TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Tunafanyia kazi tafadhali
TANESCO LINI MTANDAO UTAREJEA? NINA SIKU YA TATU SASA SINA UMEME ,MITA IMETEMPLE NIMETUMIWA NO ZA KU CLEAR KILA NIKIWEKA NAAMBIWA REJECTED(SIKU YA TATUU HII). MAFUNDI WA TANESCO WAMEKUJA WANATOA MAJIBU SIMPLE "SYSTEM IPO CHINI IKIKAA SAWA TUTAKUTUMIA NO ZINGINE UWEKE"[emoji3166]HIYO SYSTEM INARUDISHWA LINI?
 
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MANUNUZI YA LUKU KWA BAADHI YA WATEJA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu iliyotokea kwenye mfumo wa manunuzi ya umeme wa LUKU siku ya Jumatatu, Mei 17, 2021 na kusababisha baadhi ya wateja kushindwa kununua umeme.

Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wanafanya kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa haraka.

Tutaendelea kutoa taarifa kadri huduma itakavyo kuwa ikirejea.

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

Kituo cha miito ya simu makao makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya kijamii

Twitter: www.twitter.com/tanescoyetu

Facebook Tanesco Yetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Mei 18, 2021.
Hata namba za simu mnazotuwekea hazipokelewi mnaweka za nn sasa
 
Wasi wasi wangu kuna jambo Tanesco wanafanya. Na watakapo rudisha huduma INAWEZEKANA WAKARUDI NA BEI TOFAUTI YA UMEME PER UNIT.

Lazima umeme utapanda bei.
 
Hivi kwanini TANESCO msingetoa taarifa ya kutokuwepo kwa huduma ya luku watu wanunue umeme wa kutosha kuliko kufanya ujinga huu mlioufanya!!?

Au mnamtia hujuma Mama Samia maana hii kitu haijawah kutokea ikachukua muda mrefu namna hii.

Mnachokitafuta mtakipata.😈😈😈
 
Tafadhali tuwekeeni option ya kupunguziana Units. Siku ya tatu Leo sina umeme..samaki wote wabiashara wamechina zaidi ya tani moja.
 
Tunaomba mtueleze tatizo ni nini katika mfumo wa kununua umeme kwa njia ya mtandao naona tatizo hili ni kwa nchi nzima.
Muda huu natoka TANESCO makao makuu ya Mkoa wa MWanza, kompyuta wapo wanachezea game la karata maana mfumo wa kuuza umeme hakuna, asante sana kwa kuihujumu nchi!
 
Ngoja nivute pumzi kwanza ili nipoze hasira....nimepata sehemu ya kuhifadhi vyakula vyangu visioze kwenye friji...(kwa jirani)

Jamani Mama Samia Rais wetu mpendwa, unawategemea watendaji wako ndio wakupe taarifa kuhusu nchi yako eti? Kwa taarifa yako mtangulizi wako alikuwa na informers wengi nje ya system ya kawaida....
 
Kwa hiyo ina maana ni nchi nzima umeme haununuliki waziri mwenye dhamana na shirika amelala usingizi mpaka rais tumekwisha.
Ngoja nivute pumzi kwanza ili nipoze hasira....nimepata sehemu ya kuhifadhi vyakula vyangu visioze kwenye friji...(kwa jirani)

Jamani Mama Samia Rais wetu mpendwa, unawategemea watendaji wako ndio wakupe taarifa kuhusu nchi yako eti? Kwa taarifa yako mtangulizi wako alikuwa na informers wengi nje ya system ya kawaida....
 
Kwa hiyo ina maana ni nchi nzima umeme haununuliki waziri mwenye dhamana na shirika amelala usingizi mpaka rais tumekwisha.
Ni nchi nzima mkuu, kama una akiba ya unit kwenye meter yako jitahidi uzime vifaa na taa za ziada maana hakuna anayejua hili tatizo litatatuliwa lini, labda wadukuzi waliodukua bomba la mafuta la huko USA wameelekeza mashambulizi yao Tanzania!
 
Je unaongelea kijiji gani? TAFADHALI tambua huduma ya usambazaji wa umeme maeneo ambayo haujafika inaenda kwa awamu hivyo vijiji ambavyo havijapata vitafikiwa mwa awamu zijazo.Jm
Oya nimeunganisha umeme Direct kwangu

Kama fidia kwa uzembe wenu mkinikamata nitajua naenda vp kujitetea mahakaman

Heko TANESCO
 
Back
Top Bottom