Kuna wakati huwa namkubali sana J.K Nyerere jamaa alikua mzalendo wa kweli sana
1. Jaribu kumlinganisha Nyerere kwa mtazamo wa umuliki wa mali kwa kuwaangalia maraisi wengine wa Afrika katika kipindi chake, angalia maraisi hao walipokuwa madarakani na baada ya kustaafu
2. Nyerere alidiriki kufunga ubalozi wa Israili na kufuta mahusiano nao licha ya kuwa Nyerere alikua mkatoliki haswaaa, lakini alifanya hili kuonyesha kuchukizwa na uvamizi wa Israili katika ardhi ya Palestina
Na hili alilifanya licha ya msaada mkubwa tu wa ujenzi wa UDSM na MUHIMBILI HOSPITAL ya leo
3. Alikubali lawama za udini kwa Wazee wa Dar es Salaam lakini alisimamia misingi ya usawa kwa wote aliishia kutoa shukran za teuzi kwa nafasi mbalimabli za watoto wa waislamu walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika na sio kuleta udini katika serikali kama walivyokuwa wakitaka wao
4. Jamaa alikua na uwezo mkubwa sana wa kuchomeka na kurithisha familia na watoto wake katika nafasi za meza kuu ya nchi lakini hakufanya hivyo na aliwaacha wapambane wenyewe kupitia demokrasia
Ukiachana na Hawa matapeli kama kina Kakobe, Lusekelo, Mwamposa n.k.
J.K Nyerere alikuwa nabii wa kweli Tanzania na unabii wake ulishatimia na wote tumeshuhudia kwa macho