Tanzania inatarajiwa kuingia mkataba na Kampuni ya DP World ya Dubai kuendeleza bandari ya Dar es Salaam
Bunge DHAIFU la CCM limepitisha azimio la kubinafsisha bandari ya DSM kwa kampuni ya DP World ya Dubai kwa miaka 100 hadi 2123.

#MyTake:
1. Maamuzi haya yamelenga kunufaisha watu wachache na kufuta urithi kwa vizazi vijavyo. Mwaka 2123 hakuna yeyote kati yetu atakayekua hai. Maana yake tumeamua kuwaachia msalaba wajukuu zetu ambao hata hawajazaliwa.

Unadhani Nyerere alishindwa kubinafsisha madini, bandari, mbuga za wanyama? Angeweza but alifikiria vizazi vya baadae. Ila sisi tumeamua kuuza urithi wa vizazi vyetu kwa tamaa ya muda mfupi. Tukikubali huu ujinga wajukuu zetu watapiga viboko makaburi yetu.

2. Kagame aliwahi kutukejeli tumpe bandari ya DSM atupe nusu ya bajeti ya nchi kila mwaka. Tukaona ametudharau. Lakini leo tunajiuza "cheap" kwa waarabu. Hakuna cha nusu wala robo ya bajeti. Kama tumeshindwa kuendesha bandari si bora tungempa Kagame, maana heri mwendawazimu uliyemzoea kuliko kichaa mpya.

3. Kampuni ya DPWorld inatuhumiwa "kupora" bandari nchi mbalimbali kwa kigezo cha uwekezaji. Bandari ya Sarubaya (Indonesia), Batangas (Ufilipino), Palao (Peru), Dakar (Senegal), bandari ya Djibout etc. Huko kote vimebaki vilio. Badala ya kujifunza, tumejipeleka kichwakichwa tukale za uso.

4. Katika kuonesha jinsi bunge lilivyo DHAIFU, limetoa siku 1 tu wananchi kutoa maoni yao. Yani jambo litakaloathiri maisha yetu na vizazi vyetu kwa miaka 100 ijayo litolewe maoni siku 1? Hawa watu wana kichaa? Halafu maoni yatolewe ukumbi wa Msekwa, uliopo bungeni. Ebo.!

Bandari inagusa maisha ya kila mtu, kuanzia mkulima wa Runzewe hadi Mwalimu wa Ludewa. Magari, mafuta, vyakula, nguo, pembejeo vinapita bandarini. Kugusa bandari ni kugusa maisha ya kila mtu. Ingeundwa kamati kukusanya maoni nchi nzima, sio kusema watu wakatoe maoni ukumbi wa Msekwa. Mwananchi wa Namtumbo anafikaje Msekwa?

5. Wananchi kataeni upuuzi huu. Mkinyamaza kwa kuona ni jambo la kisiasa msije kulia baadae. Maana mna "kaupuuzi" ka kunyamaza mkidhani waathirika ni wanasiasa tu. Utadhani bei ya petrol inapanda(ga) kwa wanasiasa tu. Siku yakiwachachia ndo mnaomba kupaziwa sauti. Ukikaa kimya usiombe kupaziwa sauti.
 
Bunge DHAIFU la CCM limepitisha azimio la kubinafsisha bandari ya DSM kwa kampuni ya DP World ya Dubai kwa miaka 100 hadi 2123.

#MyTake:
1. Maamuzi haya yamelenga kunufaisha watu wachache na kufuta urithi kwa vizazi vijavyo. Mwaka 2123 hakuna yeyote kati yetu atakayekua hai. Maana yake tumeamua kuwaachia msalaba wajukuu zetu ambao hata hawajazaliwa.

Unadhani Nyerere alishindwa kubinafsisha madini, bandari, mbuga za wanyama? Angeweza but alifikiria vizazi vya baadae. Ila sisi tumeamua kuuza urithi wa vizazi vyetu kwa tamaa ya muda mfupi. Tukikubali huu ujinga wajukuu zetu watapiga viboko makaburi yetu.

2. Kagame aliwahi kutukejeli tumpe bandari ya DSM atupe nusu ya bajeti ya nchi kila mwaka. Tukaona ametudharau. Lakini leo tunajiuza "cheap" kwa waarabu. Hakuna cha nusu wala robo ya bajeti. Kama tumeshindwa kuendesha bandari si bora tungempa Kagame, maana heri mwendawazimu uliyemzoea kuliko kichaa mpya.

3. Kampuni ya DPWorld inatuhumiwa "kupora" bandari nchi mbalimbali kwa kigezo cha uwekezaji. Bandari ya Sarubaya (Indonesia), Batangas (Ufilipino), Palao (Peru), Dakar (Senegal), bandari ya Djibout etc. Huko kote vimebaki vilio. Badala ya kujifunza, tumejipeleka kichwakichwa tukale za uso.

4. Katika kuonesha jinsi bunge lilivyo DHAIFU, limetoa siku 1 tu wananchi kutoa maoni yao. Yani jambo litakaloathiri maisha yetu na vizazi vyetu kwa miaka 100 ijayo litolewe maoni siku 1? Hawa watu wana kichaa? Halafu maoni yatolewe ukumbi wa Msekwa, uliopo bungeni. Ebo.!

Bandari inagusa maisha ya kila mtu, kuanzia mkulima wa Runzewe hadi Mwalimu wa Ludewa. Magari, mafuta, vyakula, nguo, pembejeo vinapita bandarini. Kugusa bandari ni kugusa maisha ya kila mtu. Ingeundwa kamati kukusanya maoni nchi nzima, sio kusema watu wakatoe maoni ukumbi wa Msekwa. Mwananchi wa Namtumbo anafikaje Msekwa?

5. Wananchi kataeni upuuzi huu. Mkinyamaza kwa kuona ni jambo la kisiasa msije kulia baadae. Maana mna "kaupuuzi" ka kunyamaza mkidhani waathirika ni wanasiasa tu. Utadhani bei ya petrol inapanda(ga) kwa wanasiasa tu. Siku yakiwachachia ndo mnaomba kupaziwa sauti. Ukikaa kimya usiombe kupaziwa sauti.
Msisingizie mama wa watu kuwa amewafanyeni wapumbavu. Mama wa watu amewakuta mmeumbwa hivyo na maupumbavu yenu.
Tangu lini mliwahi kutokuwa wapumbavu
 
Yaani sijui Kuna watu huwa wanafikiria Nini,mtu huna uchungu kabisa na nchi yako urithi wa taifa lako unautoa kihivi kweli,Kwanini tunafikiri pafupi hivi ,akili zetu zimeishia wapi.Ebu tuzinduke hata Kama Ni raia wa kawaida sauti zetu tusipaaze zisiishie kwny minong'ono tuseme ukweli.
 
Yaani sijui Kuna watu huwa wanafikiria Nini,mtu huna uchungu kabisa na nchi yako urithi wa taifa lako unautoa kihivi kweli,Kwanini tunafikiri pafupi hivi ,akili zetu zimeishia wapi.Ebu tuzinduke hata Kama Ni raia wa kawaida sauti zetu tusipaaze zisiishie kwny minong'ono tuseme ukweli.
Watu wameshasain mkuu
 
Wabunge ambao kweli wanaelewa biashara ni Shabiby na Kimei. Sijasikia mawazo yako kwenye hili na tuwe makini kama hawatachangia!

Nafikiri kama sisi wengine tusiunge mkono au kukataa nia pekee bali tuangalie mkataba na kuona je mkataba una nini hasa? Cha kushangaza kuna wabunge wanaunga mkono bila hata kujua mkataba ukoje?
 
Kwa maoni yangu, hakuna mkataba hatari kuwahi kutokea kama huu baada ya Uhuru.

Huu ni mkataba kama aliosaini Mangungo kwa Carl Peters.

1. Bandari zote za Tanzania Bara zinakwenda kuchukuliwa na Waarabu.

2. Waarabu wanakwenda kuchukua ardhi ya Tanzania Bara kiasi chochote wanachokitaka.

Maana yake ni kwamba, hata kama watataka kuchukua Mikoa yote ya Tanzania Bara, watachukua tu.

Ninachokiona mimi ni kwamba, wakishachukua Bandari zote Tanzania Bara, wataanza kuchukua ardhi ya Nchi kavu.
Hapo wataweza kuchukua hata mbuga za wanyama na hata migodi yote. Maeneo hayo yatachukuliwa kwa visingizio mbalimbali.

Rai yangu ni kwamba:-
*Viongozi wetu wa Dini zote wapaze sauti hadharani bila kificho kupinga jambo hili.

*Waandishi wa habari waungane kupinga jambo hili.

*Watanzania wote wote bila kujali tofauti zetu tupaze sauti zetu kupinga jambo hili.

Zaidi sana Serikali hii iunde majopo huru kadhaa ili kujadili kwa kina mkataba huu kabla mambo hayajaharibika.
Majopo hayo yahusishe viongozi wa kimila, viongozi wa Dini, Vyama vya siasa, Wananchi wote wa Bara (NB:- Wananchi wasiwakilishwe na viongozi wa siasa)

RIP, JPM, Baba.
 


Tanzania Jamani Inatia Kinyaa Wasomi Sijui Wamesoma Nini

 
Back
Top Bottom