Tanzania kuna familia ambazo zinaishi kifalme bila Watanzania kuzifahamu au wamepiga kimya tu

Tanzania kuna familia ambazo zinaishi kifalme bila Watanzania kuzifahamu au wamepiga kimya tu

Mkuu,

Tatizo kubwa watu hawataki kuona uhalisia huu.

Halafu, watu wanatakiwa kujua Wanasiasa wote Ni Wale wale. Hakuna MALAIKA.

Hata ikitokea CCM ikatoka madarakani, kitakachoendelea Ni jina la chama tu, ila watu Ni wale wale.

Lowassa wa CCM ndiyo yule yule wa CDM.

Bible inasemq, palipo na mzoga ndipo wakusanyikapo TAI.

Chama chochote kitakachokuja kuingia madarakani, hata iqe CHAUMA huko huko ndiko wazee wa FURSA watakakohamia, maana kuhama Vyama Ni demokrasia na haki yake.

Kwahiyo, utakuwa Hawa watu unaokesha unatukana kumbe sababu wako CCM au chama usichokipenda na siyo kwamba wanachofanya hukipendi
Unataka kusema hata tukiwapa chadema bado mambo kama haya yataendelea kuwepo?
 
Anyway, huwezi kutumia nguvu zako zote akili na maarifa kupigania maslahi ya mwanasiasa kuliko yako halafu ukaanza kushangaa kwanini mwanasiasa anafanikiwa kuliko wewe.

Unamsindikiza mwanasiasa kwenda kuchukua fomu ya kugombea

Unaenda kumsikiliza kwenye kampeni zake na kumsifia muda wote 24/7.

Unamchangia pesa.

Unaenda kumpigia kura. Halafu unabaki kituoni mpaka atangazwe kushinda.

Wasipomtangaza kashinda unaandamana na kupigwa ukishinikizwa atangazwe ameshinda.

Kwa hali hiyo unashaangaaje mwanasiasa kufanikiwa kuliko wewe?
Mkuu umeongea kweli kabisa, wabongo tunapigania masilahi ya wanasiasa kuliko masilahi yetu na wakati huo wanasiasa wanapigania masilahi yao kuliko ya kwetu.

Wanasiasa wakikutana na rais mengi wanayoomba ni ya masilahi yao kuliko ya wananchi.
 
Watasema unawivu..😂
Ofcoz ni wivu tu babake alikuwa wapi wakati wenzake wanafanya siasa ye alikuwa busy kusaka mademu. Sasa hivi analaumu baba za watu wengine.

Badala ya Sasa nae kuingia kwenye siasa ili wanae wale bata anaendelea kulaumu tu na wanae watalalamika hivyohivyo tu.

Anza sasa kama vipi it's never too late.
 
Wananchi gani waliopiga kura?. Mpaka sasa kuna watu mnaamini bado kuna haki inatendeka kwenye sanduku la kura Tanzania hii?
Watu bado wana imani na sanduku la kura ndio maana wamekuwa bado wanaenda kupanga foleni kupiga kura, wenyewe wanaona uchaguzi wa 2020 ndio kulikosekana haki.
 
Ridhiwani Kikwete-mbunge na waziri
Mama-Mbuge
Baba-Rais Mstaafu


Husein Mwinyi-Rais Zanzibar
Baba-Rais Mstaafu Tanzania
Dada-Rais Tanzania Bara

SSH-Rais Tanzania
Baba-Rais mstaafu Tanzania
Mtoto-Mbunge Zanzibar
Mkwe-Mbunge na Waziri Tanzania Bara


CCM ni kama ukoo wa Panya yani Baba-Mwizi
Mama-Mwizi
Babu-Mwizi
Bibi-Mwizi
Watoto-Wezi
wakwe-wezi
Mashemeji-wezi
Mawifi-Wezi
Mjomba-Mwizi
Wajukuu- Wezi
Vilembwe-Wezi
Tutapataje maendeleo kwa hii Module?
 
Ofcoz ni wivu tu babake alikuwa wapi wakati wenzake wanafanya siasa ye alikuwa busy kusaka mademu. Sasa hivi analaumu baba za watu wengine.

Badala ya Sasa nae kuingia kwenye siasa ili wanae wale bata anaendelea kulaumu tu na wanae watalalamika hivyohivyo tu.

Anza sasa kama vipi it's never too late.
Na kwa Tanzania nafasi ya uongozi inatafsirika ni ulaji, utasikia mtu anasema Mwigulu ana mganga mzuri ndio maana amechaguliwa tena kwahiyo issue sio kuwa na sifa za uchapakazi na kuwatumikia wananchi.
 
Unataka kusema hata tukiwapa chadema bado mambo kama haya yataendelea kuwepo?
 
Mkuu umeongea kweli kabisa, wabongo tunapigania masilahi ya wanasiasa kuliko masilahi yetu na wakati huo wanasiasa wanapigania masilahi yao kuliko ya kwetu.

Wanasiasa wakikutana na rais mengi wanayoomba ni ya masilahi yao kuliko ya wananchi.
Rais sio mwanasiasa?
Kwa nini anaombwa?
 
Halafu kapuku kama mimi huku sina hata kakiwanja ili nijenge.Nipo hapa nahangaika kujichanga walau nipate sehemu nijenge aisee.

Mwenye mawasiliano ya brother Riziwan tafadhari. Mungu amsaidie moyo wa kutoa anisaidie nipate tu ardhi na wala si pesa.Ili niweze kulima na kujenga hapo.

Najua anao uwezo wa kunisaidia maana ndo naibu huko
 
Unakuta kwenye familia moja baba ni Rais mstaafu, mama ni mbunge na mtoto ni mbunge na ni naibu waziri, hii familia inahitaji shamba kwa ajili ya kulima chochote au ni kuitegemea serikali tu?

Familia nyingine unakuta baba ni Rais mstaafu, Mtoto ni Rais na Watoto wengine wawili ni wabunge hii familia bila serikali inaweza kuishi?

Familia nyingine mama ni Rais , mtoto ni mbunge na mkwe ni mbunge na ni waziri.

Huu mfumo umekaa sawa au nimekuelewa tofauti?
Ndiyo màana Mbowe kila siku anasema," Mi naona wivu sana. Tusaidiane tuiondoe CCM madarakani."
 
Peace of mind huwa haipatikani kwa kuwa na Mali wala nyadhifa !! Hicho ndicho kinachowatesa watu !!
Uliona wapi kuna Peace of mind mahala ambako njaa inauma? Hela hamna hio peace of mind inatokea wapi!?
 
Sasa kama wewe Chokoraa hata baba yako ajulikani ?utafananaje na watoto wa Ndesamburo,Mwinyi,Kikwete,Karume au Mbowe.
 
Hasa ndugu zetu wa dhehebu hili wanatabia ya kutokutosheka.Japo huwa wa....
 
Usisahau na kutoa mfano yule mzee wa dhehebu lile aliyepewa zawadi tofali la dhahabu, akajimilikisha migodi na nyumba za umma 😀
Nchi hii....
Hasa ndugu zetu wa dhehebu hili wanatabia ya kutokutosheka.Japo huwa wa....
 
Jamaa kanichekesha saana
Mimi hapa sina la kusema, ila TANZANIA 🇹🇿 kuna MAMBO! Tena sio madogo, ni MAMBO MAKUBWA sana.

Mengine inabidi tuyaache kama yalivyo, maana ukishughulika nayo unaweza kupata UGONJWA WA PRESHA.

WATU WA TANGA huwa wana msemo unaosema hivi - MWENYEZI MUNGU ana SHANI yake, humpa amtakaye na kumnyima amchaguaye.

Kwahiyo, aliyejaliwa kajaliwa na RIZIKI ni MAFUNGU SABA na kila MTU atapata RIZIKI yake aliyoandikiwa na MWENYEZI MUNGU, hata kama iko NYUMA 🙏🏽.
 
Fred Lowassa ni mbunge wa Jimbo la monduli. Kaachiwa jimbo na baba yake.

Hali hii mwisho italeta changamoto kwenye jamii isipodhibitiwa.
Kitu chochote kama MTU alikipata kwa hila iwe ni Mali au nyadhifa hatopata peace of mind katika maisha yake yote !ndio maana wanasiasa wengi hata wakiwa na Mali nyingi sana bado huwa hawajiamini kuishi nje ya siasa !!
 
Back
Top Bottom