Hii itakuwa miaka ya 1997 kuja juu usajili wa magari ulikuwa bado TZ hapo naona gari lina Namba TZL.... huku Vipanya vya kumwaga City centre
 
ama kweli nahisi kama naota vile!!! hivi hawa na mipango miji mibovu wametoka wapi? kuna watu wa upimaji na ramani humu JF na watu wa NEMC kweli na wala hawaa aibu? duuh,!! naona bendera ya Tanganyika kwa mbaaali naitamani. yaaani.
 



nina wasi wasi kama picha hii imepigwa ENZI HIZO, inawezekana imepigwa siku ya siku ambayo watu ni wachache, check hata mlima kilimajnaro barfu ilivyokwisha, enzi hizo kipara chote cheupe, barafu tupu... mmmmh
hii picha siya zamani,hizo cruizer ni 98 hivi,defender gari ya 2000+,caldina 1998,baloon 94+,tangazo la picha ya ccm ukutani ni 2000+,mitambo ya simu za mkononi juu ya ghorofa,tangazo la celtel ukutani
 


Hii itakuwa miaka ya 1997 kuja juu usajili wa magari ulikuwa bado TZ hapo naona gari lina Namba TZL.... huku Vipanya vya kumwaga City centre

No!!!hii picha ya 2005+,hii toyota land cruizer hpo posta bank ni gari za 2004 kuja juu,posta bank kuna tangazo la western union,gari za mwenge toyota costa zimeanza kuuingia miaka ya karibuni
 
Important to note: Enzi hizo hakuna gabbage inaonekana mitaani, siku hizi road drainage ndio dampo; mifuko ya plastic kila mahali utadhani mapambo.
 
Kinachonivutia sana kuhusu picha hizi ni usafi wa miji na mazingira enzi hizo. Hebu wekeni picha za sasa kama hamkuona maji ya choo yanavyotiririshwa kwenye mifereji ya barabara za mijini na madampo kibao katikati ya miji. Halafu miji imepambwa kwa mifuko ya plastiki nyeusi. Kunguru wezi weusi ndio wanapamba miji badala ya njiwa ishara ya amani.
 
Huwezi kufananisha tandale ya enzi hizo na ya sasa
 
Hapo ni Mnazi mmoja Mji mtulivu na mwanana hata Zebra cross ilikuwa km ya futi sita tu mnavuka kwa raha hapo mtaa wa Lumumba
View attachment 80986



Hapo mnazi mmoja magari machache na taa zilikuwa zinafanya kazi hao wanaovuka kulia na Pijot 404 inaoneka kwa nyuma kulikuwa na Hotel inapika Bilyan Tamu sana... kwa sasa kuna maduka na mjengo wa Benki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…