Niseme tu, nyakati zimebadilika sana. Leo hii hata kama angekuwepo Moses Kulola bado angepata taabu sana kuhubiri aina yake ya Injili. Baada ya kuja uchafuzi wa Injili ya wasaka afya na mafanikio, masikio ya watu wote, wapagani, Waislamu kwa Wakristo wameelekeza mioyo yao huko. Ndio maana utaona wafuasi wengi wa akina kuhani Musa, Mwamposa nk ni Waumini wa imani tofauti. Wahubiri wanaofuata maagizo ya Kristo kwa kuhubiri toba wapi ila hawawezi kuwa na mega churches, ni makusanyiko madogo mno. Matapeli wa Injili ndio wanawake, sawa sawa na Kristo alivyosema itakuwa nyakati za mwisho.
Hivyo hoja sio Kulola kutokabidhi kipawa kwa sababu afanyaye hivyo ni Roho Mtakatifu wala si mwanadamu. Tatizo hapa ni watu kupenda mafundisho ya uongo. Nakumbuka kwenye uchaguzi wa mwisho kabla ya kifo chake kulikuwa na njama za maaskofu kumng'oa Kulola. Sasa ndio uone uasi ulianzia humo humo ndani, na hao waliotaka kumng'oa ndio wameshika kijiti hii leo. Kutwa kucha mahakamani kwa kesi za wizi na kugombania madaraka. Vipofu wanawezaje kuwaongoza vipofu wenzao?
Moses injili yake haikuwa kushawishi akili
Kama leo mahubiri yake yalijikita kwenye kwenda Jehanamu kwa wenye dhambi na unyakuo watu waliokoka kibao
Akihubiri Habari xs Jehanamu neno linafanyika live kwa msikilizaji anaona Jehanamu live bila chenga na yeye akipelekwa ndio maana wengi walikimbia mbio kuokoka akihubiri unyakuo watakaoenda na kuachwa mtu atakaeachwa anapata maono live akiachwa watu wakinyakuliwa akiita kuokoka ili mtu asiachwe unyakuo watu walikuwa kama wehu wanakimbia mbele wengine mabosi maofisini
Sasa hivi mahubiri ya kiinjilisti yanawinda akili sio roho ndio maana matokeo madogo.
Sasa hivi wahubiri Jehanamu na unyakuo .hawapo
Moses alijikita maeneo hayo mawili tu ns watu walikoma walijua kiyama hiki hapa walikiona live bila chenga
Akihubiri mwenye dhambi utaachwa siku.ya unyakuo au utaenda Jehanamu alikuwa hatanii lazima Jehanamu uione live hapo hapo mkutanoni na maono ya kuachwa unyakuo ukija ujiaona bila chenga.Alikuwa.akihubiri dakika chache tu ila huo muziki wake mwenye dhambi lazima akimbie mbio kwenda madhabahuni hata kabla kuitwa akilia mno akilia kujali elimu yake au cheo chake
Aliamini kuwa neno lazima lifanyike mwili akihubiri Jehanamu mtu lazima aone Jehanamu akihubiri unyakuo mtu lazima aone live ns yeye anafall wapi?
Sasa hivi uinjilisti unawinda akili tu
Akilia kwa watakaoenda jehanamu mkutano wote unatungua kilio sababu Jehanamu kwao inakuwa live
Sasa hivi porojo nyingi zinahubiriwa injili za ku convince akili na kushawishi kujiunga na kadini ketu
Mtume Paulo alisema wazi nilipokuja kwenu sikuja na injili.ya ushawishi wa akili bali.katils udhihirisho wa nguvu za Mungu sio porojo.za ushawishi wa akili xa manipulation xa kisaikolojia za ku.manipulate human brain