Tanzania kuna familia ambazo zinaishi kifalme bila Watanzania kuzifahamu au wamepiga kimya tu

Bado kitambo kidogo nao watakuwa wa kawaida tu
Mwl alikoroga udongo akasemaaaaa ( usultani ufamle havina nafasi kwenye ardhi ya Tz)
Acha wajitutumue lakini muda ni mwalimu mzuri sana
Peace of mind huwa haipatikani kwa kuwa na Mali wala nyadhifa !! Hicho ndicho kinachowatesa watu !!
 
Mkuu,

Tatizo kubwa watu hawataki kuona uhalisia huu.

Halafu, watu wanatakiwa kujua Wanasiasa wote Ni Wale wale. Hakuna MALAIKA.

Hata ikitokea CCM ikatoka madarakani, kitakachoendelea Ni jina la chama tu, ila watu Ni wale wale.

Lowassa wa CCM ndiyo yule yule wa CDM.

Bible inasemq, palipo na mzoga ndipo wakusanyikapo TAI.

Chama chochote kitakachokuja kuingia madarakani, hata iqe CHAUMA huko huko ndiko wazee wa FURSA watakakohamia, maana kuhama Vyama Ni demokrasia na haki yake.

Kwahiyo, utakuwa Hawa watu unaokesha unatukana kumbe sababu wako CCM au chama usichokipenda na siyo kwamba wanachofanya hukipendi
 
Mi nauliza tu kuna member mwenzetu hapa Andrew Nyerere sijui yuko wapi?
Ni muda sasa hajasikika,karudi Butiama?hana bando? Au nini kimemkumba.
Huyu ndie mmiliki mjengo wa mzee pale Msasani kama madai yake yanavyosema.
Kuna hoja zake nyingi humu zina changamoto sana.
 
Vumilia mkuu,mi nimeamua kuwa mkimbizi ndani ya nchi yangu mwenyewe.
 
Fred Lowassa ni mbunge wa Jimbo la monduli. Kaachiwa jimbo na baba yake.

Hali hii mwisho italeta changamoto kwenye jamii isipodhibitiwa.
 
Fred Lowassa ni mbunge wa Jimbo la monduli. Kaachiwa jimbo na baba yake.

Hali hii mwisho italeta changamoto kwenye jamii isipodhibitiwa.
Anyway, huwezi kutumia nguvu zako zote akili na maarifa kupigania maslahi ya mwanasiasa kuliko yako halafu ukaanza kushangaa kwanini mwanasiasa anafanikiwa kuliko wewe.

Unamsindikiza mwanasiasa kwenda kuchukua fomu ya kugombea

Unaenda kumsikiliza kwenye kampeni zake na kumsifia muda wote 24/7.

Unamchangia pesa.

Unaenda kumpigia kura. Halafu unabaki kituoni mpaka atangazwe kushinda.

Wasipomtangaza kashinda unaandamana na kupigwa ukishinikizwa atangazwe ameshinda.

Kwa hali hiyo unashaangaaje mwanasiasa kufanikiwa kuliko wewe?
 
Kama mtu ametaka kuwa mwanasiasa na mkampigia kura na akapita.....shida iko wapi akiwa serikalini?
 
Hao wanaishi kwa kodi zetu maisha yao yote bila kodi zetu hawawez kuendesha maisha na utawasikia wakiwaambia mjiajiri
 
Fred Lowassa ni mbunge wa Jimbo la monduli. Kaachiwa jimbo na baba yake.

Hali hii mwisho italeta changamoto kwenye jamii isipodhibitiwa.
Kwani si amepigiwa kura
Na wananchi jimboni kwake hawana shida nae 🤷🤷🤷
 
I have got no problem of who is doing what if the doing is done na sio kufuja mali na kujaza matumbo yao bila kushiba....

Tatizo nothing is done..., Jambo ambali ningekasirika hata kama hao wanaotakiwa kufanya wangekuwa wametoka Sayari tofauti....

Tatizo uongozi umekuwa sio utumishi / wito tena bali mtaji / fursa ya watu kujinufaisha; That's why unaongelea neema / kuula which means na wewe ungepata chance ungekula hio neema na sio kuwatafutia neema waliokuweka hapo...
 
Nafikiri kuna jambo halijakaa sawa kwa WaTz. Ninaamini lazima lipo genge lenye power,linakaa na vikao kupanga safu ya uongozi iweje. Huyu atapewa huku na yule kule.

Sasa ikitokea ukapita kibahati bahati bila hilo genge kuridhia ndio hivyo yatatokea ya kutokea
 
Na wewe pambana familia yako iishi kifalme.
Soma sana,
Fanya kazi kwa juhudi sana.
Tafuta konekeksheni sana,
Jipendekeze sana sehemu sahihi kwa wakat sahihi
AU
Pigani katiba mpya itakoyotoa fursa kwa yoyote mwenye talents na jitihada
Kusoma sana siku hizi sio tiket tena. Utaishia tu kaanzisha genge la nyanya
 
Ndio neema na baraka anazogawa Mungu kwa viumbe wake.why haijatokea kwa nyerere,kawawa,au mzee mangula?.tuwe wavumilivu nanyi siku moja itafika zamu yenu,sisi tunapumua na kutoa hoja JF kuna wengine wanapumulia mashine muhimbili,wengine hawajuwi wanakula nini? Leo na wengine wanauwana ukraine wanatamani wawe kama sisi ila haiwezekani, hayo yote hupangwa na Mungu na anamakusudi yake.cha msingi amani inalindwa tuendele kuchapa kazi maisha yaende.uwaza sana kwanini? Yule yuko vile utatenda dhambi bure ulitaka awe nani? Vile.tuwaombe watuongoze vema wasimwage damu za watu na kutenda haki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…