Tanzania kuna familia ambazo zinaishi kifalme bila Watanzania kuzifahamu au wamepiga kimya tu

Abdulla Ali Mwinyi: Ninagombea nafasi ya Naibu Spika, tuziache mamlaka husika zitimize taratibu kisha Wabunge wapige kura——Yale yale tunayoyasema​

 
Ukweli uliosema unatatizwa na Aina ya mifano yako Tu, bila shaka unaongozwa na hisia Fulani hasi Sana dhidi ya watu hao.....hayo mengine umetafuta Tu namna ya kuingilia. Imepangwa hivyo na Mola na itabaki hivyo Hadi atakapoamua mwenyewe lkn si Kwa sababu ya kuchukia Tu watu fulani. Poleni sana
 
Unauhakika?yaani MTU yupo madarakani Kwa Miaka 22 alafu familia yake ibaki kuwa masikini?kuna vitu bado hatujui nchi hii.
 
Keki ya taifa huliwa na wachache. Hii ndio kanuni ya maisha.
 
Keki ya taifa huliwa na wachache. Hii ndio kanuni ya maisha.
Haya maneno yaongee mwaka 2025.
Wakati wa uchaguzi keki ya Taifa ni kwa wote, baada ya uchaguzi keki ya taifa huliwa na wachache
 
Unauhakika?yaani MTU yupo madarakani Kwa Miaka 22 alafu familia yake ibaki kuwa masikini?kuna vitu bado hatujui nchi hii.
Kwa ulimwengu huu wa kidigitali katika sayansi na technolojia tungekua tushaona au kujua mkuu familia ile hamna hata balozi aliewakilisha Burundi au Malawi

Kwa harakaharaka tu mfano Nyumba ya Kikwete pale Mikocheni Regent na Nyumba ya Mkapa pale seaview zote ni Nzuri kuliko ya Nyerere pale sasani sijui umenielewa

Pamoja na kuwa zote zimekarabatiwa kuendana na mazingira ya kisasa lakini utaiona ya Nyerere ni ya kawaida sana

Hivyo ni kwa vinavyoonekana kwa macho tu
 
Wewe ndiyo umeguswa mpaka umechanganyikiwa,wewe hujui kila struggle ina starling Mandela alivyopiganiwa ni ndugu zake tu,waliomchangia nyererere kwenye kesi ni ndugu zake,struggle ya skua gang kutawala milele icon wao si mna wajuwa,ndugu kila struggle ina icon wake
 
ROBERT HERIEL aliwahi kusema hapa jeiefu kuwa..

Hata baba yako mleta uzi alikuwa n nafasi ya kufika hapo walipofika hao,,, na angepewa wanavyopewa...

So hizo ni rewards za jasho lao na sacrifices walizofanya kufika hapo walipo,, Life is not fair na halitakuja kuwa fair hata siku moja...

-mwisho wa kunukuu-

So Mkuu acha wivu.. Hao wanakula matunda ya juhudi zao.
 
Sasa udaktar wa mil 2 una ufalme gani na wewe🤣
 
Mnaosema katiba mpya itaondoa hili suala ni wajinga watupu, wapumbavu na malofa. Bila kujuana hakuna kula hiyo keki ya taifa CCM wala upinzani. Hapo upinzani wanaofaidi ni ndugu au watu wa karibu wa vigogo wa upinzani. Kwa mfano Lema katoka kijiji kimoja na Mbowe na wana undugu. Zitto alishikwa mkono na marehemu Sita. Wale Covid19 karibu wote utakuta kama sio mke au hawara wa kiongozi basi ni ndugu. Mi naona kama huwezi kutafuta connections zako mwenyewe zikaja kuwabeba kizazi chako basi kubali tu hizo familia ndo ziko hivyo na wanapambana kutoachia nafasi.
 
Iko hivyo.

Walionacho wanapambana kukilinda na wasiokuwa nacho wanapambana wakipate.
 
Utapewa kesi ya uhujum uchumi mkuu ohoo.. hutakiw kuhoji
 
Sawa mkuu wacha tuendelee kupigania haki na masilahi ya wanasiasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…