Tanzania kuna tatizo very serious kuhusu hiki tunachokiita mahusiano hasa ya ndoa, tumekosea wapi? Nini kifanyike?

Tanzania kuna tatizo very serious kuhusu hiki tunachokiita mahusiano hasa ya ndoa, tumekosea wapi? Nini kifanyike?

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2010
Posts
60,050
Reaction score
104,466
Wanajukwaa Mimi binafsi ni mfuatiliaji mzuri wa mambo mengi tu, mpaka nimeleta Uzi huu nimejiridhisha kuna tatizo sehemu au kuna kitu sisi binadamu au niseme Watanzania kuna sehemu tumekosea, sitaki kuhusisha dini labda Mungu tu ndio tumuhusishe.

Katika utafiti wangu usiyo rasmi nimeshuhudia watu waliokosa connection na kujikuta na hali ngumu kiuchumi ndoa zao zimekuwa ndowano, labda nikajidanganya hawa tatizo ni pesa tushauriane kutafuta pesa, kumbe nilikuwa najidanganya mwenyewe.

Mimi Kwa nafasi yangu katika jamii najichanganya na watu wa hadhi zote, nimekuja kubaini kumbe hata matajiri, hapa namaanisha matajiri kweli siyo kumiliki gari na nyumba, wote wana matatizo makubwa kwenye ndoa zao, na cha kusikitisha tatizo siyo usaliti kwamba wanagongewa wake zao hapana, Bali maelewano hakuna ndani ya nyumba, je tatizo liko wapi? Wanaume tumekosea wapi kuwaelewa wanawake? Iweje asiye na pesa na kwenye mihela wote wana kilio kimoja?

Nimeandika hii thread Leo baada ya kukutana na mwanangu mmoja tumepotezana miaka kibao nilipomuuliza Shemeji anaendeleaje akanijibu tumeshamwagana, Sasa kuanza kujumlisha watu ninaowafahamu wengi wamemwagana na wapendwa wao Tena ukifuatlia hakuna kesi ya usaliti wa ndoa au Mke anagongwa nje nimepata taharuki kubwa sana, tatizo liko wapi? tumekosea wapi ili tunusuru hizi familia ambazo bado hazijasambaratika?

Mimi naamini kuna tatizo sehemu ila sijui tatizo liko wapi ingawa wanawake nawabebesha sehemu kubwa ya lawama katika hili.

Wananzengo, nini kifanyike kunusuru ndoa za kizazi hiki?

N:b, hapa sijahusisha boy friend na girl friends naongelea wana ndoa, tatizo liko wapi?
 
Kisaikoloji Wanawake wanataka mwanaume dikteta, sasa dini na elimu ukiwa navyo huwezi kuwa dikteta. Wanaume madikteta wake zao wamenyooka kwenye reli awaleti hata fyoko, tofauti na sisi madiplomatic. Ukiwa diplomatic uwe na pesa utasumbuliwa usiwe nayo utasumbuliwa pia.
 
Wanajukwaa Mimi binafsi ni mfuatiliaji mzuri wa mambo mengi tu, mpaka nimeleta Uzi huu nimejiridhisha kuna tatizo sehemu au kuna kitu sisi binadamu au niseme Watanzania kuna sehemu tumekosea, sitaki kuhusisha dini labda Mungu tu ndio tumuhusishe.
Kaka shida naiona kuanzia kwenye hizi zama za kileo na mapokeo ya wapenzi au wanandoa

Yaani leo utakuta mke yupo very updated na mambo ya kisasa wakati mme bado yupo nyuma ni hapo sasa mwanzo wa kutoelewana

Ila vile nikikaa na watu wazima kwangu naona wamama wa leo sio sawa na wa zama zile namaanisha hivi

Wa leo heshima hakuna ...
Wa leo dharau pale ukosapo hela ...
Wa leo hawapo na wewe wala kujali nduguzo ila ulicho nacho

Kaka ni shida sana , ila yote kwa yote nahisi chanzo ni wanawake
 
Upagani!
Watanzania wengi ni Wapagani hata kama hawajijui na hawakubali, lkn wamelelewa kwa Imani za kipagani, shida iko hapo.
Upagani umeletwa na Nyerere, mbio za mwenge ni ushirikina unaopaswa kupigwa vita na kila mtu kwenye akili timamu bila kujari itikadi ya vyama na kidini.

Ingawa ukweli uliowazi ushirikina wa mwenge umeletwa na waislamu ndio walimshauri Nyerere kutumia ushirikina huu baada ya kupokea maagizo ya mizimu pale Bagamoyo.

Kwa bahati mbaya Sheikh Yahya Hussein ndio alikuwa mtu wa mwisho kufariki katika wale washirikina 6, waliokwenda Bagamoyo kwenye mbuyu kufanya tambiko na kuikabidhi Tanganyika mikononi mwa shetani, watu wameshindwa kumuhoji akiwa hai.
 
Lengo kuu la tamthilia zote duniani ni kubomoa ndoa thus maudhui karibu yote ufanana zote zinafunya vurugu, ukosefu wa heshima na staha kwa mume, ukosefu mipaka. Akili ya mwanamke ni kukopi na kupaste KILA kitu akionacho kwenye tamthilia na kukipractice kwenye ndoa yake, hapo ndipo crash uanzia hapo.

Hawa madirector wa hizi tamthilia uenda wanajua au awajui bali wanatumika kwenye ajenda hizi za siri. Hakuna mwanamke asiye penda kutazama tamthilia hii ipo duniani nzima. Tamthilia zote kuanzia za kiingereza, korea, kihindi, china, kiswahili nk hazifundishi maadili zaidi ya magomvi, ukali, kufokea mwanaume, jeuri, ubinafsi, nk.
 
Kwa kweli ndoa nyingi chanzo ni wanawake midomo imekuwa mikubwaaa mnooo kwenye nyumba kujifanya wajuaji na wazaz wa wanawake wanachangia pakubwa mnoo kuvunja ndoa za watoto wao me binafsi ndan kwangu kunawaka moto mda wowote kutaripukaa 😂😀
 
Upagani umeletwa na Nyerere, mbio za mwenge ni ushirikina unaopaswa kupigwa vita na kila mtu kwenye akili timamu bila kujari itikadi ya vyama na kidini.

Ingawa ukweli uliowazi ushirikina wa mwenge umeletwa na waislamu ndio walimshauri Nyerere kutumia ushirikina huu baada ya kupokea maagizo ya mizimu pale Bagamoyo.

Kwa bahati mbaya Sheikh Yahya Hussein ndio alikuwa mtu wa mwisho kufariki katika wale washirikina 6, waliokwenda Bagamoyo kwenye mbuyu kufanya tambiko na kuikabidhi Tanganyika mikononi mwa shetani, watu wameshindwa kumuhoji akiwa hai.
Walienda kuonana na shetani mapangoni bagamoyo wazo lilitolewa na magwiji wa fani ya ndumba na ulozi lengo ni kwenda kuomba jinsi ya kuwaondoa wazungu, shetani akawaambia SAwa uhuru mtapata lakini sharti muwe masikini wale wazee wakakubali ndo shetani akawapa mwenge, mmoja wa wazee akatolewa kafara humo humo. Ndio asili ya mwenge na umasikini wa nchi. Na mikoa yote iliyofanya matambiko watu wake uwezo wao wa kufikiri upo chini sana na hawatokuwa na maendeleo japo raslimali kedekede, Lindi, Pwani, Tanga, Tabora. Hii nchi inatakiwa iwe formated upya ya kuvunja Laana zote.
 
Back
Top Bottom