Tazama ushahidi huu wa kimahesabu wa Michango ya Lissu Unaothibitisha CHADEMA haifikishi wanachama hata million Moja

Tazama ushahidi huu wa kimahesabu wa Michango ya Lissu Unaothibitisha CHADEMA haifikishi wanachama hata million Moja

Nyie UWT ni lini mlichangia ndani ya siku 2? CDM wanataka haki, nyie huwa mnachangisha wakuu wa idara na taasisi pamoja na wafanyabiashara kwa nguvu
CCM hata ikitaka keshi ya Billion moja inaweza kupata ndani ya siku moja tu tena kwa saa chache. Maana watu wanaoipenda CCM na kuwa na utayari wa kuichangia kwa hiyari ni wengi sanaa.
 
Anashindwa kutofautisha chama kinachoendeshwa na mfuko wa serikali 100% (CCM) na chama kinachojikongoja chenye (vyama vilivyobaki vya siasa ikiwemo CDM).
Yaani kutoa mchango wa mia tano au buku kumchagia Lissu imekuwa nongwa na mabishano makali.kwanini mnakuwa na mioyo migumu kiasi hicho?
 
Yaani kutoa mchango wa mia tano au buku kumchagia Lissu imekuwa nongwa na mabishano makali.kwanini mnakuwa na mioyo migumu kiasi hicho?
Naona nabishana na kichaa.
Embu endelea na ujinga wako hasara kwa jamii kwa hizi akili zako.
Usinipotezee muda.
 
Nahisi kichwani una matatizo ya kifikra jamaa.
Kwahiyo ushaniweka CHADEMA kwa kuchangia uzi na kutoa maoni!?
Je kila anayehudhuria kanisani hutoa sadaka!?
Embu nipe jibu ya hilo swali kwanza,maana cocept ndogo tu washindwa kuing'amua.
Wapo wanachama walioona kuna manufaa kuchangia ila wapo wanachama walioona kuwa hilo jambo la gari la Lissu limekaa kibinafsi zaidi.
Tumia ubongo wako vizuri kijana/mzee.
Kwa hiyo kipi ni kipi? Je mmeweka mgomo wa kumchangia Lissu au hamna wanachama.maana hueleweki kabisa ewe mwanachadema uliyejaa msongo wa mawazo kichwani mwako. Maana naona umeanza hadi kuhusisha mambo ya kanisani. Kwa hiyo chama Chenu ni tawi la kanisa?
 
Naona nabishana na kichaa.
Embu endelea na ujinga wako hasara kwa jamii kwa hizi akili zako.
Usinipotezee muda.
Leo ni moto juu ya moto mpaka akili zinewarukeni kichwani. Mna wanachama hai wangapi? Maana inaonyesha hata laki tano tu hamgiki kati ya mamilioni ya watanzania waliopo.
 
Kwa hiyo kipi ni kipi? Je mmeweka mgomo wa kumchangia Lissu au hamna wanachama.maana hueleweki kabisa ewe mwanachadema uliyejaa msongo wa mawazo kichwani mwako. Maana naona umeanza hadi kuhusisha mambo ya kanisani. Kwa hiyo chama Chenu ni tawi la kanisa?
Nakuelekeza mara ya mwisho kijana pia uwe na uelewa.
Mie sio mwanachama wa chama chochote bongo,elewa hilo kwanza.
Pili idadi ya watu waliochangia sio kipimo halali cha idadi ya wafuasi kwasababu wapo wanachama waliolichukulia hili jambo kuwa ni la kibinafsi zaidi,wapo ambao waliotamani kumchangia ila kwasababu za kiuwezo wakashindwa hali ngumu.
Na wapo walioliona lina umuhimu na wakachangia,watu hamuwezi kuwa na mawazo sawa.
Ndio maana nikakuuliza je,wanaoingia kanisani wote hutoa sadaka?
Je ambao hawajatoa kwasababu zao tofauti ndio tuwatoe kuwa hao sio waumini!?
Unaelewa maana ya mifano!?
Au shule ulikimbia wewe!?
Kama hujaelewa hili usini quote tena unanipotezea muda kujibizana na wewe na unaongea upuuzi.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Michago ya kumchangia Lissu Fedha za kununulia Gari imewaumbua sana CHADEMA, imewapa aibu,fedheha ,imewavua nguo hadharani na imeonyesha na kuthibitisha kauli yangu nayosemaga humu jukwaani kuwa CHADEMA imepuuzwa na inaendelea kupuuzwa na mamilioni ya watanzania kila uchwao.

Michago inayoendelea kuchangwa imeonyesha CHADEMA haina wanachama hai hata million moja tu.imeonyesha CHADEMA huwa wanapika takwimu ili kuwapofua macho na akili wafuasi wake kiduchu na wafadhili wao. Sasa kwa sasa tangia michango imeanza kuchangwa kwa ajili ya Lissu, CHADEMA na wana CHADEMA mpaka muda huu wameshindwa kufikisha millioni 30.

Sasa tizama mahesabu haya kutoka kwangu Mwashambwa Lucas kada kindaki Ndaki wa CCM.

Kama CHADEMA ingekuwa na walau wafuasi na wanachama hai hata laki tano Tuuuu yaani 500,000 na kila mwanachama akachanga walau elfu moja tu maana yake mpaka sasa ingekuwa imepatikana Million mia tano keshi. Yaani

500,000×1000= 500,000,000/=

je pesa hizi zisingetosha kununua gari analolitaka Lissu na chenji kubaki??

Kama CHADEMA ingekuwa na wafuasi Million moja na kila mtu akachanga walau shilingi mia tano maana yake ni kuwa bado Lissu angepata millioni mia tano keshi.

Sasa hao mamilioni ya wanachama ambao CHADEMA huwa inasema inao wengi kuliko wana CCM wapo wapi? Wamejificha wapi? Hawajaona na kusikia kuwa Lissu anahitaji na kuomba walau hata miatano tu? Ikumbukwe kuwa CHADEMA huwa wanasema wana wanachama zaidi ya millioni kumi.

Sasa kama kati ya wanachama zaidi ya milioni kumi wanashindikana kupatikana hata wanachama laki tano tu wa kuchangia elfu moja tu ili kupata million mia tano.je hamuoni kuwa chama hiki kinapika takwimu mara nyingi?

Hata zile kura alizopata Hayati Lowassa mwaka 2015,zilitokana na mgawanyiko uliotoka ndani ya CCM katika upatikanaji wa mgombea Urais. Hata katika ngazi ya ubunge mahali popote pale wanapopata ubunge CHADEMA huwa ni kura za wana CCM wenzetu wanaokuwa wamegawanyika nakupiga kura za hasira kwa upinzani kama sehemu ya kutoridhishwa wakati mwingine na jina linalokuwa limerejeshwa na vikao vya juu.

Lakini kama sisi sote Wana CCM Pamoja na mashabiki wetu na wakereketwa na wanachama kindaki ndanki tukiamua kupigia kura wagombea wetu,nawahakikishia CHADEMA na upinzani wote kuwa hakuna kiti kinachoweza kwenda upinzani kuanzia mwenyekiti wa kitongoji hadi ngazi ya Urais. Upinzani hauwezi kuambulia chochote kile.

Na kwa sasa wale Wana CCM wachache waliokuwa wanapiga kura za hasira kwa upinzani hasa CHADEMA wamejifunza na kujutia makosa yao kwa machozi na maumivu makali sana.wametambua kuwa walikuwa wanajikomesha wenyewe na siyo chama.maana wameona upinzani kazi yao ni kupinga kila kitu na kila jambo pasipo kumpigania mwananchi kwa lolote lile. Kwa hiyo huu mserereko na mteremko waliokuwa wakipata CHADEMA kwa sasa wasahau kabisa kuupata.maana kila mwana CCM amejilia kiapo cha kuipa kura ya ndio CCM Katika kila ngazi ya uchaguzi.

Naweka kalamu yangu chini na kuishia hapa. CHADEMA njooni Nataka tubishane kwa hoja na siyo makelele na matusi. Weka hesabu nami niweke hesabu. Weka takwimu nami nishushe nondo za uhakika. Raha ya CCM Ni kubishana kwa hoja na siyo matusi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kwamba kila mwanachama wa Chadema atachangia Gari kilazima?
Au kila mwanachama wa Chadema amefikiwa na hili tangazo?
 
wanachama wengi wa chadema ni wasomi na wachumi sio mazezeta kama wa ccm,mtu unaambiwa mnunulie rais form unanunua wakati huna uhakika wa dagaa wa mwanza wa 200 na dona mtu unakiduchu afu huyo aliyesababisha uwe nakiduchu hicho anakuja kukunyang'anya kidogo ulichonacho kwa gia ya kujiliza ili aonekane analia lugha moja na watanzania huo ni unafiki
 
Leo ni moto juu ya moto mpaka akili zinewarukeni kichwani. Mna wanachama hai wangapi? Maana inaonyesha hata laki tano tu hamgiki kati ya mamilioni ya watanzania waliopo.
We una uhakika gani kama mimi Chadema!?
Mie sina raisi hapa bongo na sishabikii siasa.
Umeleta mjadala watu wajadili,kwahiyo kila anaejadili huu mjadala ni mfuasi wa siasa!?
😂😂😂😂Aisee kweli ni ngumu kushinda mjadala dhidi ya mtu mwerevu ila ni karibia na haiwezekani kushinda mjadala dhidi ya mpumbavu(Lucas mwashamba).
 
wanachama wengi wa chadema ni wasomi na wachumi sio mazezeta kama wa ccm,mtu unaambiwa mnunulie rais form unanunua wakati huna uhakika wa dagaa wa mwanza wa 200 na dona mtu unakiduchu afu huyo aliyesababisha uwe nakiduchu hicho anakuja kukunyang'anya kidogo ulichonacho kwa gia ya kujiliza ili aonekane analia lugha moja na watanzania huo ni unafiki
Kwa hiyo mmegoma kumchangia Lissu hela baada ya kugundua anakula sana michango yenu?😃😃😃
 
CCM hata ikitaka keshi ya Billion moja inaweza kupata ndani ya siku moja tu tena kwa saa chache. Maana watu wanaoipenda CCM na kuwa na utayari wa kuichangia kwa hiyari ni wengi sanaa.
Mkapa kwenye kitabu chake alikiri kuiba 130B ajili ya uchaguzi wa 2005 kutoka kwenye fedha za umma, nyie ni majangili tupu, CCM kuanzia Wilaya kwenda juu wanatumia mafuta na posho za serikali kwa matumizi ya chama mpk matengenezo ya magari. Jinga kabisa chama kimeja majizi tupu na matapeli
 
Kwamba kila mwanachama wa Chadema atachangia Gari kilazima?
Au kila mwanachama wa Chadema amefikiwa na hili tangazo?
Kwa hiyo unamaanisha kuwa mpaka sasa wanachama wa CHADEMA hawajafikiwa na tangazo na ndio maana michango inachechemea? Kama jibu ni hilo basi wafuasi na wanachama wenu hawapo Tanzania na hawanamsaada wowote kwenu na kuna uwezekano wanaishi ardhini ndio maana hawajui kinachoendelea huku Duniani.na ndio maana michango imekuwa migumu sana kutoka.
 
Mkapa kwenye kitabu chake alikiri kuiba 130B ajili ya uchaguzi wa 2005 kutoka kwenye fedha za umma, nyie ni majangili tupu, CCM kuanzia Wilaya kwenda juu wanatumia mafuta na posho za serikali kwa matumizi ya chama mpk matengenezo ya magari. Jinga kabisa chama kimeja majizi tupu na matapeli
Sasa kwanini mmeshiindwa kuchanga hata mia tano tu ili kiongozi wenu apate gari?
 
Back
Top Bottom