Tanga: Milioni 21 waliyoiomba Wazee kwa ajili ya Tambiko yakwamisha Ujenzi wa Barabara

Tanga: Milioni 21 waliyoiomba Wazee kwa ajili ya Tambiko yakwamisha Ujenzi wa Barabara

Hii nchi tunaelekea pabaya sana aisee.

Tunafikia hatua ya kuamini mambo ya kishirikina hadi kutumia mamilioni ya wananchi kuyapeleka milima korelo?

WITCHCRAFT AND THE GOVERNMENT IS NEGOTIATING?! ASTONISHING.
 
Hio ni dili.... Lazima kuna watu nyuma ya hao wazee...

Kwani lazima barabara ipite hapo si wahamishe uelekeo tu...
 
Halafu mimi nimeshangaa hawa wazigua wenzangu wameanza kuijua hela kuanzia lini?

Maana hata ukienda kuoa kule mahali huwa ni sawa na bure!

Ukienda kuaguliwa bei sawa na bure!

Sasa hilo dau la ma milioni chungu nzima hayo tangu lini?!

Lini wameanza kuijua hela hawa wagosingwa?
Wewe acha kujipendekeza sio Mzigua,Wazigua tunaijua pesa kabla wewe huna dalili ya kuja Duniani
 
Hao wanaotaka mamilioni kwa ajili ya tambiko ni wahuni na wahujumu uchumi.
Walete break down ya hayo mamilioni tuone
Isije kuwa kuna asilimia kadhaa za viongozi wa serikali waliopanga huo mchongo wa kudai mamilioni ya tambiko.
Waambieni hao wazee barabara inajengwa kwa faida yao na watoto wao waache ungese.
 
Hiyo ni elimu pana sana kwenye maandiko matakatifu. Kwa kifupi, ni Malaika waliohasi na wako busy kututoa kwenye mstari wa kumuelekea Mungu wetu.
Na labda tunaweza tusiwe na uelewa wa kutosha kuhusu viumbe hivyo na tulivyonanyo kwenye maisha yetu ya kila siku lakini vipo. Na sio kwa Waafrika tu bali Duniani kote. Na kweli vina uwezo na hao Mababu wa Matambiko wanalijua hilo vizuri.
Hatahivyo suala la kuwafuata ama kuwategemea ni uamuzi wa binadamu.
Na ndio kurahisisha mambo Amri ya kwanza Mungu inatuambia tusiabudu “miungu” wengine.
Ndo umeamishwa hivyo na umekubali kuamini mkuu, siwezi kukubadili imani yako.

Ila kwangu mimi matambiko si mapepo yalikuwepo toka enzi na enzi. Huyo mkuu wa wilaya si mjinga kunegotiate na hao wazee, lazima watakuwa wamejaribu wameshindwa.

Nimeshuhudia visa kadhaa kwenye ujenzi kugoma maeneo ya matambiko.
 
Ndo umeamishwa hivyo na umekubali kuamini mkuu, siwezi kukubadili imani yako.

Ila kwangu mimi matambiko si mapepo yalikuwepo toka enzi na enzi. Huyo mkuu wa wilaya si mjinga kunegotiate na hao wazee, lazima watakuwa wamejaribu wameshindwa.

Nimeshuhudia visa kadhaa kwenye ujenzi kugoma maeneo ya matambiko.
Uwe na siku njema.
 
Huu ujinga na upumbavu ndo unasababisha nchi hii isiendelee!

How comes Mkuu wa Wilaya anazungumzia watu kulipwa hela za serikali ili wafanye tambiko???

Kama hawataki barabara kwa nini mnawapelekea? Waacheni na uchawi wao waendelee kuwa masikini na izo fedha za barabara pelekeni sehemu wanapojua maana ya maendeleo!


Hii ndio Taarifa mpya kutoka Kijiji cha Kwa Msisi Mkoani Tanga ambapo imeombwa kwanza hela ya Tambiko mil 21 ili ujenzi wa barabara unaohusisha ukataji wa miti uendelee.

Tambiko la pili litafanyika baada ya barabara hiyo kukamilika ambapo wazee watafanya dua maalum. Juhudi za Mkuu wa Wilaya kuomba punguzo zinaendelea.

Habari kamili hii hapa

 
Yaani watu wanacheleweshewa maendeleo eti kisa tambiko....sasa hayo matambiko yao yangekuwa na maana sitayari wangukuwa na barabara zao wenyewe tangu zama za kale...hayo matambiko na mizimu ingekuwa na msaada wote hao wazee wasingekuwa wamechoka hivyo na kuvaa manguo yamechanika.....DC acha story na hao watu peleka watu waanze kazi tena ikiwezekana peleka JWTZ kabisa hapo wajenge hiyo barabara... kila tukikwama tembezeni kipigo..
Tunaanza kuweka mambo ambayo baadae yanaweza kuleta matatizo katika kutoa maamuzi. Ukishakubali hayo matambiko yafanyike huko, huoni sasa matambiko mengi tu yatatokea sehemu nyingine za nchi? Je, katika Sheria ya Manunuzi tambiko linakadiriwaje? Hivi CAG atahakiki vipi gharama za hii kitu na kutoa thamani ya fedha kwa kazi ya tambiko lililofanyika?
 
Hao wanaotaka mamilioni kwa ajili ya tambiko ni wahuni na wahujumu uchumi.
Walete break down ya hayo mamilioni tuone
Isije kuwa kuna asilimia kadhaa za viongozi wa serikali waliopanga huo mchongo wa kudai mamilioni ya tambiko.
Waambieni hao wazee barabara inajengwa kwa faida yao na watoto wao waache ungese.
Hivyi Mbunge na mawaziri kutoka Tanga wameshindwa kuwaelimisha Hawa wachawi? Au na wao wanajipatia chochote Kama ulivyosema.
 
Tunaanza kuweka mambo ambayo baadae yanaweza kuleta matatizo katika kutoa maamuzi. Ukishakubali hayo matambiko yafanyike huko, huoni sasa matambiko mengi tu yatatokea sehemu nyingine za nchi? Je, katika Sheria ya Manunuzi tambiko linakadiriwaje? Hivi CAG atahakiki vipi gharama za hii kitu na kutoa thamani ya fedha kwa kazi ya tambiko lililofanyika?
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Back
Top Bottom