sana mmesababisha. Sidhani kama Kitengo chenu cha Mawasiliano kwa sasa kina fanya kazi zake ipasavyo Tunamkumbuka sana Leila Muhaji, sasahivi tungemsikia kwenye maredio huko anataoa ufafanuzi
 
Changamoto ya kulipia umeme ( LUKU)
Tokea jana mchana nimejaribu weka luku imekataa.. mtandao unaonesha nimeshalipa ila haileti token. Nomejaribu na tigo pia. But nikiweka inakataa. Malalamiko Arusha, Moshono
 
Changamoto ya kulipia umeme ( LUKU)
Tokea jana mchana nimejaribu weka luku imekataa.. mtandao unaonesha nimeshalipa ila haileti token. Nomejaribu na tigo pia. But nikiweka inakataa. Malalamiko Arusha, Moshono
mkuu vp umefanikisha hata mimi inanzingua tu
 
Tangu jana mnaonekana mna shida kwenye kununua luku. Baada ya ucheleweshaji nimepata token. Ila napoingiza umeme hauingii. Je hii itakuwa ni shida gani?

TANESCO
 
Nimepeleka form ya maombi ya kuunganishiwa umeme tangu mwezi wa 8 mwaka 2019 mpaka leo sijapata huduma
 
Tanesco kama kuna shida kwenye mfumo si mseme mbona hatuwezi kununua umeme kwenye mitandao ya simu?
 
Tanesco kama kuna shida kwenye mfumo si mseme mbona hatuwezi kununua umeme kwenye mitandao ya simu?
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MANUNUZI YA LUKU KWA BAADHI YA WATEJA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme.

Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka.

Tutaendelea kutoa taarifa kadri huduma itakavyo kuwa ikirejea.

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

Kituo cha miito ya simu makao makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya kijamii

Twitter: www.twitter.com/tanescoyetu

Facebook Tanesco Yetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Mei 18, 2021.
 
Tanesco kama kuna shida kwenye mfumo si mseme mbona hatuwezi kununua umeme kwenye mitandao ya simu?
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MANUNUZI YA LUKU KWA BAADHI YA WATEJA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme.

Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka.

Tutaendelea kutoa taarifa kadri huduma itakavyo kuwa ikirejea.

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

Kituo cha miito ya simu makao makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya kijamii

Twitter: www.twitter.com/tanescoyetu

Facebook Tanesco Yetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Mei 18, 2021.
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MANUNUZI YA LUKU KWA BAADHI YA WATEJA


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme.

Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka.

Tutaendelea kutoa taarifa kadri huduma itakavyo kuwa ikirejea.

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

Kituo cha miito ya simu makao makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya kijamii

Twitter: www.twitter.com/tanescoyetu

Facebook Tanesco Yetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Mei 18, 2021.
Jitahidini mrekebishe haraka , maana mnatukwamisha wateja wenu
 
Back
Top Bottom