Gily Gru
JF-Expert Member
- Jul 4, 2016
- 8,632
- 23,673
I meant raga ya milele. .Pole sana mkuu, hii "RAHA YA MILLENNIUM" ndio Raha gani?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
I meant raga ya milele. .Pole sana mkuu, hii "RAHA YA MILLENNIUM" ndio Raha gani?
Ukiona mtu anakwambia HAKUNA UCHAWI ujue ndio mchawi mwenyewe huyo.Kuna minafiki haijui hata utani....
Mda wote sura zimekakamaa kwa kujifanya serious.
Na hiyo minified inayojifanya kupinga uchawi ndo inapaa usiku kabisaa
Usichokila usikitie hila
Uzembe wa madereva wewe ulikuwepo?ajali imesababishwa na uzembe wa madereva wote wawili
Hivi uislam hautakiwi,kusafirisha maitiإنا لله وإنا إليه راجعون
Utaratibu wa kusafirisha maiti ni katika taratibu mbaya zaidi katika kushughulikia mwili wa marehemu, kwanza husababisha huzuni zaidi kwa wafiwa na pia ni kwenda kinyume na mafundisho na maajabu waislamu nao siku hizi wanasafirisha.
9View attachment 2505507View attachment 2505508View attachment 2505511
Picha za Ajali
Ndugu waandishi wa Habari na Ndugu wananchi wa Mkoa Wa Tanga na Tanzania kwa ujumla Nimepokea kwa masikitiko makubwa tukio la Ajali Mbaya iliyotokea usiku wa leo. Ajali hiyo imehusisha Magari mawili na kusababisha Vifo vya watu 17 na Majeruhi 12 Pamoja na Uharibifu mkubwa wa Magari hayo..
Ajali ilitokea Tarehe 03/02/2023 Majira ya Saa 4.30 Usiku Eneo la Magila Gereza Kata ya Magila Gereza Tarafa ya Mombo Wilayani Korogwe, Barabara Kuu ya Segera - Buiko.
Magari yaliyohusika na Ajali hiyo ni Gari Na T.673 CUC aina Mitsubish Fuso Ikiendeshwa na Dereva ambaye Jina Lake Halijafamika iligonga na Gari T.863 DXN aina ya Coaster Coaster Iliyokuwa imebeba Mwili wa Marehemu n Abiria 26 iliyokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa mazishi.
Ajali hii inasababisha Vifo 17 na Majeruhi 12. Ambao Majina yao wote Hayajafahamika. Miili ya Marehemu imehifadhiwa katika Hospitali yetu ya Wilaya Ya Korogwe na Majeruhi 10 Wamehamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo na Majeruhi 2 wamebaki Hospital ya Korogwe Kwa Matibabu.
Chanzo cha Ajali ni Mwendo Kasi na Uzembe wa Dereva wa Gari Na :T.673 CUC M/Fuso Kulipita gari la mbele Bila Ya kuchukua Tahadhari na kugongana Uso kwa uso Gari Na :T.863 DXN T/Coaster
Tukio la Ajali Baada ya kukaguliwa , Magali yote yameshaondolewa barabarani na Sasa Barabara inapitika.
Mgumba T. Omary
Mkuu wa Mkoa Wa Tanga.
LNarudia tena Tanzania ni miongoni mwa nchi hatarishi uwapo barabarani.
Ajali za namna hii zinaakisi akili za watu wetu kwamba sisi ni taifa la wajinga wengi.
Siku moja, nimepewa lift na ndugu yangu mtu mwenye elimu yake na kazi nzuri, lakini namna alivyokua anaendesha ovyo barabarani nikasema huyu lazima apate ajali. Wamenishusha zangu Moro, wao wakielekea Dodoma, baadaye napata taarifa wamekula mzinga gari haifai, yeye na mkewe wameumia vibaya.
Pole kwa wafiwa, inasikitisha sana!!Poleni sana wajomba poleni sana akina Mrema. Hawa waliopata ajali ndiko bibi yangu alikozaliwa. Baba yangu angekuwa kwenye coaster hii aisee leo ningekuw nalia sana. .
Its very sad. Marehemu kafa na watoto wake watatu. Msiba mkubwa Rombo siamanzi kubwa sana ndugu zangu. .
Huwa tunasikia msiba za ajali ila usisikie kwa watu wa nyumbani very sad indeed. .
Raha ya milele uwaangazie ee Bwana. .
Inaumiza kwakweliPoleni sana kwa wafiwa.
Una msiba mzito marafiki wanajitolea kukusindikiza ukampumzishe mpendwa wako. Ajali inatokea hata wale wanaokupenda nao wanaondoka OMG[emoji24][emoji24][emoji24]
Sasa ndio marehemu Aue watu wote.. Hiyo fuso imezingua sana. Madereva wa tz tunatakiwa tupewe course upyaCoaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 Ikitokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.[emoji848][emoji2827]
Marehemu hakuwa tayari kusafirishwa? Ama kuna mtu hakupenda awepo kwenye msafara?
sasa nibishane na divisheni zero s ntakuwa kichaaUzembe wa madereka wewe ulikuwepo?
Tunaomba ripoti ya kiuchunguzi inayosema hivyo!
ACHA KIHEREHERE.
Nafundisha wakubwa uzalendo na kujitegemea, .T
Tuition yako ziwez kumleta mwanangu kama ndo comment yako hii tichaaa.......
Kaka pole sana, maana hata kuandika leo unakosea sana "RAGA"I meant raga ya milele. .
Dereva wa coster ni jirani yangu kule kijijini Anaitwa Festo Momburi. Yeye ilikuwa ndio shughuli zake. Alikuwa akipatikana pale biafra kinondoni. Wapumzike kwa amani.
Brother nazidi kukupa pole , mpaka simu ina kukataa kutaype bado haupo kwenye utulivu.I meant raga ya milele. .
Kaka sidhani kama ndivyo..ni uzembe tu wa madereva..Sisi wenyewe tuliwahi koswa na fuso mwaka Jana mwezi wa sita MITA kama hiyo tulikuwa tunamsafirisha mwili..pona yetu dereva wetu alikuwa yuko smart na anawafahamu vizuri madereva wa fuso..baada ya kuukwepa huo mtego nilimuuliza alijuaje..Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 Ikitokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.[emoji848][emoji2827]
Marehemu hakuwa tayari kusafirishwa? Ama kuna mtu hakupenda awepo kwenye msafara?
Lakini hawa ni wa mokala. Huko ubaa kivipiDah dah napafahamu huko barabara ya convent ya masista Huruma.
Kwa utaratibu wa Moshi..gari linalobeba mwili wa marehemu ndilo linalobeba ndugu zake wa karibu..kama ni baba basi humo watapakia mke na watoto..kaka na madada ..yaani wa ndugu wa karibu Sana..so waona utakuwa ni msiba mkubwa kiasi gani..yaani ni ukoo umeondokewa na watu waote haoHapo lazima kuna ndugu zaidi ya 10