Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Uzembe wake umegharimu maisha ya watu, lakini tulivyo wajinga ukisoma comments utaona watu wanahusianisha ajali na uchawi, wengine wanachukulia mzahaNingekua miongoni mwa mashuhuda na ninamuona huyo dereva wa fuso bado akiwa hai ambaye ndiye aliyesababisha ajali kwa uzembe, ningeenda kumsimanga na kummalizia afe vizuri.
Dah dah napafahamu huko barabara ya convent ya masista Huruma.Kijiji cha Ubaha. Unashuka posta ya zamani unaelekea shule ya ubaha unafika sehemu panaitwa maviloni. Hapo unaweza uliza ukaelekezwa. .
au unashuka kiboro unapanda mpaka ukute njia panda then hapo unauliza. .
Kivyovyote vile hii ajali ni uzembe wa madereva, na madereva wengi wa siku hizi ni wavuta bangi......Uzembe wake umegharimu maisha ya watu, lakini tulivyo wajinga ukisoma comments utaona watu wanahusianisha ajali na uchawi, wengine wanachukulia mzaha
Pole sana mkuu, hii "RAHA YA MILLENNIUM" ndio Raha gani?Poleni sana wajomba poleni sana akina Mrema. Hawa waliopata ajali ndiko bibi yangu alikozaliwa. Baba yangu angekuwa kwenye coaster hii aisee leo ningekuw nalia sana. .
Its very sad. Marehemu kafa na watoto wake watatu. Msiba mkubwa Rombo siamanzi kubwa sana ndugu zangu. .
Huwa tunasikia msiba za ajali ila usisikie kwa watu wa nyumbani very sad indeed. .
Raha ya millennium uwaangazie ee Bwana. .
Itakuwa ni typing error si unajua simu zinajiongeza! Milele imekuja millenniumPole sana mkuu, hii "RAHA YA MILLENNIUM" ndio Raha gani?
14 ni familia moja!!??Watu 17, ambapo 14 ni wa familia moja, wamefariki dunia na wengine 12 wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Magira Gereza, Tarafa ya Mombo wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amesema Ajali hiyo imehusisha gari aina ya Mitsubishi Fuso iliyoligonga gari aina ya Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Moshi kwa ajili ya mazishi.
Waliofariki kwenye ajali hiyo ni wanaume tisa, wanawake sita, watoto wawili mmoja wa kike na mmoja wa kiume.
Majeruhi 10 wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga, Bombo kuendelea na matibabu na wawili wamebaki Hospitali ya Wilaya Magunga huku hali zao zikiendelea vizuri.
Mgumba amesema miili ya marehemu ipo katika Hospitali ya Wilaya Magunga, Korogwe.
Chanzo cha ajali ni kimeripotiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa gari aina ya fuso kutaka kulipita gari lililokuwa mbele yake na ndipo lilipogongana uso kwa uso na Coaster hiyo.
TBCOnline
Marehemu kaondoka na roho zingine 17إنا لله وإنا إليه راجعون
Utaratibu wa kusafirisha maiti ni katika taratibu mbaya zaidi katika kushughulikia mwili wa marehemu, kwanza husababisha huzuni zaidi kwa wafiwa na pia ni kwenda kinyume na mafundisho na maajabu waislamu nao siku hizi wanasafirisha.
Mzee wa utamaduni...tulia basiCoaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 Ikitokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.[emoji848][emoji2827]
Marehemu hakuwa tayari kusafirishwa? Ama kuna mtu hakupenda awepo kwenye msafara?